Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, samani na nyaraka muhimu zilizokuwa katika ofisi ya mbunge wa Nyamagana, jijini Mwanza, ikiwemo picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete, 'zimetoweka'.
Kutoweka kwa samani hizo zilizogharimu fedha nyingi kutoka ofisi ya Bunge kulibainika jana baada ya mbunge mpya wa Nyamagana, Ezekiel Wenje (CHADEMA), kuingia rasmi kwa ajili ya kuanza kazi.
Alisema, samani hizo zimeibwa katika kipindi cha siku mbili za hivi karibuni kwa kuwa aliwahi kufika kwenye ofisi hizo na kuzikuta baada ya kutoka bungeni.
"Niliwabana viongozi ngazi ya wilaya na mkoa wanieleze vimeenda wapi hivi vitu… niliambiwa eti vilinunuliwa na mtu binafsi na havikuwa mali ya serikali," alisema mbunge huyo.
"…Ofisi ya mbunge ni mali ya umma kama ilivyo Ikulu (Ofisi ya Rais), fedha za walipakodi zinatumika kugharamia; sasa hivi vitu nani kaviiba?" alihoji Wenje kwa masikitiko.
Kutoweka kwa samani hizo zilizogharimu fedha nyingi kutoka ofisi ya Bunge kulibainika jana baada ya mbunge mpya wa Nyamagana, Ezekiel Wenje (CHADEMA), kuingia rasmi kwa ajili ya kuanza kazi.
Alisema, samani hizo zimeibwa katika kipindi cha siku mbili za hivi karibuni kwa kuwa aliwahi kufika kwenye ofisi hizo na kuzikuta baada ya kutoka bungeni.
"Niliwabana viongozi ngazi ya wilaya na mkoa wanieleze vimeenda wapi hivi vitu… niliambiwa eti vilinunuliwa na mtu binafsi na havikuwa mali ya serikali," alisema mbunge huyo.
"…Ofisi ya mbunge ni mali ya umma kama ilivyo Ikulu (Ofisi ya Rais), fedha za walipakodi zinatumika kugharamia; sasa hivi vitu nani kaviiba?" alihoji Wenje kwa masikitiko.