Habari ambayo imeenea hivi sasa kwenye mitandao ya kijamii ni kukamatwa kwa masanduku yenye kura feki! Wengi wetu tunaamini huu ndio mwanzo tu wa lile bao la mkono ambalo tulipata kusikia likihubiriwa! Pamoja na yote hayo, je hivi ni kweli tunafahamu malengo ya hayo masanduku?
Kila kituo kina ulinzi na mawakala wa vyama! Now assume Kituo X chenye mlinzi na mawakala wa vyama vyote. Hivi ni kipi ambacho ni rahisi kati ya kununua mawakala wa vyama hasimu AU kuingiza mi-box mikubwa yenye kura feki kinyemela-- mi-box ambayo inaonekana wazi na mtu yeyote? Hizi kura hazipigwi gizani... na kabla kituo cha kupigia kura hakijafunguliwa na upigaji kura kuanza, eneo zima linakaguliwa ikiwa ni pamoja na chumba chenyewe. Sasa haya masanduku yenye kura feki yanaingiaje humo hadi kura zake kujumlishwa pamoja na kura zingine halali?Ikiwa hawa mawakala wetu watashindwa kuyaona masanduku yenye kura feki yakiingizwa kwenye masanduku halali; je kweli wataweza kuona uhesabuji wa kura zilizo halali? Kisheria, kabla ya idadi ya kura zilizopigwa kutangazwa; mawaka wa vyama vyote wata-sign kuafikia wa kura hizo... je, hizo kura feki zilizo kwenye masanduku zitasainiwa na mawakala gani?!
Kama issue ni kura, ni kwanini basi mtu asiweke hizo kura feki kwenye bahasha na kwenda kuzipenyeza kupitia wahusika waliohongwa kwenye kituo husika badala ya kupita na masanduku ambayo popote utakapotia mguu yataonekana?
Kwenye media moja ya nje imeandika; bila kujali nani atashinda kwenye uchaguzi huu; lazima machafuko yatatokea! Watu tukaichana live ile media lakini kwa mtindo huu ni kweli machafuko yanaweza kutokea! Watu hatutaki kuangalia uwezekano mwingine wa matukio haya ambayo ukiangalia kwa makini wala hayana nia ya kuiba kura bali kuvuruga uchaguzi na hatimae kuleta maafa akilini! Sina shaka zipo njia mzuri tu za kuiba kura lakini ni mwendawazimu peke yake ndie anaweza kuiba kura kwa kuingiza masanduku feki ambayo yanaweza kuonekana yeyote! Narudia... kama lengo ni ku-tally kati ya hard votes/karatasi za kura na idadi itakayoandikwa, bado kuna better way ya kufanya hivyo badala ya kutembea na masanduku barabarani! Na kama ikiwa ni kweli hayo masanduku yanakamatwa mengine yakiwa kwenye magari; hao wanaokamata wanajuaje kwamba hayo magari yamebeba ma-box kama sio hao wabebaji wali-stage ili wakamatwe? Na ikiwa wali-stage ili wakamatwe; kwanini walitaka wakamatwe kama sio kudhihirisha kwamba walibeba masanduku ya kura?
Kila kituo kina ulinzi na mawakala wa vyama! Now assume Kituo X chenye mlinzi na mawakala wa vyama vyote. Hivi ni kipi ambacho ni rahisi kati ya kununua mawakala wa vyama hasimu AU kuingiza mi-box mikubwa yenye kura feki kinyemela-- mi-box ambayo inaonekana wazi na mtu yeyote? Hizi kura hazipigwi gizani... na kabla kituo cha kupigia kura hakijafunguliwa na upigaji kura kuanza, eneo zima linakaguliwa ikiwa ni pamoja na chumba chenyewe. Sasa haya masanduku yenye kura feki yanaingiaje humo hadi kura zake kujumlishwa pamoja na kura zingine halali?Ikiwa hawa mawakala wetu watashindwa kuyaona masanduku yenye kura feki yakiingizwa kwenye masanduku halali; je kweli wataweza kuona uhesabuji wa kura zilizo halali? Kisheria, kabla ya idadi ya kura zilizopigwa kutangazwa; mawaka wa vyama vyote wata-sign kuafikia wa kura hizo... je, hizo kura feki zilizo kwenye masanduku zitasainiwa na mawakala gani?!
Kama issue ni kura, ni kwanini basi mtu asiweke hizo kura feki kwenye bahasha na kwenda kuzipenyeza kupitia wahusika waliohongwa kwenye kituo husika badala ya kupita na masanduku ambayo popote utakapotia mguu yataonekana?
Kwenye media moja ya nje imeandika; bila kujali nani atashinda kwenye uchaguzi huu; lazima machafuko yatatokea! Watu tukaichana live ile media lakini kwa mtindo huu ni kweli machafuko yanaweza kutokea! Watu hatutaki kuangalia uwezekano mwingine wa matukio haya ambayo ukiangalia kwa makini wala hayana nia ya kuiba kura bali kuvuruga uchaguzi na hatimae kuleta maafa akilini! Sina shaka zipo njia mzuri tu za kuiba kura lakini ni mwendawazimu peke yake ndie anaweza kuiba kura kwa kuingiza masanduku feki ambayo yanaweza kuonekana yeyote! Narudia... kama lengo ni ku-tally kati ya hard votes/karatasi za kura na idadi itakayoandikwa, bado kuna better way ya kufanya hivyo badala ya kutembea na masanduku barabarani! Na kama ikiwa ni kweli hayo masanduku yanakamatwa mengine yakiwa kwenye magari; hao wanaokamata wanajuaje kwamba hayo magari yamebeba ma-box kama sio hao wabebaji wali-stage ili wakamatwe? Na ikiwa wali-stage ili wakamatwe; kwanini walitaka wakamatwe kama sio kudhihirisha kwamba walibeba masanduku ya kura?