Masaa manne ya kusota bank, NMB Kenyata road ongezeni ubunifu

maramia

JF-Expert Member
Jul 17, 2015
2,030
1,344
Fikiria umeacha kazi zako kwenda benki kutoa pesa kwa ajili ya kununua bidhaa za biashara yako.Huko benki unakuta wateja zaidi ya 100 huku wakiongezeka kadri muda unavyosonga.

Pamoja na kufurika wateja, dirishani kuna wahudumu wawili tu madirisha mengine matatu yakiwa yamefungwa tangu saa nne asubuhi mpaka saa nane hii, benki hii ya tawi la Kenyatta road haina kiti wala fomu za kukaa wateja, ni shida tupu hasa kwa wazee na akina mama wasioweza kusimama kwa muda mrefu.

Hivi kweli benki hizi hazina uwezo wa kuweka benchi au viti kwa ajili ya kukaa wateja wake? Kibaya zaidi hata wale wanaojaribu kuketi nje kwenye msingi wa benki baada ya kuchoka kusimama ndani wanatimliwa ili mradi ni shida tupu.
Ebu NMB Kenyatta road ongezeni ubunifu, kwanini mtu kuja kuchukua au kuweka pesa yake asimamishwe masaa manne bila huduma?
 
Fikiria umeacha kazi zako kwenda benki kutoa pesa kwa ajili ya kununua bidhaa za biashara yako.
Huko benki unakuta wateja zaidi ya 100 huku wakiongezeka kadri muda unavyosonga.
Pamoja na kufurika wateja, dirishani kuna wahudumu wawili tu madirisha mengine matatu yakiwa yamefungwa tangu saa nne asubuhi mpaka saa nane hii, benki hii ya tawi la Kenyatta road haina kiti wala fomu za kukaa wateja, ni shida tupu hasa kwa wazee na akina mama wasioweza kusimama kwa muda mrefu.
Hivi kweli benki hizi hazina uwezo wa kuweka benchi au viti kwa ajili ya kukaa wateja wake? Kibaya zaidi hata wale wanaojaribu kuketi nje kwenye msingi wa benki baada ya kuchoka kusimama ndani wanatimliwa ili mradi ni shida tupu.
Ebu NMB Kenyatta road ongezeni ubunifu, kwa nini mtu kuja kuchukua au kuweka pesa yake asimamishwe masaa manne bila huduma?
Karibu CRDB "the bank that listen"
 
Hilo ndio tawi langu la kwanza nilipofungua account yangu ya kwanza mara baada ya kuajiiwa miaka 15 ilyopita, kumbuka wakati huo hakuna kitu kinaitwa ATM, kile nilichokiona pale kuanzia msongamano wa watu, nk. hadi leo halini ile ile.
 
Ebu chekini tulivyozagaa ndani bila utaratibu kama harusi isiyo na Mc.
80b97a8d9ded88c96afa33b927d93a51.jpg
 
Nakumbuka mwaka fulani nilikuwa naumwa lakini nikalazimika kwenda bank (NMB) kuchukua hela. Nilivyofika pale nilikuta foleni ambayo hadi leo sijawahi kukutana nayo popote pale. Nilifika pale saa tatu asubuhi na hadi saa saba mchana nilikuwa niko kwenye foleni bila kumfikia teller. Kuondoka ili kurudi siku nyingine nikawa nashindwa kutokana na shida niliyokuwa nayo. Na wakati huo miguu ilishachoka kusimama. Ikabidi niwaage wateja wenzangu wa mbele na nyuma yangu kwamba niko pembeni kidogo nasubiri foleni isogee. Baada ya kutoka kwenye foleni nikaenda pembeni ukutani nikachuchumaa kwa sababu hakukuwa na mabenchi au viti. Bahati nzuri meneja wa tawi alipita na kunikuta nimechuchumaa na kuniuliza kulikoni. Nikamwambia nimekaa sana kwenye foleni kwa zaidi ya masaa manne na pia naumwa. Alichofanya ni kunipeleka ofisini kwake nikakaa kwenye kiti na yeye akachukua cheque yangu na kunihudumia hadi nikaondoka. Ni siku ambayo sitakuja kuisahau. Kwa kweli NMB foleni zao uwa siyo za kitoto.
 
Nmb mwenzi mzima nataka kujiunga na nmb mobile naambiwa hakuna mawasiliaono yani sijue awana IT Wa network
 
Pole sana nmb hasa Kenyatta road ni shida kwa kweli... Me huwa narudia mlangoni nikiona ule umati wa watu....polen wafanyabiashara mliowekeza nmb..!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nakumbuka mwaka fulani nilikuwa naumwa lakini nikalazimika kwenda bank (NMB) kuchukua hela. Nilivyofika pale nilikuta foleni ambayo hadi leo sijawahi kukutana nayo popote pale. Nilifika pale saa tatu asubuhi na hadi saa saba mchana nilikuwa niko kwenye foleni bila kumfikia teller. Kuondoka ili kurudi siku nyingine nikawa nashindwa kutokana na shida niliyokuwa nayo. Na wakati huo miguu ilishachoka kusimama. Ikabidi niwaage wateja wenzangu wa mbele na nyuma yangu kwamba niko pembeni kidogo nasubiri foleni isogee. Baada ya kutoka kwenye foleni nikaenda pembeni ukutani nikachuchumaa kwa sababu hakukuwa na mabenchi au viti. Bahati nzuri meneja wa tawi alipita na kunikuta nimechuchumaa na kuniuliza kulikoni. Nikamwambia nimekaa sana kwenye foleni kwa zaidi ya masaa manne na pia naumwa. Alichonifanya ni kunipeleka ofisini kwake nikakaa kwenye kiti na yeye akachukua cheque yangu na kunihudumia hadi nikaondoka. Ni siku ambayo sitakuja kuisahau. Kwa kweli NMB foleni zao uwa siyo za kitoto.
Duh mpaka una historia...hahah pole
 
Fikiria umeacha kazi zako kwenda benki kutoa pesa kwa ajili ya kununua bidhaa za biashara yako.
Umeacha kazi zako kwenda kutoa pesa kwa ajili ya kununua bidhaa za biashara yako. Sasa unachukia nini kama umeenda hapo kuvinjari? Maana hukuwa kazini.

Matatizo kama haya yanaendelea kwa vile hatuwezi kudai haki zetu mbele ya wahusika, hutujui kujieleza.

Badala ya kupinga kupotezewa muda unadai upewe kiti au fomu ukae! Sijui fomu ndio nini maisha haya, sijui mkeka?

Badala ya kusema mnakwamisha kazi zangu unasema nimeacha kazi zangu. Basi pumzika na kazi hapo ndani huku ukifanya mazoezi ya kusimama!
 
Unapoenda benki unatarajia kutopoteza muda, Kama ukienda na kupoteza Muda sio sahihi. ATM Zenu zinasumbua sana ndani ni msongamano wa watu, mtandao unasumbua.

NMB mobile sio kabisa mbovuuuu unatuma pesa leo zinafika baada ya siku tatu wakati shida imeisha na nimetafuta alternative ya kufanya.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom