falcon mombasa
JF-Expert Member
- Mar 5, 2015
- 9,159
- 9,241
Wakuu,
Serikali imepiga marufuku daladala kusimamisha na kujaza abiria, taratibu ambao haukuzoeleka sana haswa kwa jiji la Dar.
Mimi nikiwa mmoja wa wamiliki wa daladala hizi naishauri Serikali mambo machache haswa katika kipindi hiki cha mpito kwakuwa Serikali imesema daladala itakayosimamisha abiria itapigwa faini laki Tisa au gerezani miaka miwili ifanye hivi ili kubalance situation.
Mfano daladala ikitoka mbezi hadi Temeke umbali wa kilomita 37 Kila abiria analipa 600 na daladala moja inasiti za abiria 26 hadi 22 akifika temeke anakuwa anapata 15600tsh hadi 13200tsh ambapo kwa umbali huo gari inaweza kutumia lita 5 ambapo ambapo ni sawa na tsh 11000.
Sasa Kama gari hadi inafika Temeke imekusanya 15600 za nauli ukitoa mafuta 11000tsh inamaana daladala hi itabakiwa na 4600.
Sasa kwa namna hii je huyo dereva atapataje hesabu na posho yake ya kila siku, bado kuna zile pesa za kupigia kiwi za jamaa zetu wale aliosema mkuu ambapo kwa siku nzima huenda zikafika 10000 tena hizi huwa hazinaga ubishi lazima utatoa tu.
Ushauri wangu, Serikali ipunguze bei za mafuta kwa daladala zote ikiwezekana iwe na vituo vyake vya mafuta na maduka yake maalumu ya vipuri pia Serikali itafute muda ikae na wadau husika lakini sio kufanya maamuzi bila kushirikiana na wadau watakaoteseka ni wananchi wakawaida wanategemea magari haya.
Serikali imepiga marufuku daladala kusimamisha na kujaza abiria, taratibu ambao haukuzoeleka sana haswa kwa jiji la Dar.
Mimi nikiwa mmoja wa wamiliki wa daladala hizi naishauri Serikali mambo machache haswa katika kipindi hiki cha mpito kwakuwa Serikali imesema daladala itakayosimamisha abiria itapigwa faini laki Tisa au gerezani miaka miwili ifanye hivi ili kubalance situation.
Mfano daladala ikitoka mbezi hadi Temeke umbali wa kilomita 37 Kila abiria analipa 600 na daladala moja inasiti za abiria 26 hadi 22 akifika temeke anakuwa anapata 15600tsh hadi 13200tsh ambapo kwa umbali huo gari inaweza kutumia lita 5 ambapo ambapo ni sawa na tsh 11000.
Sasa Kama gari hadi inafika Temeke imekusanya 15600 za nauli ukitoa mafuta 11000tsh inamaana daladala hi itabakiwa na 4600.
Sasa kwa namna hii je huyo dereva atapataje hesabu na posho yake ya kila siku, bado kuna zile pesa za kupigia kiwi za jamaa zetu wale aliosema mkuu ambapo kwa siku nzima huenda zikafika 10000 tena hizi huwa hazinaga ubishi lazima utatoa tu.
Ushauri wangu, Serikali ipunguze bei za mafuta kwa daladala zote ikiwezekana iwe na vituo vyake vya mafuta na maduka yake maalumu ya vipuri pia Serikali itafute muda ikae na wadau husika lakini sio kufanya maamuzi bila kushirikiana na wadau watakaoteseka ni wananchi wakawaida wanategemea magari haya.