JamboJema
JF-Expert Member
- Jun 14, 2011
- 1,143
- 209
Ijumaa ya Tarehe Mosi mwezi huu wa Julai nilikwenda mpaka wa Tanzania na Uganda eneo la Mtukula. Nikiwa naelekea huko pale maeneo ya Kyaka, kama kilomita 35 hivi toka Mtukula niliyaona maroli mengi yakiwa yamesheheni nafaka mbalimbali yakiwa yamepaki hapo Kyaka.
Nilipouliza kulikoni nikaambiwa magari hayo yalikuwa yakipeleka mazao hayo Uganda lakini mamlaka za Tanzania zimezuia kufanya hivo kwa maelekezo kutoka serikalini kwamba chakula hakiruhusiwi kutoka nje ya nchi kwani kuna njaa nchini.
Ninachoshindwa kuelewa ni kwa nini wakulima wabanwe namna hiyo katika kutumia kilicho chao kihalali? Mbona mfanyakazi hapangiwi aufanyie nini mshahara wake?
Kwa nini mkulima asiachwe kuuza mazao yake kule anakoona kuwa atapata profit na kurudisha gharama zake za kilimo?
Ninavyodhani ni bora, iwapo say, Uganda bei ni kubwa na serikali inania ya dhati kuzuia njaa nchini, basi ichangie gharama ya hicho chakula ili mkulima alipwe sawa na kama angeuza Uganda, na si kumzuia.
Nawasilisha
Nilipouliza kulikoni nikaambiwa magari hayo yalikuwa yakipeleka mazao hayo Uganda lakini mamlaka za Tanzania zimezuia kufanya hivo kwa maelekezo kutoka serikalini kwamba chakula hakiruhusiwi kutoka nje ya nchi kwani kuna njaa nchini.
Ninachoshindwa kuelewa ni kwa nini wakulima wabanwe namna hiyo katika kutumia kilicho chao kihalali? Mbona mfanyakazi hapangiwi aufanyie nini mshahara wake?
Kwa nini mkulima asiachwe kuuza mazao yake kule anakoona kuwa atapata profit na kurudisha gharama zake za kilimo?
Ninavyodhani ni bora, iwapo say, Uganda bei ni kubwa na serikali inania ya dhati kuzuia njaa nchini, basi ichangie gharama ya hicho chakula ili mkulima alipwe sawa na kama angeuza Uganda, na si kumzuia.
Nawasilisha