Inasikitisha sana kuona Serikali yetu inavyowapa wazungu first priority.Wazungu wanatoka kwao wanakimbilia Tz kupata kazi,wakati wenyeji wanapigwa danadana.Ni kweli marubani wa kitanzania sio wengi,kwa sababu kusomea ni ghali sana,karibu mil 80.Wapo waliojitahidi kujisomesha kwa kupitia mikopo,lakini baada ya kurudi hawapewi kazi.Mzungu anatoka kwao,direct from school,akija anapewa kazi.hawa wana lengo moja,kupata uzoefu na masaa then anarudi kwao,kabla hajaondoka anamwita mwenzake.kwa hiyo inakua ni mzunguko.Kitu cha kushangaza ni nani anaetoa hizo work permit.Kumejaa rushwa tupu huko mambo ya ndani,wana njaa kama darfur.Kwa maana hiyo vijana marubani wapo mbioni kuandaa maandamano kupinga ubaguzi huu ndani ya nchi yao wenyewe.makampuni yanaongoza kwa wazungu ni,Coastal Aviation,precesion Air,na Arusha huko zimejaa.Maandamano yatakua ya amani,na yaliodhihinishwa na chama cha marubani tanzania PTPA.,maandamano hayo yataelekea moja kwa moja kwa Rais,magogoni.Vyombo vyote vya habari vitahusishwa.