Lord Diplock MR
JF-Expert Member
- Mar 16, 2015
- 1,393
- 3,234
Msanii wa nyimbo za injili Martha Mwaipaja ambaye ni miongoni mwa wasanii walio karibu sana muimbaji Rose Muhando ameeleza kilichotokea kwa Rose Muhando .
Martha ameeleza jinsi Rose alivyojiingiza kwenye madawa ya kulevya na jinsi alivyolazimika kujihusisha kimapenzi na meneja wake aitwaye Nathani.
Martha anaeleza kuwa vita ya kiroho ilimuelemea Rose Muhando. Rose Muhando ana meneja wake aitwaye Nathan ambaye ndiye aliyemtoa kimuziki mpaka akafahamika. Kiufupi huyo meneja wake ndiye aliyegharamia gharama zote za kurekodi albamu ya kwanza ya Rose Muhando baada ya kuachana na kitimtimu kwaya. Rose Muhando aliingia mkataba na Nathan ambao kwa mujibu wa Martha Mwaipaja ulikuwa ukimkandamiza Rose Muhando na kumnufaisha meneja.
Martha Mwaipaja anayedai amekuwa karibu na Rose Muhando kiasi cha kumueleza kila lililomsibu anatolewa mfano kwamba ili umualike Rose Muhando kwenye show ni lazima uingize milioni mbili kwenye akaunti ya Nathan, halafu laki tano utampatia Rose Muhando atakapokuja kupafomu. Hivyo Rose Muhando akitoka kwenye show anapewa laki tatu kwenye hiyo milioni mbili na inayobaki yote anachukua meneja. Ilifika hatua ikawa meneja akila pesa za watu mbalimbali na kumlazimisha Rose ajaperform na mara nyingine Rose aligoma kwenda na matokeo yake alikuwa akipata lawama za utapeli mara kwa mara.
Martha Mwaipaja anaendelea kueleza kwamba Nathan alitumia nafasi yake ya umeneja kumtumia Rose Muhando kimapenzi pamoja na kuwa alikuwa mume wa mtu. Rose Muhando alijaribu kupambana na hali hiyo lakini mwisho wa siku akajikuta akijihusisha kimahusiano na meneja wake huyo.
Meneja alimtumia Rose Muhando kimapenzi na kiuchumi, kuna kipindi Rose Muhando alipata mchumba mwingine ambaye alitaka kumuoa lakini alikabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa Nathan. Martha Mwaipaja anasema mchumba huyu aliyekuwa rafiki wa karibu wa Masanja mkandamizaji alipata vitisho vikali kutoka kwa Nathan. Yeye Martha na Masanja ndiyo waligeuka wasuluhishi wa kutafuta utatuzi wa hali hiyo. Martha anasisitiza kuwa Nathan hakupenda Rose Muhando aolewe na mtu mwingine, wakati Rose Muhando akiwa amechoka kuzini na Nathan akijitakia ndoa yake mwenyewe. Kuna siku Nathan alimnyoishea bastola kwa muda wa dakika tano akimtishia asimuache kwenda kwa huyo mchumba wake mpya.
Rose Muhando ndiye aliyekuwa akimhudumia mchumba huyu mpya kwani alikuwa na hali duni kifedha. Rose alifikia hatua ya kumjengea nyumba kwao kwa wazazi wa mchumba wake huyu mchumba wake. Kama wahenga wasemavyo bora umfadhili mbuzi utakula mchuzi Rose alimfumania mchumba huyu mpya na mwanafunzi wa shule laivu bila chenga.
Rose Muhando alichanyikiwa na akajikuta amerudi tena na kuangukia kwenye penzi la meneja wake Nathan ambaye ni mme wa mtu.
Martha anasema Rose Muhando alitumikishwa kwa show zisizokoma na ilifika hatua anachoka anaishiwa nguvu anaanguka jukwaani anatolea mfano alivyoanguka madhabahuni kwa Rwakatale. Martha Mwaipaja anasema Rose Muhando alikuwa si mtu wa furaha muda mwingi alikuwa akilia awapo peke yake. Martha Mwaipaja anasema Rose Muhando alimwambia kwa uchungu kuwa anafanya kazi ngumu lakini anawafanyia watu wengine.
Ili kuondoa uchovu na stress kutokana na wingi wa matamasha ambayo Nathan alikuwa ameshakula pesa, Nathan alimlazimisha Rose kunywa vilevi ili akaperform bila kuchoka haraka, Martha Mwaipaja anasema alishuhudia hili kwa macho yake kwenye show ya mwanza.
Ilifika hatua pombe zikawa hazifui dafu ikawa zamu sasa ya madawa ya kulevya, ikafika hatua haimbi tena amekuwa teja na ndiyo hali Rose Muhando aliyonayo sasa.
Martha Mwaipaja anaeleza kuwa Rose Muhando alipoamua kujinasua kwa meneja wake huyo alipata vitisho vikali kutoka kwa Nathan na Msama wa msama promotion waliomtisha kuwa kama ataachana na huyo meneja atapoteana kimuziki.
Martha Mwaipaja anasema tumuombee Rose Muhando badala ya kumhukumu. Waimbaji wa nyimbo za injili wamechukua nafasi ya shetani, shetani ndiye alikuwa kiongozi wa sifa kabla ya kutupwa kuzimu. Hivyo shetani anawawinda sana kwani wamechukua nafasi yake.
NB: Nimeshindwa kuipandisha Audio clip ya Martha Mwaipaja akiongea.
UPDATES
Clip za Martha Mwaipaja akisimulia sakata la Rose Muhando
Part one
Part two
Martha ameeleza jinsi Rose alivyojiingiza kwenye madawa ya kulevya na jinsi alivyolazimika kujihusisha kimapenzi na meneja wake aitwaye Nathani.
Martha anaeleza kuwa vita ya kiroho ilimuelemea Rose Muhando. Rose Muhando ana meneja wake aitwaye Nathan ambaye ndiye aliyemtoa kimuziki mpaka akafahamika. Kiufupi huyo meneja wake ndiye aliyegharamia gharama zote za kurekodi albamu ya kwanza ya Rose Muhando baada ya kuachana na kitimtimu kwaya. Rose Muhando aliingia mkataba na Nathan ambao kwa mujibu wa Martha Mwaipaja ulikuwa ukimkandamiza Rose Muhando na kumnufaisha meneja.
Martha Mwaipaja anayedai amekuwa karibu na Rose Muhando kiasi cha kumueleza kila lililomsibu anatolewa mfano kwamba ili umualike Rose Muhando kwenye show ni lazima uingize milioni mbili kwenye akaunti ya Nathan, halafu laki tano utampatia Rose Muhando atakapokuja kupafomu. Hivyo Rose Muhando akitoka kwenye show anapewa laki tatu kwenye hiyo milioni mbili na inayobaki yote anachukua meneja. Ilifika hatua ikawa meneja akila pesa za watu mbalimbali na kumlazimisha Rose ajaperform na mara nyingine Rose aligoma kwenda na matokeo yake alikuwa akipata lawama za utapeli mara kwa mara.
Martha Mwaipaja anaendelea kueleza kwamba Nathan alitumia nafasi yake ya umeneja kumtumia Rose Muhando kimapenzi pamoja na kuwa alikuwa mume wa mtu. Rose Muhando alijaribu kupambana na hali hiyo lakini mwisho wa siku akajikuta akijihusisha kimahusiano na meneja wake huyo.
Meneja alimtumia Rose Muhando kimapenzi na kiuchumi, kuna kipindi Rose Muhando alipata mchumba mwingine ambaye alitaka kumuoa lakini alikabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa Nathan. Martha Mwaipaja anasema mchumba huyu aliyekuwa rafiki wa karibu wa Masanja mkandamizaji alipata vitisho vikali kutoka kwa Nathan. Yeye Martha na Masanja ndiyo waligeuka wasuluhishi wa kutafuta utatuzi wa hali hiyo. Martha anasisitiza kuwa Nathan hakupenda Rose Muhando aolewe na mtu mwingine, wakati Rose Muhando akiwa amechoka kuzini na Nathan akijitakia ndoa yake mwenyewe. Kuna siku Nathan alimnyoishea bastola kwa muda wa dakika tano akimtishia asimuache kwenda kwa huyo mchumba wake mpya.
Rose Muhando ndiye aliyekuwa akimhudumia mchumba huyu mpya kwani alikuwa na hali duni kifedha. Rose alifikia hatua ya kumjengea nyumba kwao kwa wazazi wa mchumba wake huyu mchumba wake. Kama wahenga wasemavyo bora umfadhili mbuzi utakula mchuzi Rose alimfumania mchumba huyu mpya na mwanafunzi wa shule laivu bila chenga.
Rose Muhando alichanyikiwa na akajikuta amerudi tena na kuangukia kwenye penzi la meneja wake Nathan ambaye ni mme wa mtu.
Martha anasema Rose Muhando alitumikishwa kwa show zisizokoma na ilifika hatua anachoka anaishiwa nguvu anaanguka jukwaani anatolea mfano alivyoanguka madhabahuni kwa Rwakatale. Martha Mwaipaja anasema Rose Muhando alikuwa si mtu wa furaha muda mwingi alikuwa akilia awapo peke yake. Martha Mwaipaja anasema Rose Muhando alimwambia kwa uchungu kuwa anafanya kazi ngumu lakini anawafanyia watu wengine.
Ili kuondoa uchovu na stress kutokana na wingi wa matamasha ambayo Nathan alikuwa ameshakula pesa, Nathan alimlazimisha Rose kunywa vilevi ili akaperform bila kuchoka haraka, Martha Mwaipaja anasema alishuhudia hili kwa macho yake kwenye show ya mwanza.
Ilifika hatua pombe zikawa hazifui dafu ikawa zamu sasa ya madawa ya kulevya, ikafika hatua haimbi tena amekuwa teja na ndiyo hali Rose Muhando aliyonayo sasa.
Martha Mwaipaja anaeleza kuwa Rose Muhando alipoamua kujinasua kwa meneja wake huyo alipata vitisho vikali kutoka kwa Nathan na Msama wa msama promotion waliomtisha kuwa kama ataachana na huyo meneja atapoteana kimuziki.
Martha Mwaipaja anasema tumuombee Rose Muhando badala ya kumhukumu. Waimbaji wa nyimbo za injili wamechukua nafasi ya shetani, shetani ndiye alikuwa kiongozi wa sifa kabla ya kutupwa kuzimu. Hivyo shetani anawawinda sana kwani wamechukua nafasi yake.
NB: Nimeshindwa kuipandisha Audio clip ya Martha Mwaipaja akiongea.
UPDATES
Clip za Martha Mwaipaja akisimulia sakata la Rose Muhando
Part one
Part two