Marking your territory...

MwanajamiiOne

Platinum Member
Jul 24, 2008
10,470
6,562
Dear Wapendwa
Natumaini wote mu wazima wa afya. Nisameheni kwa utitiri wa Threads wajameni mwezenu mie mwanafunzi nina kiu ya elimu hii ya kuboresha mapenzi!.

Najua kuwa wengi wetu tunapoanza mahusiano na tuwapendao tunakuwa na hamu ya kuufahamisha ulimwengu mzima kuwa Flani ni mpenzi wangu! Na kwa upande mwingine sometimes hata tunapokuwa tumekwishasimika mahusiano yetu kwa let say ndoa takatifu au tu uzao huwa bado tunapenda kutangazia umma kuwa am Mrs flani au Flan keshawahiwa na pengine hata kama una uhakika na ndoa yako basi bado tu tunajitengenezea njia ya kufumuza 'mwizi'.

Mfano kwa wanawake ambao ni single mara nyingi huwa tunaweka uwepo wetu kwenye 'maisha' ya mpenzi mfano, nyumbani kwake tukienda klumtembelea basi mdada utahakikisha umeacha japo nguo ya ndani kama si khanga ili mradi kuji'homkisha' ati. Wengine huenda mpaka an extra mile ya kuhamishia baadhi ya nguo kwa mpenzi ili tu ataekuja ajue kuwa 'the vacant is filled'. Kwa wale wenye ndoa basi mtu anaacha tu kwa gari, iwe viatu/sandoz au khanga au hata handbag au hand lotion!! Ili mradi chochote cha kuweza kutambulisha 'uwepo wake'

Ninaimani kuwa wanaume nao huwa wana'namna' wanavyoweza kumark their territories mfano, wapo wanaume ambao wanademand kupewa a 'proper' introduction pale mnapokutana na mtu; wale ambao akitembea anapenda kukushika kiuno ili mradi tu ule ujumbe wa 'Hiki ni kifaa changu' ufikishwe ipasavyo.

Nauliza
1. Je unafikiri ni muhimu kuweka 'alama'?
2. Kama ndio je ni vitu gani ambavyo mtu anawezavifanya ili ku'mark his/her territory"?? kuhakikisha kuwa watu wanapata ujumbe wa 'MJ1 ni wangu' au 'Hiki ni kifaa changu, kaeni mbali' ) ?? Note mimi si kifaa maana mh labda jifaa!!.
 
inategemea na confidence ya mtu. ukiwa confident mbona huhitaji ku-mark teritorry? Ila kama unaona teritorry yenyewe ipo hatarini basi hivyo umetaja hapo ni tosha kabisa. ka nguo huku, lotion kule, maybe chain na medalion ya initial zako pia etc... hold hands, kiss na introduce him popote iwezekanapo...
 
sasa wewe wahitaji help from professional......

you are going mad now.............

usisahau mapenzi yalikuwepo kabla hatujazaliwa......huitaji kujifunza saana.......

mengine utajajua tu slowly.......
 
in short huwa sipendi watu wajue coz i strike like a player 2every gal................huh
Mh okay kama wewe hutaki, je hao kina wifi hawajawahi kuku'tegeshea' vyao? kuna mwingine akija kukutembelea anaweka alama jikoni au kwenye kabati la nguo na akija mwingine anajua tu kuna rafu imechezwa!
 
inategemea na confidence ya mtu. ukiwa confident mbona huhitaji ku-mark teritorry? Ila kama unaona teritorry yenyewe ipo hatarini basi hivyo umetaja hapo ni tosha kabisa. ka nguo huku, lotion kule, maybe chain na medalion ya initial zako pia etc... hold hands, kiss na introduce him popote iwezekanapo...

Okay so kama nimekuelewa vema its a matter of kujiamini??!! kuwa ukiamini huyu anakupenda wewe tu basi huna aja ya ku'mark your territory'? ok!
 
sasa wewe wahitaji help from professional......

you are going mad now.............
Eh umewaza mbali sana Kaka yangu....... hakuna cha kunimadisha kwa umri huu mydia just read the thread as it is, there is nothing hidden that requires you to read between the lines because there are no lines in between!!

usisahau mapenzi yalikuwepo kabla hatujazaliwa......huitaji kujifunza saana.......

mengine utajajua tu slowly.......

So kwa kuwa yalikuwepo toka mwanzo basi tusijifunze, ndo unavyotushauri kaka yangu?
Thankx anyway.
 
Eh umewaza mbali sana Kaka yangu....... hakuna cha kunimadisha kwa umri huu mydia just read the thread as it is, there is nothing hidden that requires you to read between the lines because there are no lines in between!!



So kwa kuwa yalikuwepo toka mwanzo basi tusijifunze, ndo unavyotushauri kaka yangu?
Thankx anyway.

women don't mark their territories.
kwa sababu wao ndio territories yenyewe....

labda ufanye decorations ya territories.....but mwenye kazi ya ku mark
hiyo territory ni mwanaume...
labda wewe utafute mbinu ya kumfanya yeye aanze ku mark hiyo territory.......
 
MJI...,Alama muhimu bana,pichu, lotion, perfumes, shoes, framed photo, shower gels,mtandio n so n so....,to me they hv 2 impacts;
moja nikiacha kitu changu nahisi kama nimeacha kitu ambacho kitakuwa kinamremind him of me u knw.., n secondly pia nasend ujumbe kwa mwingine atakayekuja ajue tupo wengi , na yeye kama anajiamini aache vya kwake, me love this game bana
 
women don't mark their territories.
kwa sababu wao ndio territories yenyewe....

labda ufanye decorations ya territories.....but mwenye kazi ya ku mark
hiyo territory ni mwanaume...
labda wewe utafute mbinu ya kumfanya yeye aanze ku mark hiyo territory.......

I beg to differ The Boss.............. kila mtu ni territory ya mwenzie when it comes to love ukisema hivyo unavyosema wewe ni kama vile unasema mwenye kazi ya kupalilia penzi ni mtu mmoja!!

Nafikiri hata wanawake tuna 'mark our territories' hasa ukichukulia hiyo mifano michache......The Boss unatakakusema katika maisha yako yote ya mapenzi hujawahimpata mwanamke ambaye alifanya chochote cha kujihalalishia?? hata kuiweka picha yake kama screen saver kwenye simu yako??
 
MJI...,Alama muhimu bana,pichu, lotion, perfumes, shoes, framed photo, shower gels,mtandio n so n so....,to me they hv 2 impacts;
moja nikiacha kitu changu nahisi kama nimeacha kitu ambacho kitakuwa kinamremind him of me u knw.., n secondly pia nasend ujumbe kwa mwingine atakayekuja ajue tupo wengi , na yeye kama anajiamini aache vya kwake, me love this game bana

Aksante Nailyne kwa kuwa muwazi! Unajua mie nimekuwa nikivisikia na kutokuamini but after kumwona dadangu anavyo'jitahidi' ndo nimeshikwa na hamu ya kujua wengine wanafanyaje! Binafsi napenda ijulikane wazi kuwa flani ndo nlomtunuku, na ningependa sana kuacha 'ala,a' but huwa ninajishuku kuwa ataona ninam'chock' sasa naogopa kujaribu but frankly speaking natamani sana ningekuwa naweza kuwa Aggressive kwa mwenzangu!
 
dahhh
Kipindi hicho
Nkienda kwake nabeba kila kitu nkitoka kwake siachi kitu nyuma..(harufu ya perfume tu ndo itabaki kwake)
ila kuna hii tabia moja ya nguo zangu za ndani ataichukua sjui sababu... (tullivyotengana nlimwambia anirudishie kakataa)
anyhow hainisumbui sana.. isje mletea balaa baadaye (kwa mamsap mpya)

yap hiyo tabia ya kushikana mikono, ananishika kiuno sjui kumuweka mkono kwenye mfuko wa nyuma wa suruali ,
"random kisses", kukaa kwenye mapaja yake, kunibeba tukiwa beach, dahhh mapenzi yana raha yake jamaani..
ila yakichachuka machungu kuliko ndimu.
kwenye disco ndo hupati hata nafasi ya kuhema....

Kujibu swali lako si lazima kuwekeana alama ila mkiwa kwenye ile "moment"
inakuja natural..... (hii ni kwa physical contact) ni sisahau na zile za
ku "show off"

na tukija kwenye vitu , "Ni wako" kwa hiyo haijalishi ukiacha au la
kama ke/me anakupenda ile ya haswa ye mwenyewe ataviweka mfano
picha yako jikoni hahahaha lol...

Nway MJ1 na Mbu nakimbiaga poster zenu sababu zinanikumbusha
ambako staki kukumbuka....
sante....
 
I beg to differ The Boss.............. kila mtu ni territory ya mwenzie when it comes to love ukisema hivyo unavyosema wewe ni kama vile unasema mwenye kazi ya kupalilia penzi ni mtu mmoja!!

Nafikiri hata wanawake tuna 'mark our territories' hasa ukichukulia hiyo mifano michache......The Boss unatakakusema katika maisha yako yote ya mapenzi hujawahimpata mwanamke ambaye alifanya chochote cha kujihalalishia?? hata kuiweka picha yake kama screen saver kwenye simu yako??

nimekumbana na hiyo unayoita to mark your terrotory.....nyingi saana....
but honestly i was not impressed......

labda kwa kuwa nilikuwa najua ndo mchezo wao....

naikumbuka moja tu ambayo ilikuwa sikuiona kabisa.....

mapazia ya sebuleni yalibadilishwa...

funny thing kila alipokuja mwingine cha kwanza aliuliza hayo mapazia
ulinunua wapi?ni we mwenyewe ulinunua?

nikajua taste ya mwanamke namwanaume ilivyo tofauti...

ilinishangaza hiyo tu...

mwanamke anajuaje mwanamke mwenzie alama zake.....
 
AD aksante sana nimeupenda mfafanuo wako I hope now nitaeleweka ni nini nazungumzia (Ah sie walimu wa kata bana kujielezeeea sana hatuwezi!!) Thanx mamito.

Hahahha tusamehe bana kama tunakukwaza kuanzia leo za aina hii namwachia Mbu, mie ntakuwa naleta za kukufurahisha tu AD
 
nimekumbana na hiyo unayoita to mark your terrotory.....nyingi saana....
but honestly i was not impressed......

labda kwa kuwa nilikuwa najua ndo mchezo wao....

naikumbuka moja tu ambayo ilikuwa sikuiona kabisa.....

mapazia ya sebuleni yalibadilishwa...

funny thing kila alipokuja mwingine cha kwanza aliuliza hayo mapazia
ulinunua wapi?ni we mwenyewe ulinunua?

nikajua taste ya mwanamke namwanaume ilivyo tofauti...

ilinishangaza hiyo tu...

mwanamke anajuaje mwanamke mwenzie alama zake.....

Now we are talking The Boss, umeona?? hiyo ya mapazia ndo nimeisikia kwako kuna wengine jinsi anavyopanga mataulo bafuni au vyombo kabatini, anajua kabisa hapa umepita mkono wako na hapa si ugusaji wako huu!! Mwingine ana harufu flani ya nyumbani akija mwenye perfume nyingine siku hiyo lazima atajua tu!!
 
ukiwa mjanja unafuta alama zote za mwanamke wako
kabla hujaleta mwingine...nguo,lotion,viatu unakusanya kwenye boksi
unaweka store....nilishindwa kugundua hiyo ya mapazia tu,basi..
later on niliyabadili pia lol
enzi hizo offcourse..lol
 
nimekumbana na hiyo unayoita to mark your terrotory.....nyingi saana....
but honestly i was not impressed......

labda kwa kuwa nilikuwa najua ndo mchezo wao....

naikumbuka moja tu ambayo ilikuwa sikuiona kabisa.....

mapazia ya sebuleni yalibadilishwa...

funny thing kila alipokuja mwingine cha kwanza aliuliza hayo mapazia
ulinunua wapi?ni we mwenyewe ulinunua?

nikajua taste ya mwanamke namwanaume ilivyo tofauti...

ilinishangaza hiyo tu...

mwanamke anajuaje mwanamke mwenzie alama zake.....

mhh 'The Boss' mbona hii issue ya mapazia nishakutana nayo ... bt i hope its nt u??? he he he lol
 
AD aksante sana nimeupenda mfafanuo wako I hope now nitaeleweka ni nini nazungumzia (Ah sie walimu wa kata bana kujielezeeea sana hatuwezi!!) Thanx mamito.

Hahahha tusamehe bana kama tunakukwaza kuanzia leo za aina hii namwachia Mbu, mie ntakuwa naleta za kukufurahisha tu AD

dahhhhhh
mbaona topic inajieleza kirahisi hivyo kila eleweka bana unachozungumzia
ila hapa nyumbani kwetu ni tuna amuaga tu kutoelewa si kwamba hatuelewi...
hahahahaha MJ1 wewe walimu wa kata wanapenda kujieleza hivyo mweehh
uwakute ofisini break ya saa nne ni michapo kwa kwenda mbele...lohhh

Bana mie napenda sana Topic Zenu wewe na Mbu ila yanibidi nijizuie kuchangia
mweehh usiache kuleta mambo matamu kuwafaidisha wengine huwa nasoma
comment zote kwenye thread zenu bali sjangii tuu saa nyingine wajifunza
na kujifurahisha kwa kusoma tu..

huwa nawazaga "Kama MJ1 na Mbu wakiwa pamoja"( dating or marriage)
watakuwa "Perfectooo" couples.. (siri usmwambie mtu hahahah ) :)
 
ukiwa mjanja unafuta alama zote za mwanamke wako
kabla hujaleta mwingine
...nguo,lotion,viatu unakusanya kwenye boksi
unaweka store....nilishindwa kugundua hiyo ya mapazia tu,basi..
later on niliyabadili pia lol
enzi hizo offcourse..lol

dahhh
hujakumbwaga na haya??
tumekubaliane tukutane ntapulizia perfume kali kweli
labda ufue hiyo nguo mara 5 ndo harufu ya perfume itaanza pungua..

kingine nakukumbatia tu wakati nakuga (nakupa kiss dogo tu nyuma ya bega)
naacha alama ya lipstick ... mambo madogo tu kama hayo hutayafikiria sana
muda huo lakini yanaweza kukuleta bifu na mamitoo..
 
Hayo mambo yapo, lakini ninakubaliana na yule aliyesema ikiwa kuna mapenzi ya kweli, ya kuaminiana na kuheshimiana, hakuna haja ya "kumark your territory". Pia nahisi ni mambo yanayofanyika wakati katika mazingira ya "wizi", wakati wa kutafuta, wakati bado unapigania kuchukua ushindi dhidi ya washindani wenzako na kadhalika. Lakini ikiwa tayari unaye, ya nini kumark territory? Hujiamini au humwamini? Pengine yeye anakusaidia kumark hiyo territory ili kuwambia waviziaji kuwa tayari he/she occupied.
Lakini tusichanganye baina ya kumark territory na kuonesha mahaba kwa mwenzako kama hiyo ya kushikana, kubebana, kubusiana n.k.
Kuhusu mkasa ulowahi kunifika. Siku moja mdada jirani alokuwa ananivizia akielewa hayumo katika ajenda yangu alimwaga shanga kupitia dirishani. Hii ilinigharimu uhusiano nilokuwa nao na yule dada akawa anajisifia kwa tendo lile la "ama wangu au tukose wote".
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom