Marie stopes na utoaji mimba....

KP nadhani kuna point hujaelewa au mimi sijaelewa...PJ kaongelea utoaji wa mimba nayohatarisha maisha ya mama (hii inakubalika ikithibitishwa na mganga) na hapo aliposema mimba iliyotokea involuntarily nahisi ni typo error, nimeelewa kama alitaka kusema mimba iliyotoka involuntarily kwa hivyo PAC utapata pale Marie Stopes
Exactly BHT!
Ambacho hajanielewa KH ni kati ya phrases hizi 2 "mimba kutokea kwa hahati mbaya' na "Mimba kutoka kwa bahati mbaya"
I actually meant the second phrase!, thanx for clarification!
 
bht...hata mimi nimeshangaa sana! maana mimba zinatokea involuntarily ni nyingi sana! Na kama mimba imetoka, wao wanachofanya ni kumsafisha mama na sio kutoa mimba! Mhhhh hapo kwa kweli sijaelewa..................

Mimba gani hizo ambazo hutokea involuntarily? Manake sijawahi sikia mimi hizo....hebu elezea zinavyotokea tafadhali.
 
Exactly BHT!
Ambacho hajanielewa KH ni kati ya phrases hizi 2 "mimba kutokea kwa hahati mbaya' na "Mimba kutoka kwa bahati mbaya"
I actually meant the second phrase!, thanx for clarification!

NN yalikuwa ni makosa ya kiuandishi tu

Mimba gani hizo ambazo hutokea involuntarily? Manake sijawahi sikia mimi hizo....hebu elezea zinavyotokea tafadhali.
 
hii ni hatari na hawa jamaa nadhani wameingia kwa gia ya missionary..
Bwana Ndetichia, nakuheshimu mzee!
Usiongee kitu cha Hisia za kuwatuhumu watu wasiohusika!
How can you just speculate that they originate from Missionary sector?...unless una bifu na wamisionari, which is LOW!
Umesikia lini missionaries wakahusika na arbotions?....my hairs!
 
What i heard is that they do abortion officialy.. Its part of their services. And as far as the law is concerned they are probably permitted because otherwise wangesha kamatwa by now.
Hearsay...!
You heard from whom?
Did you take your time doing a bit of follow up, or you just live by gossip!
 
Mimba ya bahati mbaya? Yaani ulikuwa unaogelea bwawani, kwa bahati mbaya manii zikaingia, au ulikuwa kwenye ngono manii zikaingia...!?

HAKUNA MIMBA YA BAHATI MBAYA.
 
Maria Stopes, wame specialized kwenye utowaji wa mimba kwa kisingizio cha Family Planning.

Huyu mama Maria Stopes, yeye alikuwa hapendi kuona watu wa kipato cha chini wakizaliana na kuwaona kama ni mzigo tu kwa taifa na hawana faida lolote lile, ndio akaja na haya mawazo ya kuwaondoa viumbe vilivyoko matumboni... Kisingizio Family Planning.
 
Ninachojua ni kwamba Marie Stopes is an arm of the Freemasons.Hili nina hakika nalo.Sasa kama unawajua freemasons jibu unalo.Go to the "Secret covenant"utatamani kulia.
nilipokuwa form two,kuna mshikaji wangu mmoja alipata kesi ya kumpa mimba msichana
kwa sisi wengine tulikuwa na wasiwasi mno jamaa atafanyaje,baada ya wiki jamaa akaja kutusimulia
yaliyotokea...akatuambia yeye na gf wake walienda clinic ya marie stpoes,wakasema wanataka kutoa mimba..
mapolezi,wakalipia gharama na risiti wakapewa,akatuonesha...
sikubuki now kilichoandikwa kwenye risiti...na baadae huyo msichana akafanyiwa abortion....

sasa later on ukubwani niliwai soma kwenye magazine moja kuwa hizi taasisi au clinic za marie stopes
ni clinic maalum kwa wanaotaka kutoa mimba...ni za wanaharakati wanaotetea utoaji wa mimba

sasa hapo kidogo ndio najiuliza

je hapa tz hawa marie stopes wana operate kwa vibali vipi?

na je ni kweli wanatoa mimba bila kificho????

sheria zetu zikoje?na kwa nini kama hawa wapo tena kwa uwazi,wapo wadada wanahatarisha maisha yao kwa
kutoa mimba vichochoroni???????
 
Hearsay...!
You heard from whom?
Did you take your time doing a bit of follow up, or you just live by gossip!

wewe acha ubishi
watu wameenda na kusema tunataka kutoa mimba
wakaambiwa lipia kiasi fulani,hakuna swali la ziada
na wakahudumiwa
 
Huu ni mjadala mwingine ambao utasababisha watu watoane macho...
Jafaham ni mjadala mngine ila swali la Maria Stopes zinahusu na dispensary zingine hata chemist. Si unaona comment ya Gaijin? kwa kweli ni bora wahalalishe tu na serikali iwe inafanya audits na inspections. bila hivo watu wataendelea kutoa kwa uficho na dispensary zitaendelea kutosa faini kubwa kwa kitu illegal.
 
Hivi kwa nini serikali isihalalishe kutoa mimba? Rwanda ni free (on state health department expences) Burundi ni halali before the 6th week etc. Kwa nini TZ wasiamui tu iwe free, na waweke sheria maalum za kitendo hicho?
Samahani Boss, maybe nimesukuma boundary ya post yako mbali kidogo

Kutoa mimba ni halali hapa Tz.......isipokuwa uhalali huo uambatane na 'sababu halali' za kutoa mimba hiyo. Utoaji wa mimba ni mojawapo ya dilema ambazo ni vigumu sana kupata ufumbuzi/consesus katika jamii nyingi. Kuna masuala mengi tu, mojawapo: haki ya kuishi ya mtoto/mimba vs haki ya mama kuchagua.
 
Kutoa mimba ni halali hapa Tz.......isipokuwa uhalali huo uambatane na 'sababu halali' za kutoa mimba hiyo. Utoaji wa mimba ni mojawapo ya dilema ambazo ni vigumu sana kupata ufumbuzi/consesus katika jamii nyingi. Kuna masuala mengi tu, mojawapo: haki ya kuishi ya mtoto/mimba vs haki ya mama kuchagua.
Mama akishapata mimba hana haki tena kumchagulia kiumbe mwingine kuishi au kufa...! Hayo ya kuchaguwa yanapaswa kufanyika kabla ya ujauzito na si baada ya ujauzito.

Vilevile mwanamke ambaye amebakwa, haruhusiwi kutoa mimba yake. Watu wengi utakuta wanatoa sababu kadhaa kuhalalisha kutoa mimba kwani kufanya hivyo, ni kutenda dhambi wakati inajulikana kuwa hicho kilichopo tumboni hakihusiki kwa njia moja au nyingine na jarima ile ya kubakwa mwanamke huyo, na maadam haikuwa ridhaa ya mwanamke kufanywa hivyo na alijitahidi kupambana na mbakaji/wabakaji akazidiwa, ni wajibu wake kukihifadhi hicho kiumbe na Mwenyezi Mungu Atakilinda na kukijaalia kuwa ni chema na poza kwa mama yake.

Mimba inaweza kutolewa ikiwa mwanamke ataambiwa na daktari mzoefu na aliyebobea katika taaluma ya kizazi na awe daktari muhadilifu, kuwa kuendelea kubeba mimba hiyo itakuwa ni hatari kwa mama. La si hivyo basi itakuwa haifai kuitoa kabisa na mwenye kutoa atakuwa ametenda kosa kubwa la jinai, na hata mbele za Mungu.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom