Maridhiano bila Suala la Wabunge Fake 19 Kuisha ni Tatizo

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,762
71,145
Kuna watu watasema suala liko Mahakamani hivyo lisubiri, lakini sio kweli.

Kesi iliyoko mahakamani ni kati ya wanachama 19 waliokuwa Chadema na chama chao cha zamani Chadema na haihusiani na Bunge kwani Bungeni wameshapewa taarifa kuwa hao wameshafukuzwa sio wanachama tena.

Kila mtu anajua kuwa wale wako bungeni kwa nguvu ya serikali ya CCM na sio nguvu ya katiba kwani hawana chama. Hivyo kulazimisha kuwa ni wabunge wa chama fulani kilichowakataa ni kunajisi hayo muitayo maridhiano na ni UKOROFI TUU.

Kamati kuu ya Chadema inayokutana leo ilijadili na hili kwani kesi ile wale wanapigania uanachama wao hivyo hawana haki kuwepo bungeni kama wawakilishi wa Chadema. Vinginevyo hayo MARIDHIANO YAMEJAA HADAA NA DHARAU . Serikali/Bunge watimize wajibu wao kuwaondoa kabla mambo hayajaharibika na Rais kuonekana muongo
 
Kuna watu watasema suala liko Mahakamani hivyo lisubiri, lakini sio kweli.
Kesi iliyoko mahakamani ni kati ya wanachama 19 waliokuwa Chadema na chama chao cha zamani Chadema na haihusiani na Bunge kwani Bungeni wameshapewa taarifa kuwa hao wameshafukuzwa sio wanachama tena...
Wale hawawezi kutoka. Bunge lazima liwe na wapinzani hata kama ni wa mchongo ndio matakwa yalivyo.

Maridhiano ndio hayo sasa.
 
Wanakuwa na utetezi wakiulizwa kuhusu hilo suala, wanasema kesi ipo mahakamani, wakati kimsingi hao wanawake hawakutakiwa kwenda mahakamani kupinga maamuzi halali ya vikao vya chama chao.

Haiwezekani taratibu zile zile zilizowashughulikia waliotangulia, zikawa na tofauti sasa, kwasababu hawana immunity yoyote, tatizo lipo kwa wale wanaowalinda kule bungeni, na mwenyekiti wao.
 
Unajua maana ya maridhiano?

Basi kama hujui ni hivi: kwenye maridhiano kila upande unakubali kupoteza baadhi ya haki zake ili mkutane katikati.

Kila upande ukishikilia msimamo wake hakutakuwa na maridhiano.

Sijui umeelewa mleta mada??
 
Unajua maana ya maridhiano?

Basi kama hujui ni hivi: kwenye maridhiano kila upande unakubali kupoteza baadhi ya haki zake ili mkutane katikati.

Kila upande ukishikilia msimamo wake hakutakuwa na maridhiano.

Sijui umeelewa mleta mada??
CCM wamepoteza au watapoteza haki gani kwenye maridhiano haya
 
Maridhiano ni process, yes pamoja na hilo la hao wabunge feki nalo lina ukakasi mkubwa - kuna mengi mengi mno, kumbukeni uchaguzi wa 2020 uliacha makovu mengi mno, kwa hiyo tuwe na subira kama CCM wameamua jambo hili basi tuwe na subira.
 
Kuna watu watasema suala liko Mahakamani hivyo lisubiri, lakini sio kweli.
Kesi iliyoko mahakamani ni kati ya wanachama 19 waliokuwa Chadema na chama chao cha zamani Chadema na haihusiani na Bunge kwani Bungeni wameshapewa taarifa kuwa hao wameshafukuzwa sio wanachama tena...
Mnyika alisema kwenye vikao vya maridhiano pi walijadili Hilo suala changamoto inakuja Sasa kama Samia kakubali kuweka interest za CCM pembeni (walipinga tume huru, katiba mpya, mikutano) ni lazima Chadema nao wameambiwa wakubali kurudisha wabunge na kupokea ruzuku maana itakua Haina maana malalamiko yenu yamefanyiwa kazi alafu Bado mmesusa.

Naona ni kheri tukose Tume huru kuliko kurudisha wale wanawake ndio itakua kaburi la Chadema na itajenga precedence mbaya huko mbele utashangaa 2025 fomu ya mgombea Urais Chadema kachukua na kairudisha na NEC inampitisha Mdee kama mgombea Urais bila hata chama kupiga kura za maoni!! Au hata wagombea ubunge kurudisha fomu bila ya kura za maoni kufanyika.

Kama Dr Slaa na Zitto walienda na chama hakikufa Hawa wamama either wakiri kosa au hukumu itekelezwe ila sio kuwarudisha eti kisa maridhiano.
 
Wale wabunge wote 19 wanabaraka za Mwenyekiti Mbowe, hivyo achana nao kabisa.
Uongo unakusaidia Nini? Kama Wana Baraka za Mbowe unadhani alishindwa kuita press conference na kueleza kwanini kaamua tupeleke wabunge?

Kuna ambaye angempiga au kuhoji? Kama aliweza ita press conference na kuendorse ujio wa Lowassa alishindwa vipi kwa Hawa wamama? Kwani anamuogopa nani?

Kingine utaratibu ni lazima ufuatwe Sasa kisheria kamati kuu haijapitisha majina Sasa Toka lini mwenyekiti apeleke wabunge? Kwani NEC au Spika hajui taratibu?
 
Kuna watu watasema suala liko Mahakamani hivyo lisubiri, lakini sio kweli.

Kesi iliyoko mahakamani ni kati ya wanachama 19 waliokuwa Chadema na chama chao cha zamani Chadema na haihusiani na Bunge kwani Bungeni wameshapewa taarifa kuwa hao wameshafukuzwa sio wanachama tena.

Kila mtu anajua kuwa wale wako bungeni kwa nguvu ya serikali ya CCM na sio nguvu ya katiba kwani hawana chama. Hivyo kulazimisha kuwa ni wabunge wa chama fulani kilichowakataa ni kunajisi hayo muitayo maridhiano na ni UKOROFI TUU.

Kamati kuu ya Chadema inayokutana leo ilijadili na hili kwani kesi ile wale wanapigania uanachama wao hivyo hawana haki kuwepo bungeni kama wawakilishi wa Chadema. Vinginevyo hayo MARIDHIANO YAMEJAA HADAA NA DHARAU . Serikali/Bunge watimize wajibu wao kuwaondoa kabla mambo hayajaharibika na Rais kuonekana muongo
Hao hawatotoka,

Angalia mambo muhimu,

Watatoka pale CDM watapokubali kupeleka wabunge wengine,

Maana Hadi sasa CDM Haina mpango wa kupeleka wabunge bungeni,

Umeelewa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom