Marekebisho ya Sheria kuondoa mamlaka ya DPP kumkamata tena mshitakiwa anayemuondolea mashitaka kwa "Nolle Prosequi"

Linguistic

JF-Expert Member
Mar 16, 2021
3,671
8,237
Wakuu Moja ya marekebisho muhimu sana ya Sheria ya Mwenendo wa Mashitaka ya Jinai, Sura ya 20, (CPA) ya Sheria za Tanzania, yaliyomo katika Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2021 ni Kifungu cha 91 (1) ambacho kinampa Mkurugenzi wa Mashitaka ya Jinai (DPP) mamlaka ya kumuondolea mashitaka mshitakiwa mahakamani kwa lugha kisheria "nolle prosequi" na kuweza kumkamata tena na kumshitaki kwa mashitaka yale yale yaliyoondolewa na kuyaanzisha upya bila kujali alishakaa mahabusu jela muda mrefu.

Mamlaka hayo ya DPP yalikuwa yanaleta kadhia kubwa sana kwa washitakiwa.

Muswada huo ambao sasa upo mikononi mwa Kamati ya Sheria na Katiba ya Bunge ikipokea na kusikiliza maoni ya wadau, unamlinda mshitakiwa kutokamatwa tena na kushitakiwa kwa makosa yale yale ya awali.

Isipokuwa kuwe na sababu za kuridhisha kwa mahakama na kesi ianze kusikilizwa mara moja bila kucheleweshwa kwa mujibu wa Kifungu cha 131A (1) cha CPA ambacho nacho ni kipya kinachopendekezwa ndani ya Muswada huo, kinachotaka upelelezi uwe umekamilika ndipo mtuhumiwa ashitakiwe.

Hivyo kukomesha kauli zilizozoeleka za waendesha mashitaka (ma-PP) kwamba "upelelezi bado kukamilika" na kutaka kesi kuahirishwa kwa tarehe nyingine za kutajwa na mshitakiwa kurudishwa mahabusu jela.

MAREKEBISHO HAYA YATALETA MANUFAA YAFUATAYO KATIKA HAKI JINAI NCHINI:
1. Mkurugenzi wa Mashitaka ya Jinai (DPP) kuhakikisha anafungua mashitaka yenye ukamilifu wa upelelezi.

2. Mahakama itaweza kukataa mashitaka yanayorudishwa tena na waendesha mashitaka kutoka ofisi ya DPP baada ya awali kuyaondoa.

3. Mashitaka hayatachelewa kusikilizwa mahakamani kwa sababu ya upelelezi kutokamilika kwani hati ya mashitaka haitapokelewa na mahakama iwapo upelelezi haujakamilika.

4. Itapunguza msongamano wa mahabusu magerezani kwani wengi husubiri kukamilika kwa upelelezi wa kesi zao.

5. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kutoka Jeshi la Polisi itabidi awe makini katika ukamataji na upelelezi wa watuhumiwa ikiwemo suala la kubambikia watu kesi ambazo DPP atakosa ushahidi na kumfanya asifungue mashitaka au ayaondoe bila ya kuyarudisha tena.

I Humbly Submit Guys
 
Kwa nini hata hicho cheo cha DPP kisiondolewe? Umuhimu wake ni upi hasa? Mimi si mwanasheria, na wala sina uelewe wowote ule wa kutosha kuhusu hiyo sheria.

Ila nilitamani kungekuwa na Ofisi moja tu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Na hivyo mambo yote yahusuyo sheria za nchi, mashtaka, nk. yangefanyika huko.
 
Huwa natizama chanel ya Discovery Investigation (ID) na kuona wenzetu walivyo makini katika kufanya upelelezi. Yaani mtuhumiwa wa mauaji hawekwi rumande mpaka wawe na uhakika kwa asilimia kubwa kwamba ni yeye alihusika ikiwemo DNA, Finger print, kushikwa na silaha iliyotumika nk. Kudos kwa Tz kama mapungufu hayo yameonekana.
 
Hili dubwana linaloitwa DPP ni kama Elephant in the small room,dubwana hili lina nguvu mno na lina uwezo wa kufanya vyovyote linavyotaka bila kuulizwa au kuwajibika kokote,ndio maana KATIBA mpya ni muhimu mno maana itaweka sawa mambo mengi ikiwemo kwa DPP kufanyiwa usaili na kamati maalum,kwa wenye interest na uwezo pls fuatilia interviews za kumtafuta CJ wa jirani zetu hapo S.A. ,its very interesting interviews,nimeota kuwa hata sisi tutafanya utaratibu huu wa CJ kupatikana in a more transparent manner.
 
Huwa natizama chanel ya Discovery Investigation (ID) na kuona wenzetu walivyo makini katika kufanya upelelezi. Yaani mtuhumiwa wa mauaji hawekwi rumande mpaka wawe na uhakika kwa asilimia kubwa kwamba ni yeye alihusika ikiwemo DNA, Finger print, kushikwa na silaha iliyotumika nk. Kudos kwa Tz kama mapungufu hayo yameonekana.
Yes nami ninaangalia sana hii kitu ID, hope police wetu watajifunza kitu fulani hapa hasa detectives wetu, A perfect murder, evil etc etc
 
Mahakama za Tanzania hazizingatii sheria kwenye kesi zenye maslahi kwa serikali au watawala kama inavyotakiwa. Mtawala au serikali ikikupeleka mahakamani, it simply means katiba, sheria, nk vikae pembeni ili kumpendeza mtawala au mlipa mishahara.

Hata warekebishe vifungu, hakuna jipya. Labda waje na katiba ya Warioba.
 
Kwa nini hata hicho cheo cha DPP kisiondolewe? Umuhimu wake ni upi hasa? Mimi si mwanasheria, na wala sina uelewe wowote ule wa kutosha kuhusu hiyo sheria.

Ila nilitamani kungekuwa na Ofisi moja tu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Na hivyo mambo yote yahusuyo sheria za nchi, mashtaka, nk. yangefanyika huko.
Kitengo cha DPP ni kitengo very powerful kuliko hata kitengo cha DCI ambacho ndiyo kinapeleleza makosa yote ya Jinai hapa Nchini,hata Kama Upelelezi umekamilika au haujakamilika, maamuzi ya kufungua kesi Mahakamani ni wao na hakuna wa kuwahoji,hata Afisa Usalama wa Taifa hawezi hoji!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Wakuu Moja ya marekebisho muhimu sana ya Sheria ya Mwenendo wa Mashitaka ya Jinai, Sura ya 20, (CPA) ya Sheria za Tanzania, yaliyomo katika Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2021 ni Kifungu cha 91 (1) ambacho kinampa Mkurugenzi wa Mashitaka ya Jinai (DPP) mamlaka ya kumuondolea mashitaka mshitakiwa mahakamani kwa lugha kisheria "nolle prosequi" na kuweza kumkamata tena na kumshitaki kwa mashitaka yale yale yaliyoondolewa na kuyaanzisha upya bila kujali alishakaa mahabusu jela muda mrefu.

Mamlaka hayo ya DPP yalikuwa yanaleta kadhia kubwa sana kwa washitakiwa.

Muswada huo ambao sasa upo mikononi mwa Kamati ya Sheria na Katiba ya Bunge ikipokea na kusikiliza maoni ya wadau, unamlinda mshitakiwa kutokamatwa tena na kushitakiwa kwa makosa yale yale ya awali.

Isipokuwa kuwe na sababu za kuridhisha kwa mahakama na kesi ianze kusikilizwa mara moja bila kucheleweshwa kwa mujibu wa Kifungu cha 131A (1) cha CPA ambacho nacho ni kipya kinachopendekezwa ndani ya Muswada huo, kinachotaka upelelezi uwe umekamilika ndipo mtuhumiwa ashitakiwe.

Hivyo kukomesha kauli zilizozoeleka za waendesha mashitaka (ma-PP) kwamba "upelelezi bado kukamilika" na kutaka kesi kuahirishwa kwa tarehe nyingine za kutajwa na mshitakiwa kurudishwa mahabusu jela.

MAREKEBISHO HAYA YATALETA MANUFAA YAFUATAYO KATIKA HAKI JINAI NCHINI:
1. Mkurugenzi wa Mashitaka ya Jinai (DPP) kuhakikisha anafungua mashitaka yenye ukamilifu wa upelelezi.

2. Mahakama itaweza kukataa mashitaka yanayorudishwa tena na waendesha mashitaka kutoka ofisi ya DPP baada ya awali kuyaondoa.

3. Mashitaka hayatachelewa kusikilizwa mahakamani kwa sababu ya upelelezi kutokamilika kwani hati ya mashitaka haitapokelewa na mahakama iwapo upelelezi haujakamilika.

4. Itapunguza msongamano wa mahabusu magerezani kwani wengi husubiri kukamilika kwa upelelezi wa kesi zao.

5. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kutoka Jeshi la Polisi itabidi awe makini katika ukamataji na upelelezi wa watuhumiwa ikiwemo suala la kubambikia watu kesi ambazo DPP atakosa ushahidi na kumfanya asifungue mashitaka au ayaondoe bila ya kuyarudisha tena.

I Humbly Submit Guys
Hivi ilipitishwa hiyo sheria au La
 
Huwa natizama chanel ya Discovery Investigation (ID) na kuona wenzetu walivyo makini katika kufanya upelelezi. Yaani mtuhumiwa wa mauaji hawekwi rumande mpaka wawe na uhakika kwa asilimia kubwa kwamba ni yeye alihusika ikiwemo DNA, Finger print, kushikwa na silaha iliyotumika nk. Kudos kwa Tz kama mapungufu hayo yameonekana.
Daah hii moja ya channel yangu pendwa sana mkuu, huwa nafuatilia sana programs zake na kiukweli ukilinganisha na hapa kwetu sisi bado sanaa.
 
Kitengo cha DPP ni kitengo very powerful kuliko hata kitengo cha DCI ambacho ndiyo kinapeleleza makosa yote ya Jinai hapa Nchini,hata Kama Upelelezi umekamilika au haujakamilika, maamuzi ya kufungua kesi Mahakamani ni wao na hakuna wa kuwahoji,hata Afisa Usalama wa Taifa hawezi hoji!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Sawa ni powerful ili kunufaisha watanzania kwa ujumla wao au ili kunufaisha watawala??
 
Back
Top Bottom