John Mnyika
JF-Expert Member
- Jun 16, 2006
- 712
- 1,240
Ujumbe toka kwa Tundu Lissu: "Muswada wa Matumizi ya Uchaguzi hauna malengo ya kuzuia fedha chafu katika uchaguzi na wala haujadaiwa hivyo na walioutunga. Hakuna kifungu hata kimoja kwenye Muswada wenyewe kinachokataza matumizi ya fedha za wizi au za madawa ya kulevya au za wakwepa kodi katika Uchaguzi. Wala haukatazi fedha za wageni. Hakuna kifungu hata kimoja kinachokataza fedha zinazotoka katika serikali au taasisi za kibeberu au mashirika yake au wananchi wa nchi hizo.
Lengo lake kuu ni kuzuia wapinzani - wawe wa vyama vya siasa au katika civil society - kupata fedha kutoka nje (hata kama ni kutoka kwa raia wa Tanzania walioko Kenya au Uganda!) au kutumia fedha zao wenyewe kama ziko ndani au nje ya nchi yetu. Huu ni Muswada hatari sana na kama kuna anayefikiri wanamtandao wameacha kuwa wanamtandao anaota ndoto au anataka na sisi tuote ndoto!
Naatambatanisha paper niliyoiwasilisha juzi katika Kongamano la DDC Mlimani Park. Nitafurahi kama nitathibitishwa kwamba nimekosea katika uchambuzi na conclusions zangu." Mwisho wa kunukuu
Ps: Nataka nianze kutafsiri uchambuzi husika kwenda kwenye lugha ya kiswahili. Ukiwa tayari nitawaletea. Au kama kuna ambaye unaweza kujitolea kutafsiri kwa haraka zaidi tafadhali anijulishe kupitia mnyika@yahoo.com au 0754694553.
Zingatieni kwamba vikao vya kamati za bunge vinaanza wiki hii, miswada hii nadhani itajadiliwa na kamati husika wiki ijayo. Hivyo, maoni na msukumo wa umma kuhusu suala hili ni jambo la dharura, na ni muhimu usambae kwa wadau wengi iwezekanavyo kwa haraka sana. Kwa jinsi serikali ilivyotangaza inaonyesha dhamira ni kupitisha katika kikao cha bunge kinachoanza karibuni.
Sambamba na muswada huu, pia kuna muswada mwingine wa sheria inayogusa masuala ya 'usalama wa taifa'.
Nawatakia mjadala mwema
JJ
Lengo lake kuu ni kuzuia wapinzani - wawe wa vyama vya siasa au katika civil society - kupata fedha kutoka nje (hata kama ni kutoka kwa raia wa Tanzania walioko Kenya au Uganda!) au kutumia fedha zao wenyewe kama ziko ndani au nje ya nchi yetu. Huu ni Muswada hatari sana na kama kuna anayefikiri wanamtandao wameacha kuwa wanamtandao anaota ndoto au anataka na sisi tuote ndoto!
Naatambatanisha paper niliyoiwasilisha juzi katika Kongamano la DDC Mlimani Park. Nitafurahi kama nitathibitishwa kwamba nimekosea katika uchambuzi na conclusions zangu." Mwisho wa kunukuu
Ps: Nataka nianze kutafsiri uchambuzi husika kwenda kwenye lugha ya kiswahili. Ukiwa tayari nitawaletea. Au kama kuna ambaye unaweza kujitolea kutafsiri kwa haraka zaidi tafadhali anijulishe kupitia mnyika@yahoo.com au 0754694553.
Zingatieni kwamba vikao vya kamati za bunge vinaanza wiki hii, miswada hii nadhani itajadiliwa na kamati husika wiki ijayo. Hivyo, maoni na msukumo wa umma kuhusu suala hili ni jambo la dharura, na ni muhimu usambae kwa wadau wengi iwezekanavyo kwa haraka sana. Kwa jinsi serikali ilivyotangaza inaonyesha dhamira ni kupitisha katika kikao cha bunge kinachoanza karibuni.
Sambamba na muswada huu, pia kuna muswada mwingine wa sheria inayogusa masuala ya 'usalama wa taifa'.
Nawatakia mjadala mwema
JJ