Marekani yazitaka nchi za kiarabu kulegeza kamba dhidi ya Qatar

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson anasema kuwa nchi za Ghuba ni lazima zilegeze hatua yao dhidi ya Qatar ambayo inalaumiwa na majirani zake kwa kuunga mkono ugaidi.

Saudi Arabia, Muungano wa nchi za kiarabu, Misri na Bahrain walikata uhusiano wa usafiri na wa Kidiplomasia na Qatar siku ya Jumatatu

Bwana Tillerson anasema kuwa hatua hiyo inasababisha kuwepo madhara ya kibinadamu.

Licha ya kumsifu Emir wa Qatar kwa kupuuza uungwaji mkono makundi ya kigaidi, Bwana Tillerson anasema mengi yanahitaji kufanywa.

Naye Rais Trump alikuwa ameandika kwenye kwenye mtandao wake wa Twitter akiunga mkono hatua ya kuitenga Qatar, na hata kudai kuwa alishiriki katika uamuzi uliochukuliwa na Saudi Arabia pamoja na nchi nyingine.

Ndege za Qatar zilipigwa marufuku ya kutumia anga za baadhi ya majirani zake.

Hatua hiyo ya ghafla ilichukuliwa baada ya msukosuko ambao umedumu miaka kadha kati ya Qatar na majirani zake wa Ghuba.


My take: Marekani acheni unafiki na undumilakuwili. Mnaleta ghadhabu na mkanganyiko sana kauli zenu.

Chanzo: BBC
 
Nchi yoyote inayo-support ugaidi ni ya kutengwa kwa nguvu zote! Kama kweli Qatar ndio mchezo wake kama wanavyodai majirani zake la muhimu asamehewe na asirudie tena upuuzi wake huo. Ila kama ilikuwa ni husda tu za majirani kutokana na mafanikio yake wenye haki wasimame naye. Ugaidi umeangamiza maelfu wasio na hatia kwa kisingizio cha dini!
 
Mwezi mtukufu
Waislam wanagombana wao kwa wao
USA anaingilia kati kutatua.

Waarabu ni watu wa ajabu sana.
Actually umuhimu wa "kafir" duniani unaonekana. Kafir ndiye huyo huyo mwenye sayansi na teknolojia; ndiye huyo huyo anayewalisha watu wa imani; ndiye huyo huyo anayewapeleka kutimiza ibada zao; ndiye huyo huyo wakigombana wanakimbilia kwake kutafuta hifadhi; ndiyo huyo huyo wakivurugana wenyewe kwa wenyewe wanamkimbilia kuomba awasuluhishe. Ila wakisimama kwenye mimbari zao matusi yanawatoka mfululizo sehemu zote za miili yao. Hao ndio watu wa imani na yule ndio kafir - maajabu hayaishi duniani humu.
 
Actually umuhimu wa "kafir" duniani unaonekana. Kafir ndiye huyo huyo mwenye sayansi na teknolojia; ndiye huyo huyo anayewalisha watu wa imani; ndiye huyo huyo anayewapeleka kutimiza ibada zao; ndiye huyo huyo wakigombana wanakimbilia kwake kutafuta hifadhi; ndiyo huyo huyo wakivurugana wenyewe kwa wenyewe wanamkimbilia kuomba awasuluhishe. Ila wakisimama kwenye mimbari zao matusi yanawatoka mfululizo sehemu zote za miili yao. Hao ndio watu wa imani na yule ndio kafir - maajabu hayaishi duniani humu.
Dini yao inasema hivi " mkitofautiana kwenye jambo basi rudini kwenye kitabu cha MwenyeziMungu"

Hawa waarabu wanashirikiana na makafiri kuwaumiaza wenzao waislam.
 
mmarekani tena!? huyu kiumbe namchukia sana huwa hapendi nchi zingine ziwe na uchumi imara haswa za kiarabu hapo anatafutwa huyo Qatar kwasababu ameonekana anakuja Kwa speed anatakiwa apunguze kidogo mmarekani hanaga urafiki kabisa na hizi nchi za kiarabu nilishangaa sana alipokuwa na uswahiba na Qatar nahisi yupo behind hii issue...
 
Marekani wamepanic kwasababu wana kituo kikubwa cha kijeshi hapo Qatar. Urusi iliishauri uturuki ipelekee majeshi haraka sana kwani Marekani na Saudi Arabia walikuwa na mpango wa regime change kwa nchi hiyo ndogo.
Qatar sio nchi inayofadhili ugaidi ni nchi inayopendelea demokrasi na uhuru wa vyombo vya habari. Kituo cha Aljezeera kinamilikiwa na serikali ya Qatar lakini serikali haiingilii utendaji wa shirika hilo ambalo ni mwiba kwa nchi za kibeberu kama Saudi Arabia.
Serikali ya Qatar iliunga mkono chama cha Muslim brotherhood kilichoshinda uchaguzi wa Egypt na serikali ya Saudi Arabia ndio ilifadhili mapinduzi ya kijeshi ambapo zaidi ya watu 10000 waliuawa.
Saudi Arabia ndio kitovu cha ugaidi.
Tatizo lingine Rais Donald Trump sera za nje ya serikali yake inayumba sana
 
Ukiwa huna akili, utashikiwa akili alafu wana ku drive watakavyo, sasa miarabu kutwa kupigwa kichwa chini, na kichwa ndio akili hukaa, sasa unategemea nini? U.S anawa drive atakavyo hata akitaka anawatia kidole kwa nyuma bado watakaa kimya tu. U.S is the only super super power..
 
Fitna inayopigwa na marekani hapa ni ya kiwango cha juu. Huku Israel huku USA Qatar ataponea wapi?
Ni ajabu sana Saudi Arabia anatoa sharti kwa Qatar kuacha kuwasaidia wapalestina Gaza na kuvunja uhusiano na Hamas wanaotawala Gaza. Kweli waarabu wamewezekana.
 
Back
Top Bottom