Marekani yawawekea vikwazo maafisa wa usalama wa taifa South Sudani kwa kuteka, kupoteza na kuua

Taso

JF-Expert Member
Jun 12, 2010
2,461
2,288
1577973646910.jpeg

Dong Samuel Luak na Aggrey Idri walitoweka January 2017

Marekani imewawekea vikwazo maafisa watano wa ngazi za juu za Usalama wa Taifa wa South Sudan, NSS, kwa kuhusishwa na utekaji na mauaji ya wakosoaji wawili wa serikali ya Rais Salva Kiir miaka mitatu iliyopita.

South Sudan imekuwa ikikana kujua kilichowasibu Mwanasheria mtetezi wa haki za binadamu, Dong Samuel Luak na mwanachama wa chama cha upinzani cha SPLM-IO, Aggrey Idri, walionyopolewa kwenye mitaa ya Nairobi, Kenya na watu wasiojulikana na kupotea January 2017.

Hata hivyo jopo la wataalam wa Umoja wa Mataifa liliripoti kuwa limedhihirisha ushahidi unaobainisha Serikali ya South Sudan ndio iliwateka, kuwasafirisha mpaka Makao Makuu ya Usalama wa Taifa wa South Sudan, mjini Juba, na hatimaye kwenye kambi ya mafunzo ya usalama wa taifa, Luri, iliyoko kwenye shamba linalomilikiwa na Rais Kiir, ambako waliuliwa.

Watano hao ni pamoja na Bw. Abud Stephen Thiongkol, ambae alikuwa Mkuu wa mahabusu ya Luri, na ndie anaeminika kuidhinisha wauawe . Wengine ni Malual Dhal Muorwel, Kamanda Mkuu wa Kambi ya Usalama ya Luri, John Too Lam, Mwambata wa Kijeshi wa Ubalozi wa South Sudan, Kenya, ambae pamoja na mtajwa mwingine, Michael Kuajien, walikuwepo Nairobi wakati wa utekaji. Pia yupo Angelo Kuot Garang, mwanausalama wa South Sudan aliyetumia passport ya Australia kurudi Afrika Mashariki kusimamia zoezi la utekaji wa wawili hao.

Ripoti ya jopo la wataalam hao wa Umoja wa Mataifa ilisema ilipata ushahidi wa vyanzo mbali mbali vilivyoshabihiana na vya kuaminika, wakiwepo watu waliowaona Bw. Luak na Bw. Idri katika mahabusu za Usalama wa Taifa mjini Jeba katika nyakati tofauti, kabla ya kuhamishiwa kwenye kambi ya Luri ambako inaaminika waliuliwa kwa kupigwa risasi Januari 30, 2017.

Vikwazo vya kiuchumi vya Marekani kwa watu binafsi vinatwaa mali yeyote ya mhusika iliyoko kwenye himaya ya Marekani, na inapiga marufuku Waamerika kufanya nae miamala. Sheria ya vikwazo pia inazuia taasisi zozote duniani zinazofanya biashara na Marekani kujihusisha na mhusika aliyeko kwenye vikwazo.

Wanaharaki wa haki za binadamu wa jumuiya ya Kimataifa wamesema wamepokea hatua hiyo ya Marekani kama mwanzo wa mchakato wa kuwafikisha wahusika mbele ya vyombo vya sheria.
 
Taso,
sidhani hatua kama hii na athali kwa haya mauaji/makatili ya watu. Ni kuwapiga mabomu tu!
 
sidhani hatua kama hii na athali kwa haya mauaji/makatili ya watu. Ni kuwapiga mabomu tu!

Kwa kiasi fulani ina athari.

Kwa mfano, mashirika ya ndege duniani hayawezi kukuuzia tiketi. Labda Iran Airways na North Korea ambao hawana business na USA.

na haya maharamia yenye madaraka ya kuua watu huwa ni matajiri yanayopenda kwenda kula bata Ulaya na Marekani, kwa namna moja vikwazo vinawakinza.

Yakikaribia kufa huwa yanaenda kutibiwa wapi haya ma kleptocrat yaliyoua na kuiba hela, yanaenda Ulaya na USA.

Wakuu wa Usalama na Wanajeshi wengine wakisha staafu kazi chafu zao wanasubiri ubalozi Ulaya. Vikwazo vinawazuia.

Wengine wana ma hisa na ma business interest kwenye ma multi nationals ya migodi, oil imports, twiga exports, yote haya sasa mabenki ya dunia yanawamulika....

Wengine wanataka kupeleka watoto shule Marekani, vikwazo vinawazuia...

there is more than one way these sanctions hurt them
 
Hivi kwa mfano ukimuwekea Magu vikwazo vya kusafiri nje ya nchi wkt yeye mwenyewe tu hua ana allergy na kusafiri,ukawawekea na watoto wake vikwazo vya kusafiri ili wasisome huko nje(wkt wao wanasomea hapa Udom) hapo unakua umemkomesha? Taso,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kwa mfano ukimuwekea Magu vikwazo vya kusafiri nje ya nchi wkt yeye mwenyewe tu hua ana allergy na kusafiri,ukawawekea na watoto wake vikwazo vya kusafiri ili wasisome huko nje(wkt wao wanasomea hapa Udom) hapo unakua umemkomesha?

Sent using Jamii Forums mobile app


Tukiongelea vikwazo kwa mtu ambae hajatajwa kwenye taarifa hii thread yetu itafutwa, kwa saab freedom yetu ya imagination is "not to that extent."

Lakini speaking in general terms, wewe na mimi hatujui kiongozi fulani na fulani wanamiliki nini ambacho wamekinunua directly kutoka nje, hata kama hawasafiri.

Kwa mfano, nadhani Rais wa Afrika akitaka gari binafsi atalinunua cash, jipya, moja kwa moja kutoka ng'ambo. Under vikwazo huwezi!

Kwa sababu, kwa tajiri anaetapika hela, hapa Tanzania ataenda ku spend hela wapi, Mlimani City?
 
Kama ni gari linaletwa na dealers hapa bongo (CFAO,TOYOTA etc) linanuliwa hapa hapa.

Okay, you are right, anaweza kuwaambia niagizieni Range Rover na wakaleta nyumbani kwake special order.

Lakini bado nadhani mtu mwenye hela kumwambia hawezi kukanyaga Ulaya kuchagua na kujipima suti, itamuwia ugumu.

By the way, huyo uliyemtaja kasema akistaafu atasafiri sana na kula bata.
 
Hawa hawa waliosema,walidanganya,waliua na kuiba wanawawekea watu vikwazo kwa sababu ya kuua!Ridiculous.Hebu someni maneno ya Mike Pompeo.Wakiua wao sawa,wakiua wengine makosa.Hizi ni double standards za ajabu sana.These lunatics do not deserve our attention at all.

US Secretary of State Mike Pompeo: "I was the CIA director. We lied, we cheated, we stole. We had entire training courses. It reminds you of the glory of the American experiment." Kwanza inabidi ujiulize what American experiment,kama sio experiment ya kuua watu.
 
Viongozi wa DC Wanafiq Mnooo
Hawa hawa waliosema,walidanganya,waliua na kuiba wanawawekea watu vikwazo kwa sababu ya kuua!Ridiculous.Hebu someni maneno ya Mike Pompeo.Wakiua wao sawa,wakiua wengine makosa.Hizi ni double standards za ajabu sana.These lunatics do not deserve our attention at all.

US Secretary of State Mike Pompeo: "I was the CIA director. We lied, we cheated, we stole. We had entire training courses. It reminds you of the glory of the American experiment." Kwanza inabidi ujiulize what American experiment,kama sio experiment ya kuua watu.
Ila Mauaji Yanayofanywa Naserikali Ya US Isiwe Sababu Ya Uhalali wa Viongozi Wengine Kufanya Mauaji

Uhai wa watu lazima Uheshimiwe Haijalishi Nitaifa Gani Ama Kiongozi Yupi Anafanya Mauaji

Kila Mtu Anahaki Yakuishi Ila Pia Ana Haki Yakufa Ikitokea Kuna Sababu Maalum

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Viongozi wa DC Wanafiq MnoooIla Mauaji Yanayofanywa Naserikali Ya US Isiwe Sababu Ya Uhalali wa Viongozi Wengine Kufanya Mauaji

Uhai wa watu lazima Uheshimiwe Haijalishi Nitaifa Gani Ama Kiongozi Yupi Anafanya Mauaji

Kila Mtu Anahaki Yakuishi Ila Pia Ana Haki Yakufa Ikitokea Kuna Sababu Maalum

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli haipaswi kuwa sababu.Ninachosema ni kwamba hawana "moral authority" ya kunyoshea wengine vidole,waache wengine ambao hawana mauaji nchini mwao wanyooshe vidole kama wapo.
 
Hawa hawa waliosema,walidanganya,waliua na kuiba wanawawekea watu vikwazo kwa sababu ya kuua!Ridiculous.Hebu someni maneno ya Mike Pompeo.Wakiua wao sawa,wakiua wengine makosa.Hizi ni double standards za ajabu sana.These lunatics do not deserve our attention at all.

US Secretary of State Mike Pompeo: "I was the CIA director. We lied, we cheated, we stole. We had entire training courses. It reminds you of the glory of the American experiment." Kwanza inabidi ujiulize what American experiment,kama sio experiment ya kuua watu.
Duuh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom