Marekani yatuma salamu za muungano kwa Tanzania

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
On behalf of President Obama and the American people, I congratulate the people of the United Republic of Tanzania as you celebrate the forty-sixth anniversary of the union of Tanganyika and Zanzibar on April 26. This is an opportunity to celebrate the culture and accomplishments of your peaceful, tolerant and democratic country, and to reaffirm the bonds of friendship between our peoples.

We commend Tanzania for its work to promote regional stability, broad-based and inclusive prosperity, and democratic governance. And we salute your participation in peacekeeping operations from Sudan to Lebanon.

Your commitment to transparent governance and inclusive growth provides a foundation for the Millennium Challenge Compact we signed in 2008. Under this partnership, we are working together to support the Government of Tanzania’s efforts to reduce poverty through expanding remote populations’ access to transportation, electricity, and water. And through the President’s Emergency Plan for AIDS Relief and the President’s Malaria Initiative, we are working together to improve the health of Tanzania’s citizens.

Americans and Tanzanians learn from one another every day through our Peace Corps program, with volunteers serving in every corner of the country from Mtwara to Mwanza, as well as through an array of educational and cultural exchanges. I have been privileged to experience the warmth and generosity of the Tanzanian people myself during my own travel to your beautiful country.


May the coming year bring continued peace and prosperity to Tanzania. I offer you best wishes for a safe and happy holiday.


Hillary Rodham Clinton
Secretary of State

Washington, DC

April 25, 2010


PRN: 2010/507
http://www.state.gov/secretary/rm/2010/04/140777.htm

Muungano.JPG-1.JPG


Tafakari yangu:

Zipo changamoto nyingi za muungano ambazo mara zote zinapozungumzwa tu zinatafsiriwa kama "kero za Muungano". Muungano wetu daima umeonekana kama ni "ndoa" iliyounganisha nchi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar iliyozaa mtoto aitwae "Tanzania" na wakati huo huo akiwepo mtoto mwingine aitwaye "Zanzibar".

Kwa kutambua dosari za kiutawala ndani ya muungano, waasisi wa Muungano pia walionelea pia kuunganisha vyama vya siasa kwa wakati huo yaani TANU na ASP ambavyo vilizaa mtoto " Chama cha Mapinduzi (CCM). Ni mwaka hu huo 1977, Katiba ya Jamhuri ya Muungano ilipitishwa ikiwa imebeba pamoja na mambo mengine yale yaliyofikiwa katika Makubaliano ya Muungano ya Mwaka 1964 "Articles of Union".

CCM alishika hatamu ya uongozi wa Serikali mpaka aliporuhusu kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992 na kwa nia ya kulinda Muungano, miongoni mwa masharti kwa vyama vyote vya siasa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siass ni kuhakikisha Muungano unadumu kwa kuwa na itikadi isiyopingana na Muungano na kukubalika zinazokubalika na wananchi wa pande zote mbili za muungano (Tanzania Bara na Visiwani).

Hata hivyo, ndani ya Katiba yetu na pia mfumo mzima wa uongozi na utawala, bado zipo dosari nyingi sana ambazo zinafanya muungano wetu kuonekana una mapungufu na hatua za lazima za kushughulikia dosari hzo si kupuuza au kuhairisha yale ambayo wanasemwa na wananchi kuwa ni mapungufu...au pengine, si kujaribu kutegeneza mazingira ya kuwatishia na kuwakemea vikali wale ambao wanajaribu kubainisha mapungufu hayo na kuwaona kama wao ni "wahaini, wapotoshaji au wasioutakia mema muungano au kutozienzi fikra sahihi za viongozi wetu na waasisi wa Muungano".

Mungu ibariki Tanzania,

Mungu ibariki Zanzibar,

MUngu Ubariki Muungano.
 
haya bana............ngoja tuendelee kusaidiana!!!!!!!!!!!
 
Muungano.JPG-1.JPG


Tafakari yangu:

Zipo changamoto nyingi za muungano ambazo mara zote zinapozungumzwa tu zinatafsiriwa kama "kero za Muungano". Muungano wetu daima umeonekana kama ni "ndoa" iliyounganisha nchi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar iliyozaa mtoto aitwae "Tanzania" na wakati huo huo akiwepo mtoto mwingine aitwaye "Zanzibar".

Kwa kutambua dosari za kiutawala ndani ya muungano, waasisi wa Muungano pia walionelea pia kuunganisha vyama vya siasa kwa wakati huo yaani TANU na ASP ambavyo vilizaa mtoto " Chama cha Mapinduzi (CCM). Ni mwaka hu huo 1977, Katiba ya Jamhuri ya Muungano ilipitishwa ikiwa imebeba pamoja na mambo mengine yale yaliyofikiwa katika Makubaliano ya Muungano ya Mwaka 1964 "Articles of Union".

CCM alishika hatamu ya uongozi wa Serikali mpaka aliporuhusu kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992 na kwa nia ya kulinda Muungano, miongoni mwa masharti kwa vyama vyote vya siasa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siass ni kuhakikisha Muungano unadumu kwa kuwa na itikadi isiyopingana na Muungano na kukubalika zinazokubalika na wananchi wa pande zote mbili za muungano (Tanzania Bara na Visiwani).

Hata hivyo, ndani ya Katiba yetu na pia mfumo mzima wa uongozi na utawala, bado zipo dosari nyingi sana ambazo zinafanya muungano wetu kuonekana una mapungufu na hatua za lazima za kushughulikia dosari hzo si kupuuza au kuhairisha yale ambayo wanasemwa na wananchi kuwa ni mapungufu...au pengine, si kujaribu kutegeneza mazingira ya kuwatishia na kuwakemea vikali wale ambao wanajaribu kubainisha mapungufu hayo na kuwaona kama wao ni "wahaini, wapotoshaji au wasioutakia mema muungano au kutozienzi fikra sahihi za viongozi wetu na waasisi wa Muungano".

Mungu ibariki Tanzania,

Mungu ibariki Zanzibar,

MUngu Ubariki Muungano.

Mkuu kwa mtazamo wangu binafsi huu muungano ulibidi uwe hivyo au uundwe ulivyo kipindi kile na namna ya kuuboresha siyo kuunda serikali tatu wala kuendelea kuuzunguka ukweli. Kinachotakiwa kwa kizazi kijacho ni kuamua kuunganisha nchi iwe na Raisi mmoja, serikali moja, bendera moja, mawaziri wa serikali moja, sheria moja nchi nzima na bunge moja tuuu! Kila Mkoa uwe na haki ya kuchagua viongozi wake na wawakilishi ndani ya serikali kuu-bungeni, Zanzibar, Pemba zikiwakilishwa kama mikoa. Tuunde Shirikisho in other words. Hapo ndipo tutakuwa tumewaenzi waasisi wa Muungano na ndipo tutakuwa imara kama URT.

Bila busara zetu kutufikisha hapo huu muungano ni wa kujadili 24/7 na hakuna kitakachoeleweka.
I SEE THAT AS A SOLUTION!!
 
Ngoshwe usiwe naive kiasi hicho. Hizi ambazo zinaitwa kero zilianza kidogo kidogo, zimekuzwa kijanja janja mpaka watu wamefikia kuhoji uhalali wa Muungano wenyewe! Lengo hasa ni kuingia IKULU si vinginevyo! Kusaini mkataba wa Muungano wazanzibari walikubali, mabadiliko yote ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano tangu mwaka 1977 hadi leo yaliridhiwa na wazanzibari na Watanzania Bara, sasa iweje Wazanzibari wanalalamika kama vile hawakuwepo miaka yote hiyo? Usichukuliwe na upepo wa wanasiasa ndugu yangu, tafakari kwa kina kama msomi, utaelewa!
 
Back
Top Bottom