Marekani yatuma mfumo wa kukinga makombora na meli ya kijeshi mashariki ya kati huku wasiwasi kati yake na Iran ukiendelea

MakinikiA

JF-Expert Member
Jun 7, 2017
5,011
6,542
Marekani yatuma mfumo wa kukinga makombora na meli ya kijeshi mashariki ya kati huku wasiwasi kati yake na Iran ukiendelea
1093940


Meli hiyo ya kivita ya USS Arlington, inayosafirisha magari na ndege , itajiunga na kundi la kijeshi la USS Abraham Lincoln katika ghuba , maafisa wanasema.

Makombora ya US B-52 bombers pia yamewasili katika kambi moja nchini Qatar , idara hiyo imesema.
Imesema kuwa hatua hiyo inafuatia vitisho vya operesheni za vikosi vya kijeshi vya Marekani katika eneo hilo.
Marekani imetoa habari chache kuhusu uwezo wa tishio hilo , ambao Iran umepinga kama ujinga, ikitaja hatua hiyo ya Marekani kama vita vya kiakili vyenye lengo la kuitishia nchi hiyo.
Wakati huohuo chombo cha habari cha Isna News Agency kilimnukuu kiongozi mmoja mkuu wa dini , Yousef Tabatabai-Nejad akisema kuwa ''msafara huo wa Marekani unaweza kuharibiwa na kombora moja pekee''.
Siku ya Ijumaa idara ya Pentagon ilisema kuwa Marekani haitaki vita na Iran lakini Washington iko tayari kulinda vikosi vya Marekani na mali yake katika eneo hilo.

''Idara ya ulinzi inaendelea kufuatilia kwa karibu vitendo vya utawala wa Iran'', ilisema katika taarifa.

Iliongezea kuwa mfumo huo wa makombora ambao unaweza kutungua makombora ya masafa marefu na yale ya chini chini na ndege za kijeshi pia utapelekwa katika eneo hilo iwapo kuna uwezekano wa shambulio lolote.
1093919
 
Back
Top Bottom