Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Marekani imeufahamisha rasmi Umoja wa Mataifa kuhusiana na matakwa yake ya vikwazo kwa Iran virudishwe. Hayo yamepelekea upinzani kutoka kwa Urusi na wanachama wengine wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Marafiki wa Marekani kutoka Ulaya pia wameonyesha upinzani, wakiitaja hatua hiyo kuwa kinyume cha sheria.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo amemfahamisha rais wa Baraza hilo la Usalama akisema Iran imekiuka pakubwa mkataba wa mwaka 2015 wa nyuklia jambo linalotoa nafasi ya kuwekwa vikwazo hivyo kwa mara nyengine tena.
"Marekani haitokubali kamwe mfadhili mkubwa wa ugaidi duniani kununua na kuuza ndege, magari ya kivita, makombora na silaha zengine bila udhibiti. Vikwazo hivi vya Umoja wa Mataifa vitaendeleza marufuku ya kununua silaha," alisema Pompeo.
Marufuku hayo ya Iran kununua silaha yalikuwa yanakamilika Oktoba 18. Yanaizuia Iran pia kufanya majaribio ya makombora na urutubishaji wa urani.
Marafiki wa Marekani kutoka Ulaya pia wameonyesha upinzani, wakiitaja hatua hiyo kuwa kinyume cha sheria.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo amemfahamisha rais wa Baraza hilo la Usalama akisema Iran imekiuka pakubwa mkataba wa mwaka 2015 wa nyuklia jambo linalotoa nafasi ya kuwekwa vikwazo hivyo kwa mara nyengine tena.
"Marekani haitokubali kamwe mfadhili mkubwa wa ugaidi duniani kununua na kuuza ndege, magari ya kivita, makombora na silaha zengine bila udhibiti. Vikwazo hivi vya Umoja wa Mataifa vitaendeleza marufuku ya kununua silaha," alisema Pompeo.
Marufuku hayo ya Iran kununua silaha yalikuwa yanakamilika Oktoba 18. Yanaizuia Iran pia kufanya majaribio ya makombora na urutubishaji wa urani.