Marekani yataka Iran kuwekewa vikwazo vipya vya ununuzi wa silaha

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Marekani imeufahamisha rasmi Umoja wa Mataifa kuhusiana na matakwa yake ya vikwazo kwa Iran virudishwe. Hayo yamepelekea upinzani kutoka kwa Urusi na wanachama wengine wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Marafiki wa Marekani kutoka Ulaya pia wameonyesha upinzani, wakiitaja hatua hiyo kuwa kinyume cha sheria.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo amemfahamisha rais wa Baraza hilo la Usalama akisema Iran imekiuka pakubwa mkataba wa mwaka 2015 wa nyuklia jambo linalotoa nafasi ya kuwekwa vikwazo hivyo kwa mara nyengine tena.

"Marekani haitokubali kamwe mfadhili mkubwa wa ugaidi duniani kununua na kuuza ndege, magari ya kivita, makombora na silaha zengine bila udhibiti. Vikwazo hivi vya Umoja wa Mataifa vitaendeleza marufuku ya kununua silaha," alisema Pompeo.

Marufuku hayo ya Iran kununua silaha yalikuwa yanakamilika Oktoba 18. Yanaizuia Iran pia kufanya majaribio ya makombora na urutubishaji wa urani.
 
Hakuna wakati wowote ambao Marekani imekuwa dhaifu mbele ya maadui zake kama hii ya chini ya uongozi wa Trump.
US is F.u.c.k€d big big time.
Screenshot_2020-06-07-08-13-53.jpg
 
Duh ukiwa na nguvu nyingi wanaogopa kuja kijeshi.. hatimae Iran si Kama Libya ama Iraq ana nguvu za kuwasambaratisha Saudia, uae wakiwa kwao.. bahati Nzuri Iran husema kila Mara yeyote middle East atakaetumika na Marekani dhidi yake amekwisha..
Nadhani hata wao Saudia uae, na wengine hukataa kabisA kufanywa vifusi kwa kumkatataza marekani asimjaribu Iran coz ukimjaribu anajibu Mara 10 zaidi.
 
Tofauti na nchi zingine zote za middle East isipokua Israel, wairani Wana chuki na visasi Sana, toka wamepata Uhuru mwaka 1979 hawajawahi kuacha tukio la ovyo lipite bila majibu!
 
Kwaiyo unahisi USA wangepata Rais tofauti na trump wangekuwa na uwezo wa kabadilisha misimamo ya taifa kama kichwa ngumu kama Iran au sikio la kufa korea kaskazini ?
Hapana MKUU sikua namaana hio nlikua namaana kwamba jamaa kawafanya mpaka washirika wake/wao wakuaminiwa waliokua ambao vwalikua hawawez pindua kwa US kwasasa wanaweza mjibu vyovyote bwana mkubwa

Kuhusiana nasuala la IRAN na KOREA hawajamaa waachwe tukama walivyo US hawawawezi tena hao jamaa.....
 
Tofauti na nchi zingine zote za middle East isipokua Israel, wairani Wana chuki na visasi Sana, toka wamepata Uhuru mwaka 1979 hawajawahi kuacha tukio la ovyo lipite bila majibu!
Kuilinda nchi yako pale inaposhambuliwa,ina kufanya uwe na chuki na kisasi?

Hivi unajua maana ya UZALENDO? Yaani unanishambulia mimi nikae kimya,hivi hata ww unakaaga kimya mtu akikushambulia?
 
Back
Top Bottom