Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,189
- 4,103
Bunge la Marekani limepitisha muswada ili kupambana na vile wanavyovisema kuwa ni vikwazo visivyo na mantiki, mateso na unyanyasaji kwa waislamu wa jamii ya Uighur nchini China.
Imelenga vile vikwazo vinavyowalenga wanachama wa serikali ya China na kumtaja kiongozi wa chama cha kikomunisti katika mkoa wa Xinjiang,Chen Quanguo.
Muswada huo bado unahitaji idhini kutoka kwa seneta na Rais Donald Trump.
Kwa upande wa China, Waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo ameoneshwa kutofurahishwa na kusema hatua hiyo ni ya ''uovu''.
Muswada wa haki za kibinadamu za Uighur wa mwaka 2019 ulipitishwa bungeni na wabunge 407 kwa 1 usiku wa Jumanne.
Kupitishwa kwake kunakuja mara baada ya Rais Trump kutia saini sheria inayounga mkono maandamano ya demokrasia mjini Hong Kong pia kusababisha ukandamizaji kutoka kwa China.
Thomas Massie kutoka chama cha Republican kutoka Kentucky, amepiga kura kupinga muswada huo wa Uighur, vilevile hakuupigia kura muswada wa Hong Kong.
Mwandishi wa BBC nchini China John Sudworth amesema kama muswada huu utapitishwa basi ''itaashiria jaribio muhimu sana la kimataifa kushinikiza China kuhusu kuwaweka kizuizini waislamu wengi wa Uighur na wale kutoka makundi mengine ya kiislam.''
Imelenga vile vikwazo vinavyowalenga wanachama wa serikali ya China na kumtaja kiongozi wa chama cha kikomunisti katika mkoa wa Xinjiang,Chen Quanguo.
Muswada huo bado unahitaji idhini kutoka kwa seneta na Rais Donald Trump.
Kwa upande wa China, Waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo ameoneshwa kutofurahishwa na kusema hatua hiyo ni ya ''uovu''.
Muswada wa haki za kibinadamu za Uighur wa mwaka 2019 ulipitishwa bungeni na wabunge 407 kwa 1 usiku wa Jumanne.
Kupitishwa kwake kunakuja mara baada ya Rais Trump kutia saini sheria inayounga mkono maandamano ya demokrasia mjini Hong Kong pia kusababisha ukandamizaji kutoka kwa China.
Thomas Massie kutoka chama cha Republican kutoka Kentucky, amepiga kura kupinga muswada huo wa Uighur, vilevile hakuupigia kura muswada wa Hong Kong.
Mwandishi wa BBC nchini China John Sudworth amesema kama muswada huu utapitishwa basi ''itaashiria jaribio muhimu sana la kimataifa kushinikiza China kuhusu kuwaweka kizuizini waislamu wengi wa Uighur na wale kutoka makundi mengine ya kiislam.''