17 September 2021
Unguja, Zanzibar
Makamu wa Kwanza wa Rais wa akutana na Balozi wa Marekani kujadili GNU na maendeleo ya Zanzibar
Makamu wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mh. Othman Masoud Othman amekutana na Mh. Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mh. Donald Wright na kufanya mazungumzo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman amesema kuwa ili kujenga nchi inayoendelea kiuchumi kunahitajika mageuzi ya msingi katika sera, mfumo bora wa uendeshaji, mshikamano pamoja na maridhiano ya kweli ya kisiasa na kijamii. Mheshimiwa Othman ameyasema hayo leo Ofisini kwake Migombani Jijini hapa, akiongea na ujumbe wa Balozi wa Marekani Nchini Tanzania, Bw. Donald Wright, uliofika kutahmini mwenendo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar (GNU).
Marekani na Zanzibar katika miezi kadhaa ya hivi karibuni, uhusiano wake umeimarika baada ya Zanzibar kusimamia katiba yake iliyofanikisha kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU), inayotambua vyama vyote vya kisiasa na kuvishirikisha katika kuunda serikali ya Umoja wa Kitaifa. Jambo hilo limepongezwa na Marekani na kusema ni mfano mzuri wa kuigwa.
Source : Zanzibar Kamili TV
Unguja, Zanzibar
Makamu wa Kwanza wa Rais wa akutana na Balozi wa Marekani kujadili GNU na maendeleo ya Zanzibar
Makamu wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mh. Othman Masoud Othman amekutana na Mh. Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mh. Donald Wright na kufanya mazungumzo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman amesema kuwa ili kujenga nchi inayoendelea kiuchumi kunahitajika mageuzi ya msingi katika sera, mfumo bora wa uendeshaji, mshikamano pamoja na maridhiano ya kweli ya kisiasa na kijamii. Mheshimiwa Othman ameyasema hayo leo Ofisini kwake Migombani Jijini hapa, akiongea na ujumbe wa Balozi wa Marekani Nchini Tanzania, Bw. Donald Wright, uliofika kutahmini mwenendo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar (GNU).
Marekani na Zanzibar katika miezi kadhaa ya hivi karibuni, uhusiano wake umeimarika baada ya Zanzibar kusimamia katiba yake iliyofanikisha kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (GNU), inayotambua vyama vyote vya kisiasa na kuvishirikisha katika kuunda serikali ya Umoja wa Kitaifa. Jambo hilo limepongezwa na Marekani na kusema ni mfano mzuri wa kuigwa.
Source : Zanzibar Kamili TV