Marekani yapiga marufuku kampuni za China kwa unyanyasaji wa Waislamu

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,442
3,353
Marekani imepiga marufuku mashirika 28 ya China kwa madai ya kuhusika katika unayanyasi wa kabila la Uighurs katika jimbo la Xinjianga nchini China.

Mashirika hayo sasa yameorodheshwa miongoni mwa yale yaliopigwa marufulku na taifa hillo hatua inayoyazuia kununua bidhaa kutoka kwa makampuni ya Marekani bila idhini ya Washington.

Mashirika hayo yaliolengwa yanashirikisha mashirika ya serikali na kampuni za kiteknolojia zinazoshughulika na vifaa vya ujasusi

Sio mara ya kwanza Marekani imechukua hatua kama hiyo dhidi ya mashirika ya China.

Mnamo mwezi Mei , utawala wa rais Trump uliiweka kampuni kubwa ya teknolojia Huawei katika orodha jhiyo kutokana na hofu ya kiusalama kuhusu bidhaa zake.

Idara ya biashara imesema kwamba mashirika hayo yanahusika na ukiukaji wa haki za kibinadamu na unyanyasaji.

Mashirika ya haki za kibinadamu Beijing yanasema kwamba mashirika kadhaa yananyanyasa Waislamu wa kabila la Uighurs katika kambi za vizuizi .

China imevitaja vituo hivyo kuwa vya kukabiliana na watu wenye itikadi kali.

Idara hiyo ya biashara imesema katika uamuzi wake siku ya Jumatatu kwamba mashirika hayo 28 yanahusika katika kampeni ya China ya ukandamizaji , kuwakamata na kuwazuia watu kadhaa na ujasusi wa hali ya juu dhidi ya Uighurs, Kazaks pamoja na makundi mengine ya Waislamu walio wachache.

Shirika la usalama wa umma la Xinjiang pia lipo katika orodha hiyo pamoja na mashirika mengine 19 madogo madogo.

Kampuni za Hikvision, Dahua Technology na Megvii ni miongoni mwa mashirika manane ya kibiashara yaliopo katika orodha hiyo , yote ambayo yanaangazia utambuzi wa sura ya mtu.

Hikvision ni mojawapo ya kampuni ilio na vifaa vikubwa vya uchunguzi duniani.

Kamera ya Hikvision


Hikvision ni kampuni inayoshughulikia vifaa vya Ujasusi
Marekani na China zipo katikati ya mgogoro wa kibiashara na zimetuma ujumbe Washington kwa mkutano kuhusu wasiwasi uliopo kati yao wiki iliopita.

Je Uighurs ni akina nani?
Watu wa kabila la Uighurs ni Waislamu Waturuki. Ni asilimia 45 ya watu wanaoishi katika jimbo la Xinjiang ; 40% ni watu wa kabila Han Chinese.

China ilichukua udhibti wa eneo hilo 1949 baada ya kuliangamiza jimbo la mashariki mwa Turkestan.

Tangu wakati huo kumekuwa na uhamiaji mkubwa wa watu wa kabila la Han Chinese na watu wa kabila la Uighurs wanahofia mmomonyoko wa utamaduni wao

Xinjiang ni jimbo huru ndani ya China, kama Tibet iliopo kusini mwake.
 
Hivi tangu lini taifa ambalo limeanzishwa na kujengwa juu ya msingi wa dhuluma na damu za mamilioni ya watu wasio na hatia likawa na nguvu ya kuwafundisha wengine kuhusu kuhusu haki za raia ?

Nchini kwake Marekani ameua maelfu ya wahindi wekundu na mamilioni ya watumwa weusi. Nje ya mipaka yake makampuni ya Kimarekani kama Ford Motors yalishirikiana kiukaribu sana na chama cha Wanazi ambacho kilisababisha vifo vya mamilioni ya watu duniani kote.

Marekani atatumia kila mbinu chafu kutaka kumzuia Uchina lakini hataweza kwasababu amechelewa sana. Makosa yote ya Uchina kuwa na nguvu leo yalifanywa na Richard Nixon.

It's too late to contain Communist China.
 
Hivi tangu lini taifa ambalo limeanzishwa na kujengwa juu ya msingi wa dhuluma na damu za mamilioni ya watu wasio na hatia likawa na nguvu ya kuwafundisha wengine kuhusu kuhusu haki za raia ?

Nchini kwake Marekani ameua maelfu ya wahindi wekundu na mamilioni ya watumwa weusi. Nje ya mipaka yake makampuni ya Kimarekani kama Ford Motors yalishirikiana kiukaribu sana na chama cha Wanazi ambacho kilisababisha vifo vya mamilioni ya watu duniani kote.

Marekani atatumia kila mbinu chafu kutaka kumzuia Uchina lakini hataweza kwasababu amechelewa sana. Makosa yote ya Uchina kuwa na nguvu leo yalifanywa na Richard Nixon.

It's too late to contain Communist China.
Hii ni kwa mtazamo wako boss!!
 
Hii ni kwa mtazamo wako boss!!
Marekani hawezishinda hii vita dhidi ya Uchina. Alijaribu miaka ya 1949, 1950-53, 1964 na 1993 wakati Uchina hana nguvu kama hii ya leo lakini akashindwa. Mwaka huu 2019, Uchina ana nguvu kubwa kuliko wakati wowote ule katika historia yake, unadhani Marekani atamzuia kweli ?
 
Marekani hawezishinda hii vita dhidi ya Uchina. Alijaribu miaka ya 1949, 1950-53, 1964 na 1993 wakati Uchina hana nguvu kama hii ya leo lakini akashindwa. Mwaka huu 2019, Uchina ana nguvu kubwa kuliko wakati wowote ule katika historia yake, unadhani Marekani atamzuia kweli ?
Wait and see who will win kama unahisi trump anafanya kitu ambacho anashimdwa basi ange kiacha maana next year ni uchaguzi inakua kama disadvantage kwake na ukichikulia anataka kurud ikulu! When it comes to economy few president are match to him!
 
Wait and see who will win kama unahisi trump anafanya kitu ambacho anashimdwa basi ange kiacha maana next year ni uchaguzi inakua kama disadvantage kwake na ukichikulia anataka kurud ikulu! When it comes to economy few president are match to him!
Ikulu ya Marekani walikuwepo watu hatari mno kama Lyndon B Johnson, Richard Nixon, Ronald Reagan, Bush Jr, Bush Sr na Bill Clinton lakini hawakuizuia Uchina kufika hapa ilipofika leo. Unadhani Trump ndiyo ataweza ?
 
Ikulu ya Marekani walikuwepo watu hatari mno kama Lyndon B Johnson, Richard Nixon, Ronald Reagan, Bush Jr, Bush Sr na Bill Clinton lakini hawakuizuia Uchina kufika hapa ilipofika leo. Unadhani Trump ndiyo ataweza ?
AKIKUJIBU UNUTAG
 
Siungi Mkono Unyanyasaji wa Waislam Unaofanywa Na CHINA Ila US Mnafiq sana asee yeye hajioni anayo yafanya

US na CHINA Wale Wale US Kapiga Marufuku Raia Wanchi Za KIISLAM Takriban 8 Kuingia Nchini Mwao

US CHINA Wote washenzi

Hlaf hili suala ukilitazama kwa undani unaona nimambo yale yale ya US Kubinywa Na CHINA Kiuchumi

Ila anatafta Attention 2 nchi Nyengne za WAISLAM
 
Kwani kumbe waislamu huwa wananyanyaswa kweli mi nilifikiri watu wa kulalamika tu ndio wamezoea.
 
Pale Marekani anapomtetea muislam, jua kuna ajenda nyuma ya pazia, sababu walishasema waislam wasiingie marekani, leo hii marekani huyo huyo anawatetea huko uchina
 
Ikulu ya Marekani walikuwepo watu hatari mno kama Lyndon B Johnson, Richard Nixon, Ronald Reagan, Bush Jr, Bush Sr na Bill Clinton lakini hawakuizuia Uchina kufika hapa ilipofika leo. Unadhani Trump ndiyo ataweza ?
China imekuja kuwa tishio kwa marekani miaka hii ya 2000s.Huko nyuma labda uniambie USSR/Russia,Huko nyuma marekani hakuwahi kuwekeza nyuvu kupambana na china kama livyowekeza kwa USSR.Sasa ukiniambia walishindwa sijui una maana gani.
 
PALE MAREKANI ANAPOMTETEA MUISLAM, JUA KUNA AJENDA NYUMA YA PAZIA, SABABU WALISHASEMA WAISLAM WASIINGIE MAREKANI, LEO HII MAREKANI HUYO HUYO ANAWATETEA HUKO UCHINA
Wana ajenda zao zasiri 2 washenzi wale hawana u2 wa namna hii wakat wao wenyewe wanawanyanyasa 2
 
China imekuja kuwa tishio kwa marekani miaka hii ya 2000s.Huko nyuma labda uniambie USSR/Russia,Huko nyuma marekani hakuwahi kuwekeza nyuvu kupambana na china kama livyowekeza kwa USSR.Sasa ukiniambia walishindwa sijui una maana gani.
Hio elf 2s walikua wapi mpaka wakawangoja ss hv kuja kua hv walivyo

Maendeleo yapo huru na hua yanaonekanika CHINA Alianza kuendelea zamani japo katika miaka hio ulosema ya 2000s ndio alikua ana kua kwakasi ya ajabu

Kama US alishindwa kumdhibiti wakati akiwa anakua kwamwendo wa kinyonga usidhanie kama ataweza kumzuia kwa ss wakat ana spidi ya umeme

Tooo late........
 
Mada ishabadilika tena. Anayejadiliwa ni Marekani na siyo China tena kuwanyanyasa waislamu. Hapa ndiyo ujue hata wenye dini wenyewe hawajielewi kwasababu ya roho mbaya walizonazo kwasababu wenyewe kwa wenyewe hawapendani.

Marekani mnafiki na ana roho mbaya na China ana roho nzuri. China hao waislamu watese, wanyime social service zote na ikibidi uwa wote wasiwepo kwenye nchi yako maana mwisho wa siku watakuwa magaidi.

Marekani anawatetea waislamu walioko china wao wanaona ni mnafiki na China anaroho nzuri. China kamatia hapo hapo mpaka watie akili na warudi walikotoka. Hapa naungana na China sababu anaroho nzuri kuliko Marekani
 
Back
Top Bottom