Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,442
- 3,353
Marekani imepiga marufuku mashirika 28 ya China kwa madai ya kuhusika katika unayanyasi wa kabila la Uighurs katika jimbo la Xinjianga nchini China.
Mashirika hayo sasa yameorodheshwa miongoni mwa yale yaliopigwa marufulku na taifa hillo hatua inayoyazuia kununua bidhaa kutoka kwa makampuni ya Marekani bila idhini ya Washington.
Mashirika hayo yaliolengwa yanashirikisha mashirika ya serikali na kampuni za kiteknolojia zinazoshughulika na vifaa vya ujasusi
Sio mara ya kwanza Marekani imechukua hatua kama hiyo dhidi ya mashirika ya China.
Mnamo mwezi Mei , utawala wa rais Trump uliiweka kampuni kubwa ya teknolojia Huawei katika orodha jhiyo kutokana na hofu ya kiusalama kuhusu bidhaa zake.
Idara ya biashara imesema kwamba mashirika hayo yanahusika na ukiukaji wa haki za kibinadamu na unyanyasaji.
Mashirika ya haki za kibinadamu Beijing yanasema kwamba mashirika kadhaa yananyanyasa Waislamu wa kabila la Uighurs katika kambi za vizuizi .
China imevitaja vituo hivyo kuwa vya kukabiliana na watu wenye itikadi kali.
Idara hiyo ya biashara imesema katika uamuzi wake siku ya Jumatatu kwamba mashirika hayo 28 yanahusika katika kampeni ya China ya ukandamizaji , kuwakamata na kuwazuia watu kadhaa na ujasusi wa hali ya juu dhidi ya Uighurs, Kazaks pamoja na makundi mengine ya Waislamu walio wachache.
Shirika la usalama wa umma la Xinjiang pia lipo katika orodha hiyo pamoja na mashirika mengine 19 madogo madogo.
Kampuni za Hikvision, Dahua Technology na Megvii ni miongoni mwa mashirika manane ya kibiashara yaliopo katika orodha hiyo , yote ambayo yanaangazia utambuzi wa sura ya mtu.
Hikvision ni mojawapo ya kampuni ilio na vifaa vikubwa vya uchunguzi duniani.
Hikvision ni kampuni inayoshughulikia vifaa vya Ujasusi
Marekani na China zipo katikati ya mgogoro wa kibiashara na zimetuma ujumbe Washington kwa mkutano kuhusu wasiwasi uliopo kati yao wiki iliopita.
Je Uighurs ni akina nani?
Watu wa kabila la Uighurs ni Waislamu Waturuki. Ni asilimia 45 ya watu wanaoishi katika jimbo la Xinjiang ; 40% ni watu wa kabila Han Chinese.
China ilichukua udhibti wa eneo hilo 1949 baada ya kuliangamiza jimbo la mashariki mwa Turkestan.
Tangu wakati huo kumekuwa na uhamiaji mkubwa wa watu wa kabila la Han Chinese na watu wa kabila la Uighurs wanahofia mmomonyoko wa utamaduni wao
Xinjiang ni jimbo huru ndani ya China, kama Tibet iliopo kusini mwake.
Mashirika hayo sasa yameorodheshwa miongoni mwa yale yaliopigwa marufulku na taifa hillo hatua inayoyazuia kununua bidhaa kutoka kwa makampuni ya Marekani bila idhini ya Washington.
Mashirika hayo yaliolengwa yanashirikisha mashirika ya serikali na kampuni za kiteknolojia zinazoshughulika na vifaa vya ujasusi
Sio mara ya kwanza Marekani imechukua hatua kama hiyo dhidi ya mashirika ya China.
Mnamo mwezi Mei , utawala wa rais Trump uliiweka kampuni kubwa ya teknolojia Huawei katika orodha jhiyo kutokana na hofu ya kiusalama kuhusu bidhaa zake.
Idara ya biashara imesema kwamba mashirika hayo yanahusika na ukiukaji wa haki za kibinadamu na unyanyasaji.
Mashirika ya haki za kibinadamu Beijing yanasema kwamba mashirika kadhaa yananyanyasa Waislamu wa kabila la Uighurs katika kambi za vizuizi .
China imevitaja vituo hivyo kuwa vya kukabiliana na watu wenye itikadi kali.
Idara hiyo ya biashara imesema katika uamuzi wake siku ya Jumatatu kwamba mashirika hayo 28 yanahusika katika kampeni ya China ya ukandamizaji , kuwakamata na kuwazuia watu kadhaa na ujasusi wa hali ya juu dhidi ya Uighurs, Kazaks pamoja na makundi mengine ya Waislamu walio wachache.
Shirika la usalama wa umma la Xinjiang pia lipo katika orodha hiyo pamoja na mashirika mengine 19 madogo madogo.
Kampuni za Hikvision, Dahua Technology na Megvii ni miongoni mwa mashirika manane ya kibiashara yaliopo katika orodha hiyo , yote ambayo yanaangazia utambuzi wa sura ya mtu.
Hikvision ni mojawapo ya kampuni ilio na vifaa vikubwa vya uchunguzi duniani.
Hikvision ni kampuni inayoshughulikia vifaa vya Ujasusi
Marekani na China zipo katikati ya mgogoro wa kibiashara na zimetuma ujumbe Washington kwa mkutano kuhusu wasiwasi uliopo kati yao wiki iliopita.
Je Uighurs ni akina nani?
Watu wa kabila la Uighurs ni Waislamu Waturuki. Ni asilimia 45 ya watu wanaoishi katika jimbo la Xinjiang ; 40% ni watu wa kabila Han Chinese.
China ilichukua udhibti wa eneo hilo 1949 baada ya kuliangamiza jimbo la mashariki mwa Turkestan.
Tangu wakati huo kumekuwa na uhamiaji mkubwa wa watu wa kabila la Han Chinese na watu wa kabila la Uighurs wanahofia mmomonyoko wa utamaduni wao
Xinjiang ni jimbo huru ndani ya China, kama Tibet iliopo kusini mwake.