Marekani yambana JK

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Labda sasa usanii wa JK kuhusu mafisadi umefikia kikomo. Jamaa wakikaza uzi na nchi nyingine za magharibi basi labda yale tuliyokuwa tukiyapigia kelele kuhusu mafisadi yatatimia

Marekani yambana JK

na Kulwa Karedia
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

SERIKALI ya Marekani, imemtaka Rais Jakaya Kikwete, kuwakamata na kuwafikisha mahakamani vigogo pamoja na watu wote wanaohusishwa na kashfa za ufisadi, bila kujali nyadhifa kubwa wanazoshika serikalini.

Imesema katika kupambana na mafisadi, Rais Kikwete hapaswi kuangalia wadhifa wa mtu, awachukulie hatua wote wanaotuhumiwa bila kujali kama ni mawaziri au watu wenye nyadhifa kubwa serikalini.

Msimamo huo wa Marekani kuhusu vita dhidi ya mafisadi,ulitolewa juzi jijini Dar es Salaam na Balozi wa Marekani hapa nchini, Mark Green alipokuwa akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya miaka 232 ya uhuru wa taifa hilo.

“Rais Kikwete anatakiwa kuchukua hatua za kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote watakaobainika kuhusika na wizi wa mamilioni ya fedha za wananchi… tunataka kuona hilo linatakelezwa bila kujali ni nani na ana wadhifa gani,” alisema Balozi Green.

Balozi huyo alisema iwapo Rais Kikwete atafanya kazi ya kuwafikisha mahakamani viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi na tuhuma nyingine dhidi ya mali ya umma, atafanikiwa kurejesha imani kwa wananchi na mataifa ya nje yanayotoa misaada kwa Tanzania, ikiwemo Marekani yenyewe.

“Rais aliagiza kufanyika uchunguzi kupitia tume yake aliyounda kwa kipindi cha miezi sita na majibu yako karibu kutoka… tunategemea kupata majibu ya msingi na kuona nini kitafanyika kwa wale wote waliohusika,” alisema Balozi Green.

Balozi Green hakusita kuonyesha hisia zake kwa vyombo vya habari vya hapa nchini, alipovimwagia sifa kwa kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi.

Alisema vyombo vya habari vya Tanzania vinastahili sifa kutokana na kufichua vitendo vya ufisadi vinavyofanywa na baadhi ya viongozi waliopewa dhamana ya kuongoza taifa.

“Tanzania ina vyombo vya habari imara, ambavyo vimekuwa vikiripoti habari muhimu na kutoa changamoto dhidi ya viongozi walioko madarakani, na matokeo yake sasa yanaonekana,” alisema.

Akizungumzia tatizo la mpasuko wa kisiasa Zanzibar, alisema wakati Rais Kikwete anaingia madarakani mwaka 2005, aliahidi katika hotuba yake kumaliza tatizo hilo kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) jambo ambalo lilitia matumaini makubwa katika jumuia ya kimataifa.

“Tulivutiwa na kauli yake pale aliposema suala hili atalipatia ufumbuzi haraka na analipa kipaumbele zaidi, nadhani sote tunapaswa kumsaidia katika hili ili kupata mafanikio,” alisisitiza.

Alisema Marekani kama rafiki wa Tanzania na Zanzibar kwa miaka mingi, haioni sababu ya pande hizo mbili kuogopa kuzungumzia matatizo yanayozikabili.

“Katika kufanya mazungumzo kila upande unatoa dukuduku lake, na wakati huo kila upande unapata kile ambacho ulikuwa unategemea na hatimaye kufikia makubaliano,” alisema Balozi Green.

Akizungumzia uhuru wa taifa hilo, alisema mwasisi wake, Jenerali George Washington alifanya kazi kubwa ya kuikomboa Marekani kutoka kwenye makucha ya wakoloni na hatimaye kuwa taifa huru ambalo limekuwa mhimili wa demokrasia na maendeleo duniani.

Tamko hilo la Marekani liliifanya serikali kusisitiza kauli yake ambayo imekuwa ikiitoa kila mara kuwa, wale waliohusika na wizi wa fedha za umma watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Mwakilishi wa serikali katika sherehe hizo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, aliwaambia waandishi wa habari kuwa kinachotakiwa ni Watanzania kuwa na subira kwa vile baada ya ripoti ya timu ya rais ya kuchunguza wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), watakaobainika kuhusika watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

“Kweli Balozi Green kazungumzia suala hili, mimi napenda kuwaambia Watanzania kuwa wawe na subira, kwa hili tunaamini wale wote watakaobainika kuhusika, sheria itafuata mkondo wake tu,” alisisitiza Waziri Masha.

Alisema serikali haiungi mkono vitendo vya ufisadi vinavyoendelea kutokea, na kwamba vyombo vya dola vinalishughulikia kwa nguvu zote tatizo hilo.

Kuhusu ushirikiano na Marekani, Waziri Masha alisema, Tanzania itaendelea kushirikiana na taifa hilo katika nyanja mbalimbali, na kuwataka Watanzania kujitolea kulitumikia taifa lao kama ilivyo kwa Wamarekani bila kujali itikadi za kisiasa.

Msimamo huu wa Marekani unaweza kumuweka Rais Kikwete katika wakati mgumu iwapo ripoti ya timu yake itawataja baadhi ya viongozi wa serikali na wafanyabiashara wakubwa wanaodaiwa kuchangia kampeni za CCM katika uchaguzi mkuu wa 2005, kuwa wahusika katika wizi wa fedha za EPA.

Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Mzee Rashid Kawawa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, wasomi na mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini.
 
Nilishwaambia wasipofanya hivyo...Na mimi nafungua kesi hapa marekani na kupeleka issue hii kwenye congress!
Wao wanafikiri tunacheza!
Tuko serious...!Na balozi keshwaambia kuwa hata wao walipiga vita ya Mkoloni wakiongozwa na George Washigton!
Wanjuwa kuwa hatuko huru...Lakini kuna MAMLUKI WANOALAZIMISHA KUWA TUKO HURU NA SASA TWENDE ZIMBABWE!
Nilishawaambia wayazingatie yale Mh Zitto aliyowaambia...Kuwa tunataka UHURU NA HAKI!
Kikwete na serikali yake wanajuwa kuwa kifo cha siasa za vita ya kupeleka wanajeshi wetu kumwondoa Mugabe imekwamishwa na UFISADI unaoikabili serikali yetu!
Na mimi naahidi kuendelea kuwa BALOZI WA WANYONGE HAPA USA!
WE WANT JUSTICE...AND WE WANT FREEDOM!
Tunashukuru kwa WAMAREKANI KUTUELEWA NA NI MATUMAINI KUWA HAKI KWA MTANZANIA IKO KARIBUNI!
 
Nilishwaambia wasipofanya hivyo...Na mimi nafungua kesi hapa marekani na kupeleka issue hii kwenye congress!
Wao wanafikiri tunacheza!
Tuko serious...!Na balozi keshwaambia kuwa hata wao walipiga vita ya Mkoloni wakiongozwa na George Washigton!
Wanjuwa kuwa hatuko huru...Lakini kuna MAMLUKI WANOALAZIMISHA KUWA TUKO HURU NA SASA TWENDE ZIMBABWE!
Nilishawaambia wayazingatie yale Mh Zitto aliyowaambia...Kuwa tunataka UHURU NA HAKI!
Kikwete na serikali yake wanajuwa kuwa kifo cha siasa za vita ya kupeleka wanajeshi wetu kumwondoa Mugabe imekwamishwa na UFISADI unaoikabili serikali yetu!
Na mimi naahidi kuendelea kuwa BALOZI WA WANYONGE HAPA USA!
WE WANT JUSTICE...AND WE WANT FREEDOM!
Tunashukuru kwa WAMAREKANI KUTUELEWA NA NI MATUMAINI KUWA HAKI KWA MTANZANIA IKO KARIBUNI!

Siye tunasubiri tu kuona JK anawashughulikia mafisadi wote akiwemo Mkapa na kuhakikisha Kiwira Coal Plant inarudishwa chini ya umiliki wa Watanzania.
 
Moderators, naomba msaada tafadhali... Hivi Balozi Green sio mwanachama wa JF kweli? Maana naona kama vile anazungumza in our style.... I suspect atakuwa ni regular visitor humu...

Welcome to JF Balozi Green... This is the only place where Tanzanians could sensibly apply the America's "First Amendment" freely. Hopefully, we're gonna incorporate it in our dilapidated constitution in the near future..
 
Awapeleke mahakamani? Shutubutuuuuuuuuuuuuu!!!!

Naam lazima tumshinikize afanye hivyo, kama alifikiri kuongoza nchi ni lelemama basi aachie ngazi ili 2010 tumpate kiongozi shupavu ambaye siku zote atahakikisha sheria za nchi zinafuatwa bila kumuogopa yeyote yule hata kama ana wadhifa mkubwa kiasi gani au ni tajiri kiasi gani. Tumechoka na viongozi wasanii, wakafute sehemu nyingine za kufanyia usanii wao.
 
Hivi kwa nini inafikia hadi Marekani wambane Kikwete kuhusu ufisadi Tanzania? It doesn't make sense to me....
 
Atabanwa tu Nyani...Mbona mlitaka mmarekani ambane Mugabe na sasa anambana Kikwete mnachukia?

Double standards hazitatufikisha mahali especially tukiwa na mawazo hayo ya ki social darwnism!

UHURU IS AROUND THE CORNER AND JK should act accordingly!

Naona na yeye yuko huko JAPAN KWENYE G8 summit!
Nasikilizia!
 
Atabanwa tu Nyani...Mbona mlitaka mmarekani ambane Mugabe na sasa anambana Kikwete mnachukia?
Double standards hazitatufikisha mahali especially tukiwa na mawazo hayo ya ki social darwnism!

UHURU IS AROUND THE CORNER AND JK should act accordingly!

Naona na yeye yuko huko JAPAN KWENYE G8 summit!
Nasikilizia!

"Mlimtaka".....kina nani hao?
 
Atabanwa tu Nyani...Mbona mlitaka mmarekani ambane Mugabe na sasa anambana Kikwete mnachukia?

Double standards hazitatufikisha mahali especially tukiwa na mawazo hayo ya ki social darwnism!

UHURU IS AROUND THE CORNER AND JK should act accordingly!

Naona na yeye yuko huko JAPAN KWENYE G8 summit!
Nasikilizia!

Kwa kuwa tuna reference kwamba mambo mengi yanayohusiana na "Nchi za Nje" yanapewa priority na serikali yetu ya Kidanganyika basi na sisi tupunguze wasiwasi kwamba kwa kuwa this time wazo hili limetokea "Nchi za Nje" (especially Marekani) basi lazima something will be done in the near future.
 
Naam lazima tumshinikize afanye hivyo, kama alifikiri kuongoza nchi ni lelemama basi aachie ngazi ili 2010 tumpate kiongozi shupavu ambaye siku zote atahakikisha sheria za nchi zinafuatwa bila kumuogopa yeyote yule hata kama ana wadhifa mkubwa kiasi gani au ni tajiri kiasi gani. Tumechoka na viongozi wasanii, wakafute sehemu nyingine za kufanyia usanii wao.

Kwa mtaji huu tunahitaji Raisi mpya, I cant see it happening under JK na sirikali yake.
 
Bwana nchi yetu kwa miaka kadhaa sasa imekuwa ikuyumba katika joto la nchi za magharibi. Viongozi wetu wanapigishwa makitaimu kweli kweli.
Naamini Marekani wakisema ni kama enzi za shule ambapo kiranja alikuwa kila kitu. Akisema hata kama mwalimu hajatoa maagizo unaufyata. hapa ndivyo inavyokwend kuwa. Subirini mtaona wenyewe.
Si mnakumbuka Denmark tu ilitupeleka puta mpaka wakaupeleka mswada wa takukuru(takatakaza wakuru) mujengoni wakati walisharefusha sharubu?
 
Akizungumzia uhuru wa taifa hilo, alisema mwasisi wake, Jenerali George Washington alifanya kazi kubwa ya kuikomboa Marekani kutoka kwenye makucha ya wakoloni na hatimaye kuwa taifa huru ambalo limekuwa mhimili wa demokrasia na maendeleo duniani.

Tamko hilo la Marekani liliifanya serikali kusisitiza kauli yake ambayo imekuwa ikiitoa kila mara kuwa, wale waliohusika na wizi wa fedha za umma watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Cha MUHIMU NI HAKI KWA MTANZANIA...NA HAKI NI SHERIA and Vice Versa.
And to be more precise and OR MORE Specific... kama alivyosema balozi Green kuhusu UHURU WA USA CHINI YA GEORGE WASHINGTON...!
Basi na sisi tunataka UHURU WETU.
 
Labda sasa usanii wa JK kuhusu mafisadi umefikia kikomo. Jamaa wakikaza uzi na nchi nyingine za magharibi basi labda yale tuliyokuwa tukiyapigia kelele kuhusu mafisadi yatatimia

Marekani yambana JK


Akizungumzia uhuru wa taifa hilo, alisema mwasisi wake, Jenerali George Washington alifanya kazi kubwa ya kuikomboa Marekani kutoka kwenye makucha ya wakoloni na hatimaye kuwa taifa huru ambalo limekuwa mhimili wa demokrasia na maendeleo duniani.


Point of observation: Wakoloni walikua ni Waingereza ambao ni chimbuko la hao Wazungu huko Marekani pamoja na Wadachi na Wataliano, Wahindi wekundu ndio wenye nchi asilia,so Mr Green,Washington, Franklin and all American Caucasians are the same leopards with a goat's skin, inside they are still Leopard = (Euro. origins). Mengine yote aliyosema kuhusu Our President ni sawa kabisa. Ni hayo tu!
 
Point of observation: Wakoloni walikua ni Waingereza ambao ni chimbuko la hao Wazungu huko Marekani pamoja na Wadachi na Wataliano, Wahindi wekundu ndio wenye nchi asilia,so Mr Green,Washington, Franklin and all American Caucasians are the same leopards with a goat's skin, inside they are still Leopard = (Euro. origins). Mengine yote aliyosema kuhusu Our President ni sawa kabisa. Ni hayo tu!

Kwani hata huku Tanzania kulikuwa na WAARABU?
Si ni BANTU...SASA bantu kama Native Indians na sisi tuseme kwenye vita va uhuru ni sisi wenyewe tu?
Ndio historia ilivyo na UHURU ni uwezo wa kujiamulia mambo yetu kwa manufaa ya wananchi na kuweza kuipatia jamii maendeleo.
 
kufikishwa mahakamani si tatizo.. nani kawaambia kuwa hawatafikishwa mahakamani? kupata conviction kwa mtindo huu? forget it.
 
Back
Top Bottom