Marekani yakana kumfahamu jasusi aliyekamatwa Venezuela

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Raia wa Marekani anayeshikiliwa nchini Venezuela kwa madai ya kufanya ujasusi nchini humo hakutumwa na serikali ya Marekani, taarifa ya kiongozi wa ngazi ya juu katika serikali ya Marekani imebainisha.

Mwendesha Mashtaka mkuu wa Venezuela, Tarek Wiliam Saab alitangaza siku ya Jumatatu kuwa jasusi huyo aliyekamatwa wiki iliyopita, Matthew John Heath, atafunguliwa mashtaka ya ugaidi pamoja na usafirishaji haramu wa silaha.

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Venezuela William Saab.jpg


Uhusiano wa kidiplomasia kati ya Venezuela na Marekani unatajwa kuwa katika hali mbaya, huku Saab akieleza kuwa jasusi huyo wa Kimarekani akipanga kulipua viwanda vya OPEC na mifumo ya umeme ya nchi hiyo.

Lakini Mjumbe Maalum wa Marekani kwa Venezuela na Iran, Elliot Abrahams anaamini kuwa Heath hakutumwa na serikali ya Marekani, ingawa amesema kuwa hawezi kusema zaidi kwa sababu za kiusalama, na kwa kuwa Venezuela haina ubalozi wake mjini Caracas.

Awali Maduro alitangaza kukamatwa kwa jasusi huyo akiwa katika harakati za upelelezi wa kiwanda cha kusafisha mafuta katika eneo la Falcon Magharibi, akiwa na silaha maalum za upelelezi.

Afisa mmoja wa Serikali ya Marekani ambaye hakutaka jina lake kujulikana amesema kuwa inaendelea na uchunguzi kumhusu jasusi huyo. Saab, hata hivyo, amesema kuwa jasusi huyo aliingia Venezuela kupitia mpaka wa Colombia, na kwamba alikuwa amebeba "sarafu" iliyomuunganisha na Shirika la Upelelezi la Marekani, CIA, bila kutoa maelezo zaidi, huku akiongeza kuwa jasusi huyo alikuwa akifanya kazi pia na mkandarasi binafsi wa jeshi.

Saab ameongeza kuwa raia wengine watatu wa Venezuela wamekamatwa kuhusiana na tuhuma za kushiriki njama ya kulipua viwanda hivyo vya kuchakata mafuta.

Mwezi uliopita, wanajeshi wawili wa zamani wa Marekani walihukumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani kwa kuhusika na jaribio la mapinduzi lililoshindwa.

Chanzo: Al Jazeera
 
Ninachofahamu Agent ukishakua exposed kwenye eneo ulilopangiwa. Kukanwa na watu wa idara yako ni moja ya vitu unavyoambiwa mwanzoni kabisa unapopewa misheni. So sana hapo watakachafanya labda Extraction Mission
 
"As always, should you or any member your IM force be caught or killed, the Secretary will disavow all knowledge of your actions. This tape will self- destruct in five seconds. Good luck."

"Her dossier's available on I-COM 3. You have 48 hours to recruit Ms. Nordoff-Hall and meet me in Seville to receive further details. Should you or any member of your IM force be caught or killed, the Secretary will disavow all knowledge of your actions."

Ethan Hunt wala hashangazwi kwa hayo kwa sababu mara zote alikumbushwa kila alipopewa mission mpya kama inavyoonekana hapo juu!
 
Hiyo ni standard procedure ya CIA,,if you get caught,,you are on your own,,,watakuruka tu..kama una bahati,baadae watafanya back chanels na kufanya deal kwa siri ili uachiwe,lakini sio kukiri hadharani eti, huyo jasusi ni wa kwetu
 
Hiyo ni standard procedure ya CIA,,if you get caught,,you are on your own,,,watakuruka tu..kama una bahati,baadae watafanya back chanels na kufanya deal kwa siri ili uachiwe,lakini sio kukiri hadharani eti, huyo jasusi ni wa kwetu
Na bahati yenyewe lazima iwe na vitu ambavyo ni worth a trade to both sides.

Kwa mfano mwaka 2010 kulikuwa na Russian Spies 10 ambao walidakwa na FBI ndani ya US na kwa bahati kwenye magereza ya Russia nako kulikuwa na 3 former Russian Spies na one nuclear weapons specialist waliokuwa wanatumikia vifungo virefu vya uhaini na espionage, na wote hawa walikuwa double agents wakiitumikia pia UK na US kabla hawajadakwa.

Ikafanyika Spy Swap na kila mmoja akashika hamsini zake!
 
Na bahati yenyewe lazima iwe na vitu ambavyo ni worth a trade to both sides.

Kwa mfano mwaka 2010 kulikuwa na Russian Spies 10 ambao walidakwa na FBI ndani ya US na kwa bahati kwenye magereza ya Russia nako kulikuwa na 3 former Russian Spies na one nuclear weapons specialist waliokuwa wanatumikia vifungo virefu vya uhaini na espionage, na wote hawa walikuwa double agents wakiitumikia pia UK na US kabla hawajadakwa.

Ikafanyika Spy Swap na kila mmoja akashika hamsini zake!
Out of curiosity, Marekani bado imeiwekea vikwazo vya kiuchumi Venezuela. Unadhani zaidi ya kuwa na mtu mmoja ambaye tayari ameshakuwa denied na Marekani, Venezuela ina nini ambacho ni worth a trade kwa Marekani?
 
Out of curiosity, Marekani bado imeiwekea vikwazo vya kiuchumi Venezuela. Unadhani zaidi ya kuwa na mtu mmoja ambaye tayari ameshakuwa denied na Marekani, Venezuela ina nini ambacho ni worth a trade kwa Marekani?
Kuwa denied sio issue kwa sababu ukishakuwa deep cover operative wa taifa lolote lile, ukidakwa utakanwa tu kwa sababu taifa husika likikubali ina maana litakuwa linakubali kuhusika moja kwa moja kwenye serious crime against another nation.

Duniani kote, kosa la ujasusi ni kubwa sana na ndio maana Majasusi huwa wanapewa diplomatic cover. Kwa mfano, mtu wa CIA anaingia Tanzania kama Commerce Attache (Mwambata wa Biashar) ili hata akigundulika, asiweze kushitakiwa kwa sababu ana kinga ya kibalozi, kwahiyo the only thing a host nation can do ni kumtimua!!

So, kwa huyo jamaa kukanwa ni kawaida kabisa lakini jambo lamsingi ni umuhimu wake kwa CIA assuming ni kweli agent wao.

Na pia tukumbushane kwamba, Venezuela hawana mtu mmoja kwa maana ya huyu aliyedakwa sasa! Mwezi Mei kulikuwa na jaribio la mapinduzi nchini Venezuela ambapo 2 former US Special Forces walidakwa kwa tuhuma za kuhusika kwenye mapinduzi hayo.

Ni mwezi uliopita tu walipohukumiwa kwenda jela miaka 20!!

On top of that, Jordan Goudreau ambae pia ni former US Special Force akiwa pia ni mwanzilishi wa security firm ya Silvercorp USA anadai kuwa ndie mastermind wa mapinduzi yale yaliyoshindwa!!

So, jambo la msingi ni umuhimu wa hao watu kwa CIA!!

So kwa haraka haraka, utaona tayari Venuzuela wana Wamarekani 3 na wote former special forces ambao kwa sasa walikuwa kwenye private firms.

Na hizi private security firms ni kichaka kizuri sana kwa plausible deniability!
 
Mnaopenda kazi za usalama wa taifa mnaona hii??

Sio unalilia kazi ya usalama ili ukatishie watu na kitambulisho chako, Kuna wakati waweza pewa mission kwenda nchi za mbali, haya Sasa ndo umepewa mission, ukakamatwa halafu nchi ikakukana ***** SI utalia machozi ya damu wewe??

Usalama wa taifa sio kutishia watu kwenye mabanda ya supu tu nyau nyie.

Unalikuta jitu linasema oooh Mimi najiona naweza Sana kuwa usalama wa taifa, halafu nipo tayari kuitumikia nchi yangu.
 
Mnaopenda kazi za usalama wa taifa mnaona hii??

Sio unalilia kazi ya usalama ili ukatishie watu na kitambulisho chako, Kuna wakati waweza pewa mission kwenda nchi za mbali, haya Sasa ndo umepewa mission, ukakamatwa halafu nchi ikakukana ***** SI utalia machozi ya damu wewe??

Usalama wa taifa sio kutishia watu kwenye mabanda ya supu tu nyau nyie.

Unalikuta jitu linasema oooh Mimi najiona naweza Sana kuwa usalama wa taifa, halafu nipo tayari kuitumikia nchi yangu.
Povu la nn mwalimu wa darasa la pili C

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: T11
Kuwa denied sio issue kwa sababu ukishakuwa deep cover operative wa taifa lolote lile, ukidakwa utakanwa tu kwa sababu taifa husika likikubali ina maana litakuwa linakubali kuhusika moja kwa moja kwenye serious crime against another nation.

Duniani kote, kosa la ujasusi ni kubwa sana na ndio maana Majasusi huwa wanapewa diplomatic cover. Kwa mfano, mtu wa CIA anaingia Tanzania kama Commerce Attache (Mwambata wa Biashar) ili hata akigundulika, asiweze kushitakiwa kwa sababu ana kinga ya kibalozi, kwahiyo the only thing a host nation can do ni kumtimua!!

So, kwa huyo jamaa kukanwa ni kawaida kabisa lakini jambo lamsingi ni umuhimu wake kwa CIA assuming ni kweli agent wao.

Na pia tukumbushane kwamba, Venezuela hawana mtu mmoja kwa maana ya huyu aliyedakwa sasa! Mwezi Mei kulikuwa na jaribio la mapinduzi nchini Venezuela ambapo 2 former US Special Forces walidakwa kwa tuhuma za kuhusika kwenye mapinduzi hayo.

Ni mwezi uliopita tu walipohukumiwa kwenda jela miaka 20!!

On top of that, Jordan Goudreau ambae pia ni former US Special Force akiwa pia ni mwanzilishi wa security firm ya Silvercorp USA anadai kuwa ndie mastermind wa mapinduzi yale yaliyoshindwa!!

So, jambo la msingi ni umuhimu wa hao watu kwa CIA!!

So kwa haraka haraka, utaona tayari Venuzuela wana Wamarekani 3 na wote former special forces ambao kwa sasa walikuwa kwenye private firms.

Na hizi private security firms ni kichaka kizuri sana kwa plausible deniability!
Argument imekaa ki-proffesional , 👍
 
Kawaida sana,na hata jasusi huyo labda alikuwa anajua kuwa akikamatwa serikali yake itamkana.
 
Back
Top Bottom