kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,991
- 17,888
Marekani yafanya njama za kutorosha dhahabu ya tani 40 kutoka kwa ISIS huko Syria
Feb 14, 2019 02:43 UTC
Shirika moja la haki za binadamu la nchini Syria limefichua kwamba muungano unaoongozwa na Marekani unaofanya mashambulizi nchini Syria unafanya juhudi za kuwakinaisha viongozi na wanamgambo wa genge la kigaidi la Daesh (ISIS) waliozingirwa huko Deire Zor wajisalimishe ili muungano huo upate kuwapokonya dhahabu za tani 40 walizo nazo magaidi hao.
Mapigano baina ya wanamgambo wa Kikurdi wanaojiita "Vikosi vya Demokrasia vya Syria" na genge la kigaidi la Daesh huko mashariki mwa Mto Furat katika mkoa wa Deire Zor yangali yanaendelea.
Shirika hilo la haki za binadamu ambalo liko karibu na waasi nchini Syria limeripoti kuwa magaidi wa ISIS wanafanya juhudi za kubakia huko mashariki mwa Mto Furat kwa hali yoyote ile ingawa hivi sasa wamezingirwa katika eneo dogo lenye ukubwa usiofika kilomita mbili.
Shirika hilo limegusia jinsi Marekani na wavamizi wenzake wanavyoendelea kufanya mashambulizi nchini Syria kwa madai ya kupambana na magaidi wa Daesh na kusisitiza kuwa, lengo la mashambulizi hayo ni kuwalazimisha viongozi na wanamgambo wa ISIS wajisalimishe lakini hadi sasa wamegoma kujisalimisha wakitaka wapewe dhamana ya kuondoka salama kwenye eneo hilo.
Madai ya shirika hilo la haki za binadamu lililoko karibu na waasi huko Syria yametolewa katika hali ambayo siku ya Jumamosi wapinzani wa serikali ya Damascus walitangaza kuwa, Marekani na wanamgambo wa Kikurdi wameshafikia mwafaka na magaidi hao wa ISIS na tayari magaidi hao wameshakubali kuondoka katika ukingo wa mashariki mwa Mto Furat.
Feb 14, 2019 02:43 UTC
Shirika moja la haki za binadamu la nchini Syria limefichua kwamba muungano unaoongozwa na Marekani unaofanya mashambulizi nchini Syria unafanya juhudi za kuwakinaisha viongozi na wanamgambo wa genge la kigaidi la Daesh (ISIS) waliozingirwa huko Deire Zor wajisalimishe ili muungano huo upate kuwapokonya dhahabu za tani 40 walizo nazo magaidi hao.
Mapigano baina ya wanamgambo wa Kikurdi wanaojiita "Vikosi vya Demokrasia vya Syria" na genge la kigaidi la Daesh huko mashariki mwa Mto Furat katika mkoa wa Deire Zor yangali yanaendelea.
Shirika hilo la haki za binadamu ambalo liko karibu na waasi nchini Syria limeripoti kuwa magaidi wa ISIS wanafanya juhudi za kubakia huko mashariki mwa Mto Furat kwa hali yoyote ile ingawa hivi sasa wamezingirwa katika eneo dogo lenye ukubwa usiofika kilomita mbili.
Shirika hilo limegusia jinsi Marekani na wavamizi wenzake wanavyoendelea kufanya mashambulizi nchini Syria kwa madai ya kupambana na magaidi wa Daesh na kusisitiza kuwa, lengo la mashambulizi hayo ni kuwalazimisha viongozi na wanamgambo wa ISIS wajisalimishe lakini hadi sasa wamegoma kujisalimisha wakitaka wapewe dhamana ya kuondoka salama kwenye eneo hilo.
Madai ya shirika hilo la haki za binadamu lililoko karibu na waasi huko Syria yametolewa katika hali ambayo siku ya Jumamosi wapinzani wa serikali ya Damascus walitangaza kuwa, Marekani na wanamgambo wa Kikurdi wameshafikia mwafaka na magaidi hao wa ISIS na tayari magaidi hao wameshakubali kuondoka katika ukingo wa mashariki mwa Mto Furat.