Marekani yachukua tena taji lake kwenye Supercomputer kwa kuipiku China

ze kokuyo

JF-Expert Member
Jan 24, 2014
7,418
9,599
Marekani imechukua tena taji lake kwa kua na kompyuta ya kasi zaidi Duniani kwa kuipiku China.
Taji hilo lilikua likishikiliwa na China tangu mwaka 2013 kwa kuipiku Marekani kwa kua na Kompyuta yenye Kasi zaidi Duniani iliyoitwa Taihulight.

Supercomputer hiyo ya Sasa ya Marekani kwa jina 'Summit' ndio yenye Kasi kwa Sasa Duniani ikiizidi uwezo ile ya China kwa asilimia 60 ikiwa na uwezo wa kuchakata mahesabu 200 quadrillion kwa sekunde (ambayo ni sawa Trillion 200,000 kwa sekunde). Taihulight (ya Uchina) ilikua na uwezo wa kuchakata mahesabu 93 quadrillion kwa sekunde.

Kompyuta hiyo yenye ukubwa sawa na viwanja viwili vya tennis inatajwa kua ni nzito zaidi ya Ndege ya abiria ikiwa na uzito wa Tani 340,imeundwa kwa seva( servers) 4608 huku ikiwa na memori kubwa zaidi ya Petabytes 10 hutumia magaloni zaidi 4000 kwa dakika kuipooza ili isipate joto sana.

Supercomputer hiyo imegharimu kiasi Cha Dola milioni Mia mbili kuitengeneza ($200 millions)


Kompyuta hiyo yenye Kasi zaidi Duniani inaarifiwa kwamba itasaidia kwenye research mbalimbali kama za magonjwa hasa Cancer,nk,Pia na Mambo yahusuyo Jeshi.nk

US beats China to build world's fastest supercomputer that's one million times faster than a laptop | Daily Mail Online
 
Marekani imechukua tena taji lake kwa kua na kompyuta ya kasi zaidi Duniani kwa kuipiku China.
Taji hilo lilikua likishikiliwa na China tangu mwaka 2013 kwa kuipita Marekani kwa kua na Kompyuta yenye Kasi zaidi Duniani iliyoitwa Taihulight.

Supercomputer hiyo ya Sasa ya Marekani kwa jina 'Summit' ndio yenye Kasi kwa Sasa Duniani ikiizidi uwezo ile ya China kwa asilimia 60 ikiwa na uwezo wa kuchakata mahesabu 200 quadrillion kwa sekunde.

Kompyuta hiyo ambayo Ni nzito zaidi ya Ndege ya abiria imeundwa kwa seva( servers) 4608 huku ikiwa na memori kubwa zaidi ya Petabytes 10 hutumia magaloni zaidi 4000 kwa dakika kuipooza ili isipate joto sana.

Kompyuta hiyo yenye Kasi zaidi Duniani inaarifiwa kwamba itasaidia kwenye research mbalimbali kama za magonjwa hasa Cancer,nk,Pia na Mambo yahusuyo Jeshi.

US beats China to build world's fastest supercomputer that's one million times faster than a laptop | Daily Mail Online

Wenzetu wanasonga tu na technology inakua kwa kasi sana huko sisi tumebaki na siasa huku ndege moja ikizinduliwa na taifa zima
 
Ingekuwa hapa kwetu sijui ingezinduliwa na nani?! Ikiwa ndege ya kununua inazinduliwa na wanene wote wa nchi
Hahaha... nadhani tungeizindua pale Uwanja wa Taifa kwa kualika na viongozi wa nchi jirani waje kushuhudia. Bila kusahau ngoma za Asili na upasuaji wa matofali ungehusika kuonyesha ukomavu wa kompyuta yetu
 
Magaloni 4000 kwa dakika kuipoza......???
Mkuu Dude lenyewe unaambiwa Lina Tani 340 na ukubwa Kama viwanja viwili vya Tennis . Unategemea nn hapo,na linapiga kazi kwa Kasi hivyo injini zake kupoozwa lazima
 
Magaloni 4000 kwa dakika kuipoza......???
Ndio....usishangae miaka kadhaa ijayo ukaambiwa inatumia galoni tano tu za maji.

Kumbuka hata 1GB ilikuwa na uzito wa tani moja, sasa hivi hata ikidondoka huioni.
 
5b352deacb928.image.jpg


maxresdefault.jpg
 
Kuunganisha servers nyingi na kutumia hela nyingi kutengeneza computer conventional yenye speed kubwa zaidi si kitu cha kustaajabisha wala kufurahisha sana watu wanaofuatilia sana habari za computer.

Kuzidisha kasi bila kubadilisha kimsingi namna computer inavyofanya kazi kunaweza kuwa na manufaa katika fani chache za computer, lakini hakuleti mapinduzi ya kimsingi (paradigm shift) katika computer.

Computers zimetoka kwenye ukubwa wa majengo na viwanja vya tennis. Huko ndiko tulikotoka, hatuhitaji kurudi huko tena.

Ninaangalia zaidi upande wa Quantum Computers na challenges zake. Atakayeweza kutengeneza a stable Quantum Computer, will take the real prize.
 
Back
Top Bottom