Marekani: Ujenzi wa jiwe la amri 10 za Mungu wapingwa

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,409
20,766

Wanaharakati katika jimbo la Arkansas nchini Marekani, wanapinga ujenzi wa jiwe moja kubwa lililo na maandishi ya amri 10 za Mungu, kwenye uwanja wa makao makuu ya bunge la jimbo hilo.

Wanasiasa walipitisha kauli ya ujenzi wa mnara huo wa jiwe wenye urefu wa futi sita, katika eneo la Little Rock mnamo mwaka wa 2015.

Muungano wa haki na uhuru wa raia nchini Marekani ACLU, umewasilisha kesi mahakamani kutaka kuondolewa mara moja kwa mnara huo, ukisema kuwa unaleta mgawanyiko na unakiuka ahadi ya uhuru wa kidini kwa wote, katika katiba ya Marekani.

Seneta wa chama tawala cha Republican, Jayson Rapert, ambaye alikuwa katika mstari wa mbele wa kutaka kuwekwa kwa jiwe hilo , alisema kuwa hatua hiyo inaenda sambamba na msimamo wa mahakama kuu ya Marekani, na hivyo ni jambo zuri kwa jimbo la Arkansas.

Chanzo:
Muungwana Blog
 

Wanaharakati katika jimbo la Arkansas nchini Marekani, wanapinga ujenzi wa jiwe moja kubwa lililo na maandishi ya amri 10 za Mungu, kwenye uwanja wa makao makuu ya bunge la jimbo hilo.

Wanasiasa walipitisha kauli ya ujenzi wa mnara huo wa jiwe wenye urefu wa futi sita, katika eneo la Little Rock mnamo mwaka wa 2015.

Muungano wa haki na uhuru wa raia nchini Marekani ACLU, umewasilisha kesi mahakamani kutaka kuondolewa mara moja kwa mnara huo, ukisema kuwa unaleta mgawanyiko na unakiuka ahadi ya uhuru wa kidini kwa wote, katika katiba ya Marekani.

Seneta wa chama tawala cha Republican, Jayson Rapert, ambaye alikuwa katika mstari wa mbele wa kutaka kuwekwa kwa jiwe hilo , alisema kuwa hatua hiyo inaenda sambamba na msimamo wa mahakama kuu ya Marekani, na hivyo ni jambo zuri kwa jimbo la Arkansas.

Chanzo:
Muungwana Blog
Nadhani ili kuondoa utata, waisalamu nao wapewe slot ya kujenga mnara wa sheria zao. Kwa jinsi waislamu wanavyochukia ukristo (wao huwaita wakristo jina la MAKAFRI) hawatakubali kuona mnara huo ukijengwa.
 
Nadhani ili kuondoa utata, waisalamu nao wapewe slot ya kujenga mnara wa sheria zao. Kwa jinsi waislamu wanavyochukia ukristo (wao huwaita wakristo jina la MAKAFRI) hawatakubali kuona mnara huo ukijengwa.
Waislamu wanazikubali amri kumi kwani wanaikubali Torati ya Musa.
 
Je wataandika amri kumi za Mungu za Wakatoliki au Waprotestant.Kwani kwa dini hizi mpangilio wa amri kumi za Mungu ni tofauti na kuna moja ambayo kwa mwingine haipo
 
Waislamu wanazikubali amri kumi kwani wanaikubali Torati ya Musa.
Wahindu je?! Na wale wanaoabudu mizimu?! Na atheists je..?! NINASEMA ULE NI UBAGUZI..!
THERE IS NO SEPARATION OF RELIGION AND STATE!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom