Farolito
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 11,634
- 26,373
Waziri wa mambo ya Afya wa Marekani ameitaka serikali ya Tanzania kuweka wazi matokeo ya Kimaabara juu ya Kifo cha mwanamke aliedhaniwa kufa kwa ugonjwa unaodhaniwa kufanana na Ebola.
Alex Azar,akizungumza na wanahabari nchi Uganda amesema wanafuatilia suala hili kwa karibu na ni vizuri serikali ya Tanzania kuweka uwazi kwakua ni muhimu katika mapambano ya ugonjwa huu.
Aidha amesema juhudi zimafanywa kuhakikisha Tanzania inatimiza matakwa ya kimataifa ya shirika la afya duniani(WHO) kulinda afya za watanzania na watu wa ukanda mzima.
Serikali ya Tanzania ilitangaza Siku chache zilizopita kwamba hakuna ugonjwa wa Ebola nchini.
Chanzo:VOA Swahili
====
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile jana amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa masuala ya kupambana na magonjwa kutoka Marekani Bw. Robert Redfield.
Mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar Es Salaam yamelenga kuona namna gani nchi hizo mbili zinavyoweza kushirikiana katika kupambana na magonjwa hususani ya kuambukiza na milipuko.
Bwana Redfield amesema ziara yake nchini imekuja mara baada ya kutembelea nchi za Kongo DRC, Rwanda na Uganda ambazo zilikwishapata mlipuko wa ugonjwa Ebola na alitaka kujua Tanzania imejidhatiti vipi kukabiliana na ugonjwa huo usiingie nchini.
Kwa upande wake Naibu Waziri Dkt. Ndugulile amemuhakikishia Mkurugenzi huyo kuwa Tanzania imekuwa ikiwa mikakati ya utayari wa kukabiliana na Ebola hususani mipakani kwa kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa wahudumu wa afya na pia imepeleka vifaa vya uchunguzi vinavyotumika kupima joto la mwili kwa watu wote wanaopita mipakani na kama atashukiwa kuwa na virusi basi kuna vituo maalum vya afya vilivyotengwa kwa ajili ya kutoa matibabu.
Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Muhammad Kambi na Kaimu Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Janeth Mghamba kimeondoka na azimio la Serikali ya Tanzania na Marekani kuendelea kushirikiana katika kupambana na kudhibiti magonjwa kupitia program za Global Health Security.
Soma pia > WHO lalalamika ukosefu wa ushirikiano kutoka Tanzania kuhusu uwezekano wa uwepo wa visa vya Ebola
Alex Azar,akizungumza na wanahabari nchi Uganda amesema wanafuatilia suala hili kwa karibu na ni vizuri serikali ya Tanzania kuweka uwazi kwakua ni muhimu katika mapambano ya ugonjwa huu.
Aidha amesema juhudi zimafanywa kuhakikisha Tanzania inatimiza matakwa ya kimataifa ya shirika la afya duniani(WHO) kulinda afya za watanzania na watu wa ukanda mzima.
Serikali ya Tanzania ilitangaza Siku chache zilizopita kwamba hakuna ugonjwa wa Ebola nchini.
Chanzo:VOA Swahili
====
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile jana amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa masuala ya kupambana na magonjwa kutoka Marekani Bw. Robert Redfield.
Mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ofisi ndogo za wizara Jijini Dar Es Salaam yamelenga kuona namna gani nchi hizo mbili zinavyoweza kushirikiana katika kupambana na magonjwa hususani ya kuambukiza na milipuko.
Bwana Redfield amesema ziara yake nchini imekuja mara baada ya kutembelea nchi za Kongo DRC, Rwanda na Uganda ambazo zilikwishapata mlipuko wa ugonjwa Ebola na alitaka kujua Tanzania imejidhatiti vipi kukabiliana na ugonjwa huo usiingie nchini.
Kwa upande wake Naibu Waziri Dkt. Ndugulile amemuhakikishia Mkurugenzi huyo kuwa Tanzania imekuwa ikiwa mikakati ya utayari wa kukabiliana na Ebola hususani mipakani kwa kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa wahudumu wa afya na pia imepeleka vifaa vya uchunguzi vinavyotumika kupima joto la mwili kwa watu wote wanaopita mipakani na kama atashukiwa kuwa na virusi basi kuna vituo maalum vya afya vilivyotengwa kwa ajili ya kutoa matibabu.
Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Muhammad Kambi na Kaimu Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Janeth Mghamba kimeondoka na azimio la Serikali ya Tanzania na Marekani kuendelea kushirikiana katika kupambana na kudhibiti magonjwa kupitia program za Global Health Security.
Soma pia > WHO lalalamika ukosefu wa ushirikiano kutoka Tanzania kuhusu uwezekano wa uwepo wa visa vya Ebola