#COVID19 Marekani: Rais Biden ataka kutolewa Dola 100 kwa kila atakayepata chanjo ya COVID-19

Subirini kuna siku utakuja ugonjwa kama Ndui kisha akili za watu kama wewe zitakaa sawa.

Ugonjwa wa Ndui ulitishia kuangamiza entire population ya dunia kipindi hicho lakini chanjo iliingilia kati na ku-rescure situation.Siku zote katika maisha yako heshimu sana vitu viwili:
1.Mungu
2.Sayansi
 
Hii ni biashara ya upaku iliyoboreshwa....mnamkumbuka yule jamaa wa songea na biashara yake ya mahindi...yaani nipe nikupe pesa tupate,ikiwezekana ata watu wafee..

Kwa kifupi ni kwamba kuna watu tayari wamesha poteza pesa zao nyingi katka kuwekeza ktka hii biashara Sasa watatumia kila mbinu warudishe pesa zao kwa faida (RETAIN ON PROFIT)....
 
Jamaa katangaza hongo ya dola 100 za marekani ili raia wa Marekani wakubali kuchanjwa. Kwa taarifa tu ni kwamba zaidi ya asilimia 50 ya wamarekani wamekataa kabisa chanjo ya aina yoyote. Kuna watu wasiojielewa wanadhani upinzani wa chanjo upo Tanzania tu, la hasha! Sasa kuona hivyo Rais Biden ameamua kutangaza dau la hongo ya dola 100 kwa kila atakayeshawishika kuchanjwa! Kama Marekani inawashawishi raia wake kwa hongo ili wachanjwe, kwa nini tusiamini piaa kuwa Marekani inawashawishi kwa hongo viongozi wa nchi nyingine ili wakubali kupokea chanjo na kuwashawishi raia wao kuchanjwa!! Tofauti tu ni kuwa kwa marekani anayechanjwa ndiye anayepewa dola 100. Huku kwa wenzangu na mimi kwa nini tusiamini kuwa viongozi watapewa dola 100 kwa kila mtu atakayechanjwa? Zikiingia chanjo milioni moja, kwa nini tusiamini watahongwa kwa dola milioni mia moja ($100,000,000)? Kama huko kwao wanahonga kitu gani kitawazuia huku wasihonge? Mungu amewafunua peupe! Fungua link hapa chini usome uhayawani huo!
Sio hongo....ni motisha ili wakachanjwe
 
Hii ni biashara ya upaku iliyoboreshwa....mnamkumbuka yule jamaa wa songea na biashara yake ya mahindi...yaani nipe nikupe pesa tupate,ikiwezekana ata watu wafee..

Kwa kifupi ni kwamba kuna watu tayari wamesha poteza pesa zao nyingi katka kuwekeza ktka hii biashara Sasa watatumia kila mbinu warudishe pesa zao kwa faida (RETAIN ON PROFIT)....
Gwajima anapata umarufu kwa kupotosha umma ya wa Tanzania wengi wasio jielewa hi ni cheap popularity au political capital inayo tafutwa wengine wameanza kumpendekeza apewe Uraisi 2025......hapo hapo CCM inagawanyika, TISS izuie upotofu wa Gwajima una mazara zaidi ya chanjo,.....ila najiuliza laiti angekua Sh Ponda na msimamo kama huo sijui kama wange ka kimya kiasi hiki
 
Mwenzangu na mimi mwingjne aliyeingizwa mkenge huyu hapa!

Sisi Tz yatuhusu Nini?
Si mnapenda kusema Tanzania sio kisiwa?, Mzigo wa chanjo milioni moja ulitoka marekani! Na mbinu anayoitumia kushawishi chanjo ameiweka wazi! Tafakari!
 
Sio hongo....ni motisha ili wakachanjwe
Nenda Takukuru ukapate maneno mengine yanayotafisiriwa kuwa ni rushwa!! Haya tukubali kuwa ni "motisha", basi unajisikiaje viongozi wapewe "motisha" ya kuwahamasisha watu kuchanjwa ya dola 100 kwa kila mtu atakayekubali kuchanjwa! Zikiisha chanjo zote 1,000,000 wanapewa "motisha" ya dola 1,000,000 × 100 = $100,000 000!
 
Unajua huko marekani wataalam kama hawa waliobobea wamewafungua watu macho watu macho na si rahisi kurubuniwa. Anaanza kwa kukumwagia CV yake kwanza ili usidhani kuwa ni mbumbumbu mwenzio. Ukitaka kujibu hoja zake na wewe tupe CV yako kwanza! Walioingizwa mkenge saa hii wanajuta!! Halafu huna pa kulalamika na wanakuambia " si ulikubali mwenyewe? si ulisaini mwenyewe? Baada ya kuona kasi ya kujitokeza kuchanja imepungua sana ndio amekuja na plan 2 ya kupewa kitu kidogo, na kuna kila dalili hata hiyo plan 2 ya kutoa kitu kidogo atashindwa!! Zaidi ya nusu ya wamarekani wamegomea chanjo!! Elimika bure toka kwa daktari bingwa huyu hapa!!
 

Attachments

  • 2782210-62048362544228fdaa1c25b4a6a16ef4.mp4
    5.1 MB
Gwajima anapata umarufu kwa kupotosha umma ya wa Tanzania wengi wasio jielewa hi ni cheap popularity au political capital inayo tafutwa wengine wameanza kumpendekeza apewe Uraisi 2025......hapo hapo CCM inagawanyika, TISS izuie upotofu wa Gwajima una mazara zaidi ya chanjo,.....ila najiuliza laiti angekua Sh Ponda na msimamo kama huo sijui kama wange ka kimya kiasi hiki

Sipati picha kwa sh ponda wangemfanya nini 😱 kama hakuitwa gaidi 😂
 
We jamaa nenda kachanjwe acha kupotosha watu. Leo kuna dose milioni 1 mnahangaika kumbwela mbwela ipo siku mtazigombania dose na hazitotosha

Acha kushikiwa akili kijinga. Vaa nguo nenda kachanjwe
 
Gwajima anapata umarufu kwa kupotosha umma ya wa Tanzania wengi wasio jielewa hi ni cheap popularity au political capital inayo tafutwa wengine wameanza kumpendekeza apewe Uraisi 2025......hapo hapo CCM inagawanyika, TISS izuie upotofu wa Gwajima una mazara zaidi ya chanjo,.....ila najiuliza laiti angekua Sh Ponda na msimamo kama huo sijui kama wange ka kimya kiasi hiki
Gwajima yupi unamzungumzia hapa!?
 
Biden kutoa dola 100 kwa kila atakapigwa chanjo ya COVID-19

100x2399= 239,900

hii ni kweli?

====

Rais wa Marekani Joe Biden amesema kila mwananchi atakaekubali kupigwa chanjo dhidi ya ugonjwa wa COVID-19 atalipwa dola 100. Marekani ni nchi yenye chanjo za kutosha, na idadi kubwa ya watu wanaopinga kuchanjwa.

Rais wa Marekani Joe Biden amewashauri viongozi wa majimbo na miji yote nchini humo kuwalipa wakazi wao dola 100 ili wapigwe chanjo dhidi ya ugonjwa wa COVID-19.

Aidha ameweka sheria mpya zinazohitaji wafanyakazi wote wa serikali kuonyesha uthibitisho wa kupigwa chanjo au kulazimika kupimwa ugonjwa huo mara kwa mara, kuvaa barakoa pamoja na kuwekewa vikwazo vya kusafiri.

Hatua hizo za hivi karibuni ni miongoni mwa juhudi za Biden kujaribu kuwahamasisha Wamarekani wenye kupiga chanjo, huku aina mpya ya virusi vya corona iitwayo Delta ikiwa inaenea kote nchini humo, hasa miongoni mwa watu ambao bado hawakuchanjwa.

Marekani inashika mkia miongoni mwa nchi zilizoendelea kwa viwango vya watu waliochanjwa, licha ya kuwa na chanjo za kutosha zinazotolewa bure. Juhudi za Ikulu ya Marekaniza kuhamasisha wananchi kuchanjwa zimegonga ukuta, hasa kutokana na vuguvugu kubwa linalopinga chanjo hiyo, habari za uwongo zinazosambazwa kuhusu chanjo pamoja na migawanyiko ya kisiasa.

Uamuzi wa Biden kuhitaji mamilioni ya wafanyikazi wa serikali na makandarasi kuonyesha uthibitisho wa kupigwa chanjo unaonyesha kuwa Ikulu imeamua kuchukua msimamo mkali zaidi huku virusi hivyo vya aina ya Delta vikiwa vinazidi kuenea.

Biden amewaambia waandishi wa habari wa Ikulu, kwamba watu wengi sana wanafariki dunia au wanapoteza watu wanaowapenda.

Kulingana na Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC), takribani watu milioni 163.8 nchini Marekani ndiyo waliochanjwa dozi kamili ya chanjo kati ya idadi ya watu milioni 330.

Serikali ndiye mwajiri mkubwa zaidi nchini Marekani, na hatua ya Biden inaweza kuwa mfano wa kuigwa na makampuni binafsi ya kibiashara na taasisi nyingine wakiwa wanajitayarisha kurudisha wafanyakazi maofisini.

Wafanyakazi wa serikali ambao watashindwa kuonyesha uthibitisho wa kuchanjwa watalazimika kupimwa ugonjwa wa COVID-19 kila wiki au mara mbili kwa wiki pamoja na kuwekewa vikwazo vya kusafiri.

Wizara ya Fedha imesema serikali za majimbo zitatumia dola bilioni 350 zilizotengwa kwa ajili ya kupambana na corona kuwalipa wananchi dola 100 kila atakaekubali kupigwa chanjo ya kuwakinga na ugonjwa huo wa COVID-19.

Biden amesema anafahamu kuwa wale ambao tayari wameshachanjwa hawatofurahichwa na umauzi huo, lakini amelazimika kuchukua hatua hiyo ili kuwalinda Wamarekani wote.
Wamarekani wenyewe wanakataa kichanjwa kwa sababu wanazozijua wao kwann sis tumeletewa na tumeanza kuitumia ?
 
Ni kweli na ikumbukwe waziri mkuu wa Uingereza alipata maambukizi juu ya kichanjwa ila haikusaidia ukiniambia chanjo zao ni fek nakubali
Hawa viongozi wa mataifa mbalimbali wanajua kabisa madhara ya chanjo lakini kwa hongo wanayopokea wanaamua kufumba macho na kusema liwalo na liwe na wao wanafanyika chambo kwa kuwa wa kwanza kuchomwa chanjo bandia (siyo chanjo yenyewe), ili watu washawishike waingie chaka kichwa kichwa!! Haushangai, viongozi wakichanjwa mkono haupati sumaku ya kunasa vitu vya chuma kama sarafu. Duniani kote wanaochanja mwanzoni ni viongozi, lakini hakuna hata kiongozi mmoja duniani aliyeathirika na chanjo ya corona, lakini watu wa kawaida ndio wanaokufa na kulalamikia athari za chanjo!. Angalia usanii wanaofanya hapa:
View attachment 1874940
 
Subirini kuna siku utakuja ugonjwa kama Ndui kisha akili za watu kama wewe zitakaa sawa.

Ugonjwa wa Ndui ulitishia kuangamiza entire population ya dunia kipindi hicho lakini chanjo iliingilia kati na ku-rescure situation.Siku zote katika maisha yako heshimu sana vitu viwili:
1.Mungu
2.Sayansi
Sasa tatizo lipo wapi ikiwa corona nayo ni hatari watu wanakufa na ikiwa chanjo imeoneka ndio kuzuia hivyo vifo kwanini watu wakatae kutumia kitu kama hicho cha kuzuia vifo? ni kwamba wamekubali tu kufa?
 
Sasa tatizo lipo wapi ikiwa corona nayo ni hatari watu wanakufa na ikiwa chanjo imeoneka ndio kuzuia hivyo vifo kwanini watu wakatae kutumia kitu kama hicho cha kuzuia vifo? ni kwamba wamekubali tu kufa?
Kwani wewe huamini kuwa duniani kuna wajinga na wapumbavu au?
 
Gwajima anapata umarufu kwa kupotosha umma ya wa Tanzania wengi wasio jielewa hi ni cheap popularity au political capital inayo tafutwa wengine wameanza kumpendekeza apewe Uraisi 2025......hapo hapo CCM inagawanyika, TISS izuie upotofu wa Gwajima una mazara zaidi ya chanjo,.....ila najiuliza laiti angekua Sh Ponda na msimamo kama huo sijui kama wange ka kimya kiasi hiki
Marekani anagawa hela huko ili kushawishi watu kuchanjwa ila sisi huku tunaangaika na Gwajima halafu ushawishi zero.
 
Kwani wewe huamini kuwa duniani kuna wajinga na wapumbavu au?
Wajinga ni watu wa aina gani ambao umewakusudia wewe? Kwa sababu nikiangalia kwa wanaopinga na wanao kukubali chanjo kunapatikana makundi yote ya watu yani huwezi kusema kwamba kundi fulani lina msimamo fulani kuhusu chanjo kwa sababu ni aina fulani ya watu tofauti na upande mwengine.
 
Back
Top Bottom