Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,498
- 9,279
Marekani haitatuma wawakilishi rasmi kwenye Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi huko Beijing. Kwa mujibu wa Ikulu ya Marekani, njia mojawapo ya kukemea ukandamizaji wa jamii ya Uyghur nchini China.
"Hakuna afisa wa Marekani au mwanadiplomasia atakayekuwepo Beijing mwezi Februari," msemaji wa White House amesema. Kwa utawala wa Marekani, ni jambo lisilowazika kufanya "kana kwamba hakuna kilichotokea" wakati "haki za binadamu zinakiukwa mara kwa mara" nchini China, hasa katika mji wa Xinjiang. Katika suala hii maalum, Jen Psaki amefkwenda mbali na kutumia neno "mauaji ya kimbari" dhidi ya watu kutoka jamii ya Uyghurs.
Mashirika yasiyo ya kiserikali yanadai kuwa zaidi ya watu milioni moja kutoka jamii hiyo ya Waislamu walio wachache kwa sasa wanazuiliwa katika kambi.
Kabla ya uamuzi huo kurasimishwa, Wizara ya Mambo ya Nje ya China ilitishia kuchukua "hatua madhubuti" ikiwa maafisa wa Marekani wataendelea kutoa wito wa kususia michezo ya Olimpiki kwa njia ya kidiplomasia.
Wazo hilo lilikuwa likifikiriwa kwa wiki kadhaa, na mkutano wa video kati ya Joe Biden na Xi Jinping haukutosha kupunguza mvutano kati ya nchi hizo mbili.
Wanariadha wa Marekani hata hivyo watashiriki katika hafla hiyo ambayo itafanyika kuanzia Februari 4 hadi 20. Na bado kutakuwa na wanadiplomasia wa Marekani katika mji huo ili kuhakikisha usalama wa wajumbe wake.
Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki imeelezea furaha yake kwamba uamuzi huu unahusu masuala ya kisiasa pekee na kwamba wanariadha wa Marekani wanaweza kutetea nafasi zao, anaripoti mwandishi wetu wa Washington, Guillaume Naudin.
Kamati ya Olimpiki ya Marekani ilipinga kujitoa kabisa kwa Marekani, ikieleza kwamba kususia michezo hiyo huko Moscow mwaka 1980 na Los Angeles mwaka 1984, katika muktadha wa Vita Baridi, kumeonyesha kwamba matumizi ya kisiasa ya matukio haya yalikuwa kosa.
Wiki iliyopita, taasisi ya wataalam ya Marekani ilichapisha ushahidi wa kuhusika kwa rais wa China mwenyewe katika kile ambacho nchi nyingi za Magharibi zinakiona kuwa mauaji ya halaiki.
RFI Swahili
"Hakuna afisa wa Marekani au mwanadiplomasia atakayekuwepo Beijing mwezi Februari," msemaji wa White House amesema. Kwa utawala wa Marekani, ni jambo lisilowazika kufanya "kana kwamba hakuna kilichotokea" wakati "haki za binadamu zinakiukwa mara kwa mara" nchini China, hasa katika mji wa Xinjiang. Katika suala hii maalum, Jen Psaki amefkwenda mbali na kutumia neno "mauaji ya kimbari" dhidi ya watu kutoka jamii ya Uyghurs.
Mashirika yasiyo ya kiserikali yanadai kuwa zaidi ya watu milioni moja kutoka jamii hiyo ya Waislamu walio wachache kwa sasa wanazuiliwa katika kambi.
Kabla ya uamuzi huo kurasimishwa, Wizara ya Mambo ya Nje ya China ilitishia kuchukua "hatua madhubuti" ikiwa maafisa wa Marekani wataendelea kutoa wito wa kususia michezo ya Olimpiki kwa njia ya kidiplomasia.
Wazo hilo lilikuwa likifikiriwa kwa wiki kadhaa, na mkutano wa video kati ya Joe Biden na Xi Jinping haukutosha kupunguza mvutano kati ya nchi hizo mbili.
Wanariadha wa Marekani hata hivyo watashiriki katika hafla hiyo ambayo itafanyika kuanzia Februari 4 hadi 20. Na bado kutakuwa na wanadiplomasia wa Marekani katika mji huo ili kuhakikisha usalama wa wajumbe wake.
Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki imeelezea furaha yake kwamba uamuzi huu unahusu masuala ya kisiasa pekee na kwamba wanariadha wa Marekani wanaweza kutetea nafasi zao, anaripoti mwandishi wetu wa Washington, Guillaume Naudin.
Kamati ya Olimpiki ya Marekani ilipinga kujitoa kabisa kwa Marekani, ikieleza kwamba kususia michezo hiyo huko Moscow mwaka 1980 na Los Angeles mwaka 1984, katika muktadha wa Vita Baridi, kumeonyesha kwamba matumizi ya kisiasa ya matukio haya yalikuwa kosa.
Wiki iliyopita, taasisi ya wataalam ya Marekani ilichapisha ushahidi wa kuhusika kwa rais wa China mwenyewe katika kile ambacho nchi nyingi za Magharibi zinakiona kuwa mauaji ya halaiki.
RFI Swahili