Marekani kupitia ubalozi wake imesema inaendelea kufuatilia kwa karibu kesi ya Erick Kabendera.

Mh! Kuna Jambo juu ya huyu kabendera linawagusa moja kwa moja! Ben kimya,Gwanda kimya, lisu kimya , MKIRU Kimya Leo kbdra mayowe! Heko tz intelligence,

Nashauri mwachieni kabendera then mtengenezeeni mazingira akimbie nchi, mtakua mmewakata maini mabeberu. Mwalimu alikua very intelligent kwa mtego wa Kambona by then. (Though Kambona was right lakini amani ya nchi ilikua muhim zaidi)
Huoni kuwa kutengeneza mazingira ya kumfukuza ni kuendelea kukiuka haki za binadamu.
 
Serikal yetu nayo kupitia Ubalozi wetu uliopo Washington DC unafuatilia kwa karibu Sintofahamu ya Wafungwa wa Guantanamo bay wa tangu 2001 ambao baadhi yao walifungwa kwa zaid ya muongo mmoja na kuachiwa huru bila ya kukutwa na hatia na wengine kuhmishiwa kwenye Magereza mengine

Watetezi wa Ushoga na usagaji wanataka kuingilia uhuru wa Mahakama na mifumo yetu

Tutatetea Nchi yetu kwa Gharama zote kama wao wanavyotetea Nchi zao kwa gharama


Walitumia Sheria gani kumchukua Scaba scuba wakati kwa tuhuma zake angeweza kushtakiwa hapa Nchini

Wakatetee kwanza Watu wanaouwa Syria waliyoichafua kwa kusambaza Silaha kwa makundi ya Wahaini ili wachote mafuta

Rais Magufuli aachwe anyooshe Nchi asibabaishwe na Watetezi wa Ushoga
Iko hivi!!
Magofool anatenda uhalifu dhidi ya katiba!!

Eti "aachwe"! Umwache mwendawazimu mwenye rungu? We kweli punguani.
 
Kuna uovu gani unafanyika hapa ambao haujawahi fanyika US?
Unamaana na sisi tuanze kununua watumwa kama ilivyokuwa marekani miaka ile!?
Ccm hata mkitwangwa kinuni pamoja na ngano hamuivi.
 
Unamaana na sisi tuanze kununua watumwa kama ilivyokuwa marekani miaka ile!?
Ccm hata mkitwangwa kinuni pamoja na ngano hamuivi.

Marekani eti imeguswa kwa Kabendera kuwekwa Mahabusu kuliko Kashoghi kuchunwa ngozi ya kichwa hadi kufa akiwa Ubalozi wa Saudia Nchini Uturuki
 
pumbavu, punguwani huna akili
kabla ya kuwaza huo upumbavu wako Waite mkeo na watoto wako waangalie Kama robo saa hivi, ukimaliza mpigie Bibi kijijini halafu uje uandike Tena

it's a disgrace kuwa na mtanzania Kama wewe unayejiita raia mwema
Ila ni sifa kuwa na kiongozi mtanzania anaeteka watu,kupiga risasi watu bungeni,kubambikia watu kesi,kuuwa waandishi wa habari,kubomolea watu nyumba bila malipo yoyote hizi ndio sifa za tanzania mpya kama mnavyo inadi
 
Acheni Upuuzi hivi sisi mambo yao Marekani huwa tunawaingilia? au mnadhani na huko Kwao ni Kusafi hivyo? Utajiri wa Marekani, Nguvu yao Kijeshi na Kiusalama bila kusahau kupenda Kwao kutoa Misaada Afrika kwa Kutumia Rasilimali zetu wenyewe ndizo zinawafanya mshindwe kujua kuwa hata nao wana Matendo yao mabaya tu ila tatizo la Watanzania wengi hampendi Kufuatilia mambo mbalimbali na mnabaki kudakia dakia tu.

Tanzania ni nchi Huru na kamwe hatutotishwa wala Kuyumbishwa na Wamarekani. Tupo pia tayari kwa lolote. Kama kweli Wamarekani wanataka Haki za Binadamu na wanazingatia hilo sana watujibu Waafrika ni kwanini wao kupitia CIA walimuua vibaya Baba wa Taifa la DRC Hayati Lumumba kiasi kwamba hadi leo hii hiyo nchi haitawaliki huku bado wakiendelea kuinyonya tu pamoja na Washirika wao wakuu Waingereza, Wafaransa bila kuwasahau Warusi pia na Ushahidi wa hili upo kila mara kupitia Literature / Publications mbalimbali.

Ninachojua tu ni kwamba Mamlaka za Tanzania siyo Wapumbavu Kumkamata huyo Mwandishi na kama hana Hatia basi ataachiwa Huru tu ila kama akikutwa na Hatia basi Maamuzi ya Mahakama yaheshimiwe na apate anachostahili na siyo kuanza Kumtetea Kinafiki hapa wakati ukweli ni kwamba wengi Wetu hatujui lolote kwakuwa ndani ya Nchi zote zile huwa kuna yale tunayoyajua na yale tusiyoyajua vile vile.

Na kama kuna nchi duniani ambayo ina najisi Haki na inazionea sana nchi zingine nyingi duniani basi ni Marekani wenu hawa hawa ambao leo hii mnajifanya mnawapenda eti kwakuwa tu wamekuwa mara kwa mara wakijitokeza Kuwatetea Watu ambao Kwenu nyie mna Maslahi nao ya Kiupinzani na Kiuanaharakati na Kuzisema zile Tawala ambazo hamzipendi na mna Chuki nazo hasa kupitia Marais wao waliopo Madarakani.

Kwenye hili Sakata la Mwandishi Erick Kabendera nipo 50 / 50 nikiwa na maana kuna Upande namlaumu Yeye kama Yeye kutokana na kwamba kuna Key Principles za Investigative Journalism alizikiuka ( na Yeye anajua hilo nina uhakika ) na sehemu ambayo nailaumu Mamlaka ni pale tu ambapo nao walijichanganya mwanzoni kwa Kuanza nae na Sakata la Uraia na ghafla baadae tena hilo la Uraia wakaachana nalo wakaja na haya mengine. Kuna Udhaifu fulani waliuonyesha hapo hata hivyo pamoja na Madhaifu yao hayo bado Mamlaka hiyo haikatazwi kuendelea na hatua za Kisheria dhidi ya huyu Mwandishi wenu.
Kama sio hao mngekua bado mnaendelea kununuliwa mnadani kama nguruwe.
 
Sidhani kama Trump hata anajua kuna ubalozi wetu Marekani.

Mimi nilipokuwa kule nilikuwa napata tabu sana kuwaeleza Tanzania ikowapi, ilibidi niwe natembea na ramani, nikiwaambia mimi ni mtanzania nawaonyesha Tanzania ilipo.
Kweli mkuu?
 
Mimi ni mtu wa kijiweni kweli

Pamoja na kuwa mtu wa kijiweni na wewe wa Ofisin kama kuna kitu umenizidi basi ni ukubwa wa tumbo na tako
Nimeongelea abstract and not physical, hata hili jibu lako lina prove nilichokiongea.
 
Marekani mnachelewesha mambo jamani raia wema wanazidi kuteseka hapa Tanganyika. Mnasubir nani atekwe na kuuawa au kubambikiwa kesi zaidi ya hawa watu waliokutwa na madhara? Hebu fanyeni kitu basi kwa hawa Watekaji, wauaji, watesaji, wabambikiaji watu kesi. Hawa sio serikali ni genge la wahalifu. Raia wema tupo nyuma yenu watu wa Marekani tuna imani na ninyi.

wewe ni mpumbavu sana. Unafikiri hao mabwana zako wamerekani watafanya nini?. Erick Kabendera ni msaliti na ni lazima tumshughulikie. Ninaungana na Musiba 100% kuwapiga vita wasaliti wote wa nchi yetu
 
Mimi naamini jambo ambalo hawa jamaa hawana maslahi nalo huwa hawatii hata neno wamekufa watu kibiti,kafa akwelina,katekwa Dr Ulimboka na mengine mengi wamenyuti ila huyu jamaa wana maslahi nae kweli ukoloni hauwezi kuisha
 
Back
Top Bottom