Marekani kufanya mazungumzo na Viongozi wa Taliban

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Marekani itafanya mazungumzo rasmi na wanamgambo wa Taliban kwa mara ya kwanza, tangu Marekani ilipoondoa vikosi vyake nchini Afghanistan.

Hayo yamethibitishwa na wizara ya mambo ya nje ya Marekani mjini Washington, katika tangazo lililosema kwamba ujumbe wa nchi hiyo utakutana uso kwa uso na wawakilishi wa ngazi ya juu wa Taliban katika mji mkuu wa Qatar, Doha leo Jumamosi na kesho Jumapili.

Marekani inataka kuwahimiza watawala hao wapya wa Afghanistan kuheshimu haki za binadamu na kuruhusu mashirika ya msaada wa kiutu kuwafikia wenye mahitaji

Tangu kuchukuwa udhibiti wa nchi katikati ya mwezi Agosti, Taliban wamekuwa wakifanya kila juhudi kutambuliwa kimataifa. Marekani imesema kukutana nao haimaanishi kuuutambua utawala wao.

Chanzo: Muungwana blog
 
Hao wahuni wanaojificha nyuma ya pazia ya dini inatakiwa wapewe kibano kikali kabisa ili wajue kuishi kama wanadamu.
 
Hao ni marafiki.....
Hao ni maswahiba.....

Kwa tunaofuatilia kwa ukaribu jinsi mambo yaendavyo huko tumemaizi mengi mno.

Mathalani Marekani imewatenga marafiki zao wa zamani "NORTHEN ALLIANCE. NOTHERN FORCES" wa kule Panjshir(150 km) kaskazini mwa Kabul, hao jamaa hawajawahi kushindwa ngomeni kwao, si na Taliban ,si na Urusi(Red Army) miaka ile ya Vita ya Mujahedeen chini ya AHMED SHAH MASSOUD (baba yake huyu kiongozi wao wa sasa AHMED MASSOUD), leo hii TALIBAN wamepandisha bendera yao nyeupe huko PANJSHIR.
 
U.S haieleweki kwa kweli
Hao ni wazee wa MASLAHI YA KUDUMU.

Ukiona wamepatana na Taliban ujue kuna mambo wamekubaliana, sijajua tu ni hiyo RASLIMALI KUBWA ya DHAHABU, PLATINUM, URANIUM?! 🤣🤣

Halafu tusisahau kuwa wale Mujahedeen waliowafurusha Urusi walikuwa wote wanasaidiwa na MAREKANI (Osama, Rashid Dostum na Ahmed Shah Massoud)🤣🤣

MASWAHIBA HAO....walikosana tu pahala.....ha ha ha
 
Anaogopa ushawishi wa China kwa Afaghanstan ndomaana wanaona bora wamalizane mapema.
Hilo neno ....

Ikumbukwe kuwa baada tu ya MAREKANI kuondoka ile August 31... PAKISTAN ,CHINA NA IRAN wameamua kuwasaidia katika mambo mengi.....

China ni adui wa India(kimaslahi)....katika hilo wako pamoja na Pakistan 🤣🤣
 
Stori za vijiweni hizo. You know nothing about US foreign policy.
Kwa kuwa humu JF kumejaa uchambuzi wa kiweledi nilitegemea wewe unayejua unikosoe kwa kuweka mifano hai ya hizo sera nisizozijua mimi....laa kama unaniambia hata wewe hujui na wengine hawajui pia kwa kuwa hizo SERA ZAO ZA NJE NI SIRI zisizojulikana ulimwenguni basi nitakuelewa vyema tu.
 
Hao ni wazee wa MASLAHI YA KUDUMU....

Ukiona wamepatana na Taliban ujue kuna mambo wamekubaliana....sijajua tu ni hiyo RASLIMALI KUBWA ya DHAHABU ,PLATINUM ,URANIUM?!!! 🤣🤣

Halafu tusisahau kuwa wale Mujahedeen waliowafurusha Urusi walikuwa wote wanasaidiwa na MAREKANI(Osama ,Rashid Dostum na Ahmed Shah Massoud)🤣🤣

MASWAHIBA HAO....walikosana tu pahala.....ha ha ha
Inatia mashaka sana na tukijiuliza hawa wanapata wapi silaha na mahitaji mengineyo naona jibu ndo linapatikana kihivi
 
Inatia mashaka sana na tukijiuliza hawa wanapata wapi silaha na mahitaji mengineyo naona jibu ndo linapatikana kihivi
🤣🤣
Mkuu wangu hao tunaowaona kuwa ni "binadamu na nusu"...huwa wanaiendesha dunia kwa maisha ya "movies"....maigizo....bahati mbaya maagizo hayo hupokewa kana kwamba ni ukweli....kwani wengi wa watu duniani ni BENDERA TU FUATA UPEPO....🤣🤣
 
Kweli kabisa
Mathalani Amrullah Saleh...makamu wa Rais wa Ashraf Ghani aliyekimbilia Qatar...inasemekana yuko Tajikistan....naye ni Mtajiki Kama alivyokuwa Ahmed Shah Massoud na wengine wote wa kule kaskazini....na ndio maana sasa Tajikistan imepeleka vikosi mpakani mwa Afghanistan kupambana na hao Taliban(maswahiba wapya wa Marekani)....

Ikumbukwe kuwa baadhi ya VIONGOZI wa Taliban kama Mullah Hassan Akhund yuko mpaka katika listi ya umoja wa mataifa ya magaidi....na wengine wengi tu...🤣🤣

Ila kwa kuwa vikao vilikaliwa kule Doha....na "makubaliano ya uhakika"...Wala hutosikia kelele za ugaidi bali tu "kuitwa misimamo mikali ya Taliban" ha ha ha 🤣🤣
 
Back
Top Bottom