MAREKANI: Kifo Cha Malcom X na Kufukuzwa kwenye Chama Cha Umoja Wa Waislam (NOI)

anonymousafrica

JF-Expert Member
Aug 24, 2016
611
639
NA AnonymousAfrica #Twitreporter
Nimeandika hii, kwaajili ya kuwapatia watu picha kamili kwa lengo la kukujuza / kuelimisha / Kwa wengine ni burudani pia. Sina lengo la kuchonganisha, wala kubagua


images.jpg

Kuuliwa kwa Malcolm X
Mnamo Februari 21, 1965, Malcolm X aliuawa wakati akitoa hotuba katika ukumbi wa Audubon Ballroom huko New York City. Aliuawa mbele ya familia yake. Watazamaji wenye hasira wakamshika na kumpiga mmoja kati ya wahusika wa mauaji hayo, ambaye alikamatwa kwenye eneo la tukio. Mashuhuda wa macho waliwagundua watuhumiwa wengine wawili.ambao walikuwa wanachama wa jumuia ya kiislam (NOI), walihukumiwa kifungo cha maisha jela.

webcast_min_ishmael.jpg

Wajumbe watatu wa Taifa la Uislamu (NATIONAL OF ISLAM (NOI)) - Talmadge Hayer au Thomas Hagan (aka Mujahid Abdul Halim), Norman Butler (aka Muhammad Abdul Aziz) na Thomas Johnson (aka Khalil Islam) - walitiwa hatiani kwa mauaji yake mnamo 1966. (NATIONAL OF ISLAM (NOI)) ni asasi ya kidini na kisiasa ya wamarekani wenye asili ya Kiafrika iliyoundwa mnamo 1930 ikiwa na lengo la kuboresha hali ya kiuchumi na kiroho kwa jamii watu weusi huko Marekani. Malcolm X alijiunga na kikundi hicho mnamo 1952.

73c32aff5586026e474c7395baf3bbda--young-celebrities-malcolm-x.jpg

Malcom x alizaliwa Omaha nchini Marekani kwenye familia ya baba mchungaji na mwanaharakati wa haki za watu weusi ambaye aliishi kwa falsafa za Marcus Garvey. Baba wa Malcom alifariki kwa kinachosemekana kuwa ni ajali ya gari, lakini ilifahamika kuwa aliuawa na kikundi cha kudhibiti harakati nchini Marekani KHU KLUX KLUN. Wakati huu Malcom alikua na miaka 6. Yeye na ndugu zake waliishi maisha ya kuhama hama na ndio sababu ya elimu yake kusuasua.

malcolmx-young-malcolm-main.jpg__400x567_q85_crop_subsampling-2_upscale.jpg

( Ndoto yake alitamani kuwa mwanasheria) lakini mwalimu mzungu alimwambia WE UMESKIA WAPI KUNA MTU MWEUSI MWANASHERIA?.. akaacha na shule yenyewe akaingia mtaani kujiunga na masela. Mguu shoka mkono upanga ukipita mbele yake anakukwapua. Mwisho wa siku miaka ya 1940 aliswekwa jela kwa kosa la udokozi, uvunjaji na kuvamia majumba ya watu ili kujitaftia riziki (MTAJI WA MASIKINI NI NGUVU ZAKE MWENYEWE)

1 qVa1bUa38E7hkE8qkMgUfQ.jpeg
Akiwa jela alisilimishwa (alibadili dini) na kuwa muislam . 1952 ALITOKA JELA AKIWA KIJANA MPYA. Na kujiunga (NATIONAL OF ISLAM (NOI)) na ghafla alionekana kuwa mtu muhimu sana kwenye jumuiya ya waislam. Kwakua alikua na uwezo mkubwa wa kuongea. Falsafa ya Malcom haikua kutia vurugu bali ni kujilinda (self defense)

NI KITU GANI HASA KILISABABISHA KIFO CHAKE?

d25cbd79229aa1e661e11923037d6611.jpg
MWAKA 1964 Malcom alijitoa kwenye chama cha waislam kwakua hakuelewa nini hasa dhamira ya kiongozi wake ELIJAH MOAHMED. Kulikua na mambo kadhaa yanaendelea kwa jamii ya waislam na watu weusi nchini marekani ambayo Ellijah hakutaka yaongelewe wala kupambaniwa.

Pia, kwa nguvu ya Malcom, viongozi wa jumuiya ya kiislam walimwona ni kama ana wapiku (kama hujui Kiswahili hapa umekwisha) namaanisha kuwazidi. Kila sehemu alikua anaonekana Malcom na walimtuhumu anataka kutumuia jumuia ya waislam kwa maslahi yake binafsi (eti kujipatia nguvu kama mpambanaji) nimeamini kuna watu ni waswahili hata wazaliwe Ulaya.

tdih-feb21-HD.jpg

Kubwa zaidi ni pale Malcom X alipoongea kuhusu kifo cha John Kennedy, Ellijah alikataza mtu yeyote kwenye NOI kuongea kuhusu kifo cha John Kennedy. Wakati wa mahojiano na waandishi wa habari, Malcom alishindwa kuvumilia akajibu

Wakati nikiwa mfugaji wa kuku nyumbani kwetu, nilikua sishangai pale kuku wanaporudi zizini kulala “the chickens coming home to roost.” Yani watazurula weee ila lazma warudi tu nyumbani. Kifo cha Kennedy ni sehemu tu ya ukatili wanaofanyiwa watu weusi, waislam na nchi maskini au wale wote wasio kwenda sawa na falsafa za marekani, kwamfano Russia na Cuba. Sasa wanarudiana wenyewe kwa wenyewe. Kifo cha Kennedy ni sawa na kuvuna kile unachokipanda “you reap what you sow”. Hii speech ilivuruga ulimwengu, alipewa suspension ya siku 90 na ELLIJAH MOAHMED na ndio ikawa MAZIMA, hakurudi tena . Wengi walimwona kama msaliti wa shirika, na alipokea vitisho vingi vya kifo kutoka ndani ya kundi.

malcolmx_008_50333807_edit.jpg

Malcolm akaamua kuanzisha mashirika mawili mapya, Muslim Mosque, Inc (MMI) na the Organization of Afro-American Unity (OAAU). Kama ilivyokuwa kwa mashirika mengi ya haki za raia na wanaharakati, Malcolm alikuwa akifuatiliwa karibu na serikali , Wakiwemo FBI chini ya babu yangu EDGER HOOVER. Kweli snitch yupo kila sehem, yani hadi ndani ya misikiti kuna mtu anatumika kutoa siri za kiongozi?, tena hasa simu zake zilikua zinarekodiwa. Kwenye movie Fulani inayoitwa Godfather of Harlem , Malcom walipomwambia kuhusu kufuatiliwa kwake na jumuiya ya waislam pamoja na FBI alijibu “sina cha kuficha, waache wanifuatilie”

ca-times.brightspotcdn.com.jpg

"walimwona kama tishio," "Walifanya kazi ya kudhoofisha juhudi zake, kuunda na kuzidisha mzozo na kumjengea maadui ili kumsababishia hata kifo chake." Hapa MALCOM anawindwa na serikali na anawindwa na umoja wa waislam chini ya Ellijah Moahmed, kumbuka alishapokea vitisho mara kadhaa.

Wiki moja tu kabla ya kuuawa kwake, nyumba ya Malcolm X katika Jiji la New York iliwashwa moto wakati yeye, mkewe Betty Shabaz na watoto wao wanne walikuwa wamelala ndani. Hakuna mtu aliyewahi kushtakiwa kuhusiana na tukio hilo. Ingawa hakuna mtu aliyejeruhiwa, ikawa ni dhahiri kwa Malcolm na wale walio karibu naye kwamba alikuwa katika hatari kubwa.

07malcolmx-superJumbo.jpg
Siku ambayo Malcom aliuawa.

Kwenye mkutano wake kulikua na watu zaidi ya 400, na hakukua na ulinzi wowote wa askari.. jambo ambalo halikua la kawaida. Kumbuka Malcom alirithi tabia ya kutokusachi watu toka akiwa NOI hivyo wengi waliingia bila kizuizi. Baada tu ya kusimama stejini alipigwa risasi Nyingi sana, siwez kusema idadi kwamaana kila mtu anataja idadi yake, nimewahi kuona sehem wanasema alipigwa risasi 21.

920x920.jpg


Talmadge Hayer alipigwa risasi ya mguu na walinzi na kukamatwa wakati anajaribu kutoroka kabla ya polisi kufika. Butler na Johnson, walikamatwa wiki moja baadaye baada ya kushukiwa pia kuhusika na tukio hilo. Butler na Johnson walikuwa wanachama mashuhuri wa Harlem NOI.

New York City Police Department (NYPD) Waliripoti kifo cha Malcom kwa kusema "jumuiya ya waislam imemuua Malcom X “ "Walidhani ni mauwaji yaliyotokea kwasababu ya upinzani kati yao."

Mahakamani sasa, Hayer alikiri kuwa sehemu ya mpango wa kumuua Malcolm, lakini akashuhudia kwamba Johnson na Butler hawakuhusika, walireport New York Times Machi 1, 1966. Wakati wa kesi hiyo, Hayer hakutaja mtuhumiwa mwingine yeyote.

Hakukuwa na ushahidi wa kumuunganisha Butler au Johnson na uhalifu huo. Butler alijitetea kuwa, siku ya kifo cha Malcom alikuwa zake nyumbani anauguza kidonda cha mguuni na daktari wake alisimama kizimbani kumtetea mgonjwa wake. Hakuna wa kuficha ukweli bwana, mwisho wanaume wote watatu walipatikana na hatia mnamo 1966 nahukumiwa kifungo cha maisha jela.

Liz Mazucci, Mtafiti Mkuu wa wa historia ya Malcolm X anasema, tukio lile la kinyama halikuchunguzwa kwa umakini na polisi, walifanya kana kwamba ni ripoti ya mchezo wa dance wakati ni mauwaji ya mtu mashuhuri na tegemezi kwa wamarekani

Mnamo 1977 na 1978, Hayer aliwasilisha hati mbili zinazo endelea kusema kwamba Butler na Johnson hawakuhusika katika mauaji hayo. Hata hivyo, Hayer aliwataja wanaume wanne - wote walitoka NOI. Alidai kwa pamoja walipanga mauaji ya Malcolm X mnamo Mei 1964. Alisema alifuatwa na watu wawili kati ya wanne ambao walimwambia kwamba Malcolm X anapaswa kuuawa . Baadaye walikutana na wanaume hao wengine wawili na kujadili jinsi watakavyotenda uhalifu huo.

elijah-muhammad-9417458-1-402.jpg

"Nilikuwa na upendo na Heshima kubwa kwa Elija Moahmed," kwa heshima yake niliona hili jambo lazima nilitimize.
Siku tano baada ya kuuawa, Muhammad alikataa kuhusika na mauaji hayo, na kusema "Malcolm X alikipata kile alichokihubiri."

Utekelezaji wa sheria haukufuatilia uchunguzi wowote kwa wanaume hao na kesi hiyo haijafunguliwa tena.

Butler alitolewa mnamo 1985. Johnson aliachiliwa mnamo 1989 na akafa mnamo 2009. Hayer aliachiliwa mnamo 2010.

ALL.jpg

Kwa miaka mingi, Betty Shabaz (Mke wa Malcom X) na familia yake walituhumu Jumuiya ya Uislam na kiongozi wake, Louis Farrakhan, juu ya kupanga mauaji ya mumewe. Kumbuka Luis ni moja kati ya vijana ambao walifundishwa kazi na Malcom X. Na baadae kuitwa Luis X Kama alivyoitwa Malcom. Malcom alipojiondoa (NOI) Alimwacha Luis AKIWA KIJANA CHIPKIZI. Luis aliwahi kuandika waraka magazetini kuwa Malcom Amemkosea Elijah na wanachama wengine hivyo muda wote anamwombea afe tu. Luis Farrakhan.

rtr1mu44_copy.si.jpg

Mnamo 1995, binti ya Shabaz Qubilah alishtakiwa kwa kuajiri muuaji kumuua Farrakhan. Farrakhan alimtetea Qubilah na kujitetea kuwa hakuwahi kupanga wala kusababisha kifo cha baba yake.
 
Daaah mbona kama umeishia njiani hivi..! Stori tamu kiasi fulani. Nina maswali kadhaa ila labda ukiimalizia stori nitapata majibu
 
Muuaji Halisi ambaye alitumia Shotgun iliyothibitika kumuua Malcom X ni huyu aliyezungushiwa nyekundu, anaitwa William X Bradley au al maarufu kama Al Mustafa Shabazi, Jasusi na mwanachama mtiifu wa Nation of Islam Msikiti namba 25 wa Newark, pia inasadikiwa kuwa alikua akitumiwa na FBI.
Screenshot_20200708-175606.jpg
 
Muuaji Halisi ambaye alitumia Shotgun iliyothibitika kumuua Malcom X ni huyu aliyezungushiwa nyekundu, anaitwa William X Bradley au al maarufu kama Al Mustafa Shabazi, Jasusi na mwanachama mtiifu wa Nation of Islam Msikiti namba 25 wa Newark, pia inasadikiwa kuwa alikua akitumiwa na FBI.View attachment 1501013
Naaam huyu jamaa kuna picture anaonekana yupo mbele kabisa
nilipoipost hii story twitter niligusia hiko kitu

F giver
 
Back
Top Bottom