Leo Jumatano, serikali ya Marekani inatarajia kutangaza kuanza kutoa chanjo ya pili kwa wale waliopata chanjo ya J&J ama ya tatu kwa waliopata chanjo zingine za kukabiliana na covid 19 kwa watu wote waliopata chanjo.
Awali, wiki iliyopita, taasisi ya afya na chakula ya Marekani, FDA ilitoa kibali kwa booster vaccine kwa wale wenye umri wa miaka 60 ama zaidi ama wale wenye magonjwa na ambao kinga yao ya mwili imeshuka, kitaalam wanaitwa immunocompromised patients.
Hii imetokana na ushahidi kutoka Marekani na Israel umeonyesha kua chanjo hupoteza uwezo wake ama ufanisi baada ya miezi 6 toka mtu amechanjwa hivyo anahitaji chanjo nyingine ili kuendelea kumpa mtu kinga zaidi.
Israel wao wameanza kutoa chanjo ya booster kwa watu wote. Hii pia ni baada ya kushuhudia kuongezeka kwa wagonjwa na vifo kwa watu waliochanjwa chanzo zote. Israel ni taifa ambalo limefanikiwa sana kwenye chanjo ya awali baada ya kuchanja zaidi ya 70% ya watu wake.
Chanjo inayopoteza ufanisi baada ya miezi 6 haifai