Marekani inafanya mchezo gani barani Afrika kwa kuitaja China?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,006
1,026
Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani anayeshughulikia mambo ya Afrika Robert Godec amesema, Marekani itawaonesha watu wa Afrika kuwa, tofauti na mtindo wa maendeleo ya uchumi unaohimizwa na China barani Afrika, Marekani itaangalia zaidi maslahi ya Afrika, kitu ambacho kitaivutia zaidi Afrika. Kauli hiyo ya Godec imeashiria kuwa Marekani itazitaka nchi za Afrika kuchagua kati yake na China. Je, sera ya serikali mpya ya Marekani kuhusu Afrika itakuwa na mabadiliko gani, na nchi hiyo itacheza mchezo gani?

Kisiasa, Marekani imeitahadharisha Afrika mara kwa mara kuhusu China, na kuanzisha “vita ya kimtindo” kuhusu mageuzi ya kisiasa ya baadhi ya nchi za Afrika. Maendeleo ya uhusiano kati ya China na Afrika hayawezi kuzuiliwa, na Marekani ina wasiwasi mkubwa na kuboreshwa kwa uhusiano kati ya China na Afrika, kiasi cha kuzitahadharisha nchi za Afrika kuhusu athari za China katika mambo ya siasa na itikadi, haswa zile zilizosaini pendekezo la “Ukanda Mmoja, Njia Moja”.

Kiuchumi, Marekani inajitahidi kuhimiza mabadiliko ya taasisi na fedha ili kupunguza athari za kiuchumi za China barani Afrika. Marekani inafanya kila iwezalo kuikashifu China kwa kufanya “ukoloni mambo leo” barani Afrika, huku ikijitapa kuongeza uwezo wa Afrika wa kujitegemea badala ya kutegemea misaada ya nje, na kuonesha kuwa itachukua nafasi ya sasa ya China na kufanya vizuri zaidi kuliko China barani humo. Mwezi Machi mwaka 2020, aliyekuwa msaidizi wa waziri wa mambo ya nje wa Marekani Tibor P. Nagy alipotoa hotuba mjini Washington alisema, “tunaishutumu China kwa jinsi inavyojieleza na kuimarisha diplomasia yetu ya umma. Tunawakumbusha watu wa Afrika kuwa mchango wa Marekani ni mkubwa kiasi cha kushindwa kufikiwa na pande nyingine zote.” Ukweli ni kuwa mkakati mpya wa Marekani kwa nchi za nje ni kukabiliana na ushindani kati ya nchi kubwa, na sera yoyote inayotungwa na dola yoyote inayotoa inalenga kuhudumia mkakati wa “Marekani Kwanza”.

Kiusalama, Marekani pia inafanya mageuzi kupitia uwepo wake wa kijeshi, kuongeza misaada ya Marekani kwenye sekta ya usalama barani Afrika, na kuizuia China kushiriki kwenye shughuli za amani na usalama barani humo. Mapema mwezi Septemba mwaka 2020, aliyekuwa waziri wa ulinzi wa Marekani Mark Esper alipofanya ziara barani Afrika alisisitiza kuwa jeshi la Marekani barani Afrika lina majukumu mawili tu, mojawapo likiwa ni kushindana na China na Russia ili kupunguza athari za nchi hizo mbili barani Afrika.

Wasomi wa Afrika wanakiita kipindi cha Donald Trump kuwa rais wa Marekani kwamba ni “miaka minne iliyopotea”, lakini mkakati wa serikali ya Biden kuhusu Afrika sio “kuzika tu mali ya Trump”. Hakuna tofauti kubwa na awamu zilizopita za serikali ya Marekani, Afrika haina uzito katika mkakati wa Marekani duniani, na haitajwi sana katika sera mbalimbali za kidiplomasia zilizotangazwa mwezi mmoja baada ya rais Biden kuingia madarakani. Rais Biden alishiriki na kutoa hotuba kwa njia ya video kwenye mkutano wa kilele wa 34 wa Umoja wa Afrika, lakini hotuba hiyo haina maudhui ya kina. Vilevile, mwongozo wa muda wa mkakati wa usalama wa taifa uliotolewa mwezi Machi unalenga kubadilisha mkakati wa serikali iliyoongozwa na Donald Trump duniani, na “kukabiliana moja kwa moja na changamoto ambazo hazijashuhudiwa katika historia na kushikilia vizuri fursa adimu”, ambapo Afrika pia sio kipaumbele chake. Inatarajiwa kuwa katika kipindi cha sasa, sera ya Marekani kuhusu Afrika itaendelea kutoa kipaumbele kwa maslahi ya Marekani, na kuongeza ushawishi wake barani Afrika katika mambo ya siasa, uchumi na utamaduni kupitia njia za jadi za kidiplomasia kama vile uchumi, mapambano dhidi ya ugaidi, jeshi na msaada.

Juu ya kauli ya afisa wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Bw. Zhao Lijian amesema China na Afrika ni marafiki na wenzi wazuri wenye hatma ya pamoja, na kuendeleza ushirikiano wa kirafiki na nchi za Afrika siku zote ni sera ya kimsingi ya diplomasia ya China. Kila waziri wa mambo ya nje wa China kwa miaka 32 mfululizo ameshikilia utamaduni wa jadi wa kufanya ziara ya kwanza kila mwaka barani Afrika. Katika miaka 20 iliyopita tangu Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC lizinduliwe, thamani ya biashara kati ya China na Afrika imeongezeka mara 20 na uwekezaji wa moja kwa moja wa China barani Afrika umeongezeka mara 100.

Hivi sasa nchi nyingi za Afrika zinakabiliwa na changamoto mpya kutokana na athari mbaya ya janga la virusi vya Corona. Jamii ya kimataifa inatakiwa kutilia maanani ufuatiliaji wa nchi za Afrika, kuchukua hatua halisi, kuongeza msaada na uwekezaji ili kuzisaidia nchi kukabiliana na changmoto na kupata mendeleo. Marekani haitakiwi kuanzisha ushindani na China barani Afrika na kuilazimisha Afrika kuwa kwenye njia panda ya kuchagua upande upi, kwani hii itaharibu maslahi ya nchi za Afrika, na watu wa Afrika pia hawatakubali.

微信图片_20210430084936.jpg
 
Mchina alichokifanya Zambia na Zimbabwe acha kabisa nashangaa anapigiwa chapuo ajenge bandari bila mikataba kuwekwa hadharani hao jamaa ni wanyonyaji watatudai mpaka vijukuu vyetu watakua watumwa wao...Kama kweli huo mkataba una maslahi ya Watanzania upelekwe bungeni usomwe na ujadiliwe kwa manufaa na maslahi ya Watanzania sio kwa kutusomea vipengele kimoja kimoja tuu...
 
Mchina alichokifanya Zambia na Zimbabwe acha kabisa nashangaa anapigiwa chapuo ajenge bandari bila mikataba kuwekwa hadharani hao jamaa ni wanyonyaji watatudai mpaka vijukuu vyetu watakua watumwa wao...
@Isanga family
Katika kuhangaika na maisha , nimejikuta nafanya kazi na wachina ,jamaa ni wanyonyaji washenzi na wakatili hatari , na ni wajanja sana , hasa kwenye mikataba , na ni wezi pia, hawangaalii wanamuibia nani wao wakiona kuna namna ya kiuba wataiba tu anyhow.
Yaliyotokea zambia ilitakiwa iwe fundisho kwetu lakini viongozi wetu ni wagumu kufanya analysis.
Mchina si mtu, bora tutawaliwe na makaburu at least wamenyooka .
 
Mchina alichokifanya Zambia na Zimbabwe acha kabisa nashangaa anapigiwa chapuo ajenge bandari bila mikataba kuwekwa hadharani hao jamaa ni wanyonyaji watatudai mpaka vijukuu vyetu watakua watumwa wao...
Usisau Eritrea na Sirilanka,hii model ya mkataba walioletewa Tanzania ya kujenga Bandari Bagamoyo ndio hiyohiyo waliowapa nchi za Eritrea na Sirilanka,hiyo nchi zinalia..
Screenshot_20210430-082050.png
 
Africa has the richest concentration of natural resources such as oil, copper, diamonds, bauxite, lithium, gold, hardwood forests, and tropical fruits. It is estimated that 30% of the earth's mineral resources are found in the African continent
 
@Isanga family
Katika kuhangaika na maisha , nimejikuta nafanya kazi na wachina ,jamaa ni wanyonyaji washenzi na wakatili hatari , na ni wajanja sana , hasa kwenye mikataba , na ni wezi pia, hawangaalii wanamuibia nani wao wakiona kuna namna ya kiuba wataiba tu anyhow.
Yaliyotokea zambia ilitakiwa iwe fundisho kwetu lakini viongozi wetu ni wagumu kufanya analysis.
Mchina si mtu, bora tutawaliwe na makaburu at least wamenyooka .
Bora uendelee kutawaliwa
 
Kwani hayo mashule, majumba, mabarabara mnafanyiwa na nani kama sio China? Yeyote anachukuliwa mali na china ujue anadeni kubwa kwa tamaa za rushwa utafuni wa hela au kavunja mkataba waliouweka baina ya China na hio nchi, Marekani akiwaletea msaada wa Arv analeta masharti kuwa wanaume kwa wanaume waowane ndio atatoa msaada, kuna msaada gani mwengine anaouleta bila ya masharti badala ya vyandarua angalau mwenzake anajenga mashule, mabarabara, viwanda , badnari, majumba nk, bora huyo China
 
@Isanga family
Katika kuhangaika na maisha , nimejikuta nafanya kazi na wachina ,jamaa ni wanyonyaji washenzi na wakatili hatari , na ni wajanja sana , hasa kwenye mikataba , na ni wezi pia, hawangaalii wanamuibia nani wao wakiona kuna namna ya kiuba wataiba tu anyhow.
Yaliyotokea zambia ilitakiwa iwe fundisho kwetu lakini viongozi wetu ni wagumu kufanya analysis.
Mchina si mtu, bora tutawaliwe na makaburu at least wamenyooka .
Kutawaliwa tena! Sasa tulidai Uhuru wa kazi gani?
 
Back
Top Bottom