Marekani ina maslahi gani kwa jumuiya ya uamusho Zanzibar?

tungependa kuona ufuatiliaji ulio makini kwa vikosi vyetu waingie kazini sasa tumeona ya libya ,tumeona ya syria .tumeona ya somalia .tumeona ya nigeria ,yaishie huko huko yasifike huku ,tahadhari zote zichukuliwe wasahau kama kulikuwa na kitu kinatwa uamsho.
 
WanaJF, tukumbuke kuwa wamarekani waliwahi kumfadhili Osama kabla hajawageuka. We waache tu wakifadhili Uamsho, watakuja kulia wenyewe!!

Lkn kama wamewapa computer, basi hizo computer zitakuwa na chip zinazosafirisha habari muhimu kwenda marekani. Let us see and wait!!!
 
Nachelea kuchangia kwa hoja ya Pasco kama uthibitisho wangu.

Kwa misingi yo yote ile ni wazi nchi hizo 3 tajwa wanalijua ombwe la uongozi tulilo nalo. Kifupi wanajitokeza kusaidia maslahi yao. Serikali yetu kwa mantiki hiyo (Rais wetu haachi kwenda kutoa taarifa ya utendaji wake USA) ni kibaraka wa nchi hizi.

Hizi vurugu zinatisha lakini zina mizizi ndani ya viongozi wetu. Nijipambanue kuwa naunga mkono vurugu hizi kwa maslahi ya muda mrefu ya ukombozi wetu. Mimi naona hasara na hofu ni "collateral damage" kwenye uwanja wa mapambano dhidi ya ukandamizaji wa dola na mabwana zao.

Mkakati wa dola si ule wa kizalendo na sustanability ya amani kwa manufaa ya maendeleo yetu. Ndivyo wanavyoshauriwa na hutasikia hata siku moja wakikemewa na mabwana hawa kwa tafrani inayosababishwa dola.

Binafsi maelezo yo yote yale ya watawala yananikifu, naunga mkono mikakati, mbinu yo yote inayotumika katika harakati hizo za kujikomboa. NI sababu naamini kuna fursa ya ukombozi dhidi ya watawala na mabwana zao haiji bila shinikizo. Kuhusu damages, zipo, zinaumiza lakini angalau watawala wanatiwa akili kuwa hali si shwari kama wanavyojifariji.
 
Mkumbuke hao Waheshimiwa Ndio wanaochangia kukamilisha Bajeti yetu, hilo pekee inawaruhusu kutia Pua popote pela. Tunaloooooooooooooo?
 
Nchi za ulaya ikiwemo uingereza ziliisha acha kabisa imani za dini, kuna watu wanaitwa liberals au democrats au leftist hawataki kusikia chochote kuhusu ukristo. Vita yao juu ya dini ya kikristo vilianza kwenye ile karne ya French revolution walipotangaza kuwa binadamu hamhitaji Mungu maishani mwake na kwamba watu ni matokeo ya evolution ya manyani na siyo kuumbwa na Mungu. Wahuni kama charles darwin wakaja na nadharia zao, sasa matokeo ya huo uhuni ni kuuangamiza ukristo ulaya. Hata hivyo hawakuelewa kuwa kanisa limesimikwa juu ya mwamba na halitashindwa na chochote hata milango ya kuzimu. Baada ya kushindwa kuuangamiza ukristo ulaya liberals wameungana na waislam ili kupata nguvu zaidi dhidi ya ukristo, wamewaruhusu waislam wakimbilie nchi za magharibi wanapewa kila kitu bure wanapewa baadhi ya makanisa na kuyageuza misikiti. Hali ni hivyo hivyo marekani pia ingawaje huko ukristo bado unanguvu kubwa licha ya liberals kuweka raisi ambaye ni mwislam wa siri, sasa naona hawa liberals wanaanza kuelekeza mashambulio yao nje ya mataifa yao, usitgemee hata siku moja wakemee vitendo na hujuma zozote dhidi ya ukristo unless wawe waathirika wao wenyewe. Machozi ya vilio vya wakristo kwenye nchi za kiislam Iran misri Sudan Nigeria Somalia Pakistan Saudi arabia nk hakuna anaejali. Roho ya mpinga kristo iliyo ndani ya Uislam ndo hiyo hiyo iliyo ndani ya liberals. Nyumba ikijipinga yenyewe kwa yenyewe haiwezi kusimama, shetani ni mjanja na ana maarifa
 
Tanzania ni strategic, politically ,geographically, and culturally kwa uchumi wa dunia.Wasomali wa kenya ni hatari sana kwa uimara wa kenya.Biashara kwa meli za South east china na middle east imekuwa ghali sana.Pirate wanapandisha bei ya vitu, kutokana na bima kuwa kubwa kwa meli zinazopita ukanda huu+kulipia ulinzi.Tanzania pamoja na kuwa na madini pia inafungua njia kwenda afica ya kati na kusini Congo, na Zambia ktk shaba ambayo inashindaniwa na China na nchi nyingine, electronic industry imepandisha bei ya shaba mara dufu.tazama bei ya wire za uememe.

zanzibar ni doa kwani ikijitenga halafu wakijiuza pasipo busara na kuwa watumwa for forever, bahari ya Tz itakuwa ndogo na si salama na njia za meli hazitokuwepo tena zaidi ya kuzunguka dunia kupitia route ndefu na ndege.africa itakuwa mzigo zaidi ,ktk uchumi duni.

Kwa Taarifa iliyopo africa kuna soko kubwa sana ktk sekta za usafiri, consumer products, research, ICT and other emerging technologies.muulize mchina kuhus Toyo, na feki nyingine kabla hazijawa original, waulize Voda na Airtel kuhusu Mobile ,money, hakuna haja ya ku run wire tena.
 
Marekani inasemekana kwa kiasi kikubwa kuifadhili jumuiya ya uamusho ya Zanzibar kwa kuipatia fedha na samani za ofisi. Hii ilijidhihirisha wazi kwa ubalozi wa nchi hiyo ikiwa ni pamoja na balozi za Uingereza na Norway kushiriki katika mazungumzo yaliyofanyika hivi karibuni baina n=ya waziri wa mambo ya ndani Dr. Nchimbi, IGP Mwema na viongozi wa kiislamu Zanzibar.

Je nchi hizi tatu zina maslahi gani na jumuiya ya uamusho?
katika hicho kikao Uamsho haikushirikishwa,walikuwepo katika kikao hicho ni jumuiya nyengine za kislamu, wacha pumbaaaaa
 
Habari za kuaminika kutoka ndani ya uamusho ni kuwa baadhi ya computers zinazotimika katika ofisi yao zimetolewa na ubalozi wa Marekani.

Aidha leo asubuhi katika Star TV mwandishi maarufu wa makala Bw. Jabir amethibitisha hilo!
Good...so US sasa wana info za kutosha kuhusu hawa jamaa...km walijisahau imekula kwao.Na interest ya Huyu balozi inaonyesha kuna serious isse with latest development.serikali itawajibishwa, akina shein watajituma, na kam nao walikuwa wakijumuika ktk mikutano wakijdai wanaachia growth of democracy and debating.Imekula kwao.
 
Na Mwinyi Sadallah
2nd June 2012
Kiongozi wa Jamhuri ya Maimamu Zanzibar na Msemaji Mkuu wa Jumuiya ya Uamsho na mihadhara ya Kiislamu (JUMIKI), Sheikh Amir Ahmed akizungumza na waandishi wa habari, kwa mara ya kwanza tangu kutokea vurugu Zanzibar, katika msikiti wa Mchangani mjini Zanzibar janaWakati mali za mamilioni ya fedha zikiwa zimeharibiwa kufuatia vurugu zilizotokea Zanzibar, Kiongozi wa Kamati ya Muungano wa jumuiya za Kiislamu Zanzibar, Sheikh Farid Hadi Ahmed amesema wamefanikiwa kupata orodha ya watu waliofanya hujuma ya kuchoma makanisa moto na kuahidi kuifikisha katika vyombo vya dola kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.
Vurugu hizo zilizodumu kwa siku tatu, zilianza Mei 26, zimesababisha hasara kubwa ikiwemo uharibifu wa nyumba za Ibada, uporaji wa mali za watu, na wafanyabiashara katika soko kuu Darajani na Mwanakwerekwe kushindwa kufanya kazi kwa siku tatu mfululizo.
Miongoni mwa athari nyingine ni kuchomwa moto kwa magari likiwemo la Askofu wa Tanzania Assemblies of God (TAG), lenye namba za usajili Z 694 AX, uharibifu wa miundombinu ya barabara, uchomaji wa matairi ya magari na upangaji wa mawe katikati ya barabara.
Padri wa kanisa la Mtakatifu Mikaeli, Ambrose Mkenda, ambalo limechomwa moto alisema kwamba tukio hilo, limesababisha hasara kubwa kutokana na mabenchi yote yanayotumiwa na waumini katika ibada kuchomwa moto pamoja na mali mbalimbali zilizokuwemo ndani ya kanisa vikiwemo vinanda viwili navyo vilitekea kwa moto huo.
"Hasara kubwa karibu milioni 20 kwa vile mali zote zilizokuwemo kanisani zimeungua moto na walinzi wetu walikimbia baada ya kuvamiwa na watu waliokuwa na silaha kali," alisema Padri huyo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Fresh Enterprises Catherine Peter alisema kwamba wamepata hasara inayofikia kiasi cha sh milioni 200, kufuatia watu waliovamia baa ya daraja bovu, na kung'oa madirisha, mabati, milango, vyoo vya masinki na kupora vinywaji vya aina mbalimbali zikiwemo bia na pombe kali mbali na fedha taslimu za mauzo.
Alisema kwamba uharibifu huo wa mali ulifanywa na watu waliokuwa na silaha za kijadi, na kutaka Serikali kuangalia uwezekano wa kufidia hasara walizozipata.
"Wakati Serikali inahamasisha wananchi wake wajiajiri kama wajasiriamali, leo wanatokea watu, wanaharibu mali ya mtu wakati tunafanya biashara halali tukiwa na leseni na kufuata taratibu zote za ulipaji wa kodi, hati ya Muungano iko kwa Rais Jakaya Kikwete, Rais Dk.Ali Mohamed Shein na Umoja wa Mataifa, lakini haipo katika baa", alisema Catherine.
Makundi mengine yaliathirika na vurugu hizo ni wafanyabiashara katika soko la Mikunguni, Darajani,
Mwanakwerekwe,wamachinga ambao wamesema walishindwa kufanya kazi na kuitaka Serikali itoe elimu ya kutosha juu ya athari zinazotokana na vitendo vya vurugu.
Kwa upande wa Nishati ya Mafuta, taarifa kutoka kwa baadhi ya makampuni ikiwemo United Petroleum, wamesema vurugu hizo zilisababisha mauzo yao kushuka kwa asilimia 25, katika kipindi cha siku tatu za vurugu.
Taarifa kutoka kitengo cha hesabu ndani ya kampuni hiyo iliyotolewa na Hady Bensulmah, alisema wateja wao wakubwa ni makampuni ya utembezaji wa watalii, mahoteli ya kitalii ambao hawakuweza kununua mafuta katika kipindi chote cha vurugu hizo mbali na wananchi wa kawaida.
Akizungumza na waandishi wa habari, Amiri mkuu wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar na Msemaji wa Muungano wa Jumuiya za Dini ya kiislamu Zanzibar, Sheikh Farid Hadi Ahmed alisema kwamba wamefanikiwa kupata orodha ya watu waliohujumu makanisa Zanzibar na wataifikisha katika vyombo vya dola ili wachukuliwe hatua za kisheria.
Alisema kwamba Jumuiya ya Uamsho haihusiki na hujuma zilizotokea na uporaji wa mali, kwa vile mafundisho ya dini ya
Kiislamu yanakataza vitendo vya vurugu na wamesikitishwa sana na kulaani vitendo vyote vya uchomaji moto wa makanisa.
Alisema kwamba wataendelea kudai haki yao, ya kuitaka Serikali ianzishe mchakato wa kura ya maoni, ili Wazanzibari waulizwe kama wanautaka Muungano au hawautaki, hadi hapo lengo lao litakapofanikiwa.
CHANZO: NIPASHE
 
katika hicho kikao Uamsho haikushirikishwa,walikuwepo katika kikao hicho ni jumuiya nyengine za kislamu, wacha pumbaaaaa

Hakuna mahali nimeonyesha kuwa Uamsho walishiriki katika kikao hicho! Acha jazba!
 
Inasemekana Marekani na Uingereza ndio walioshinikiza Tanganyika na Zanzibar kuungana kwa maslahi yao enzi zile za vita baridi. Sasa huenda wana ajenda nyingine mpya inayowalazimisha kuuvunja muungano wetu. Binafsi huu muungano sujawahi kuuelewa wala sioni faida yake hasa kwa kuwa viongozi hawataki kuuboresha
 
Marekani inasemekana kwa kiasi kikubwa kuifadhili jumuiya ya uamusho ya Zanzibar kwa kuipatia fedha na samani za ofisi. Hii ilijidhihirisha wazi kwa ubalozi wa nchi hiyo ikiwa ni pamoja na balozi za Uingereza na Norway kushiriki katika mazungumzo yaliyofanyika hivi karibuni baina n=ya waziri wa mambo ya ndani Dr. Nchimbi, IGP Mwema na viongozi wa kiislamu Zanzibar.

Je nchi hizi tatu zina maslahi gani na jumuiya ya uamusho?

mie nakwambia hizi nchi za magharibi kwa ujumla wao ni wash. popote penye utajiri na watu wenye msimamo watachochea vagi kusudi waendelee kuvuna. Na wanatumia udhaifu wetu kuleta hizo vagi. Angalia walivyoifanya Congo ya lumumba shauri ya shaba na almasi, Rwanda gonganisha na Congo, kwa Gadaffi (RIP), kwa Sadam etc.

Utajiri wa hapa umewapa wasiwasi kutokana na maendeleo ya Bunge letu kuendelea kuwa madhubuti na kuhoji mambo kadhaa. Watawatumia watu na wakishindwa ni kuua viongozi waliongagari. watawasaidia warabu warudi zenji lakini waarabu hawatafaidi matunda badala yake wata take over. Kwa bara watatafuta janga lakuwawezesha kuvuna utajiri wake.
Hawa ni wash. Walituambia samaki wetu production yake ni duni kiasi kwamba per capita protein intake yetu iko chini. Ili kuiongeza tupande Sangara lake Victoria - vichwa vyetu vikakubali - matokeo tukabaki na maPANKI na minofu hiyooooo ulaya - MBOJO wetu mtamu katoweka tumebaki na mipanki ya Sangara.

walikuwa na kiherehere cha nini - tumewaambia tumeshindwa!!!
 
Habari za kuaminika kutoka ndani ya uamusho ni kuwa baadhi ya computers zinazotimika katika ofisi yao zimetolewa na ubalozi wa Marekani.

Aidha leo asubuhi katika Star TV mwandishi maarufu wa makala Bw. Jabir amethibitisha hilo!

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Seneta wa Marekani Christopher Coons,akiwa na Ujumbe aliofuatana nao walipofika Ikulu Mjini Zanzibar jana


DSC_0050.jpg
 
iko kitu imejificha nyuma ya pazia naomba ufafanuzi hiki kikundi SMZ inakitambua uwepo wake .je ikawaje wapewe computer na wakatulia kuna mkataba gani wa siri na hiki kikundi na je ni nani wapo kwenye hiki kikundi ,wako wangapi,wana lengo gani na tanzania tuitakayo ,.tumeona vikundi kama hivi vikiibuka kama boko haram na jinsi vinavyosumbua ,wahusika wakiangalie hiki kikundi na shughuli zake zieleweke kama wapo kwenye category ya NGO WAJISAJILI .kama ni chama cha siasa kifuate taratibu zake kwa msajili wa vyama .pia uamsho wanamuamsha nani ,na kwanini iwe ni wakati huu .huko nyuma walikuwa wapi wamelala .hakuna kuwaza sana angalia boko haram walianzaje wana tofauti gani na hawa uamsho ambao sijui wanamuasha nani na nani kawatuma kwa madhumuni yapi .

Teh teh ..... Labda walidanganywa kuwa zimeletwa ajili ya NGO watumie kufundishia wale watoto wanaorandaranda beach kuokota mazailia ya bahari na kulima mwani na mama zao. Sasa jamaa wakaambiana nyuma ya mgongo ,wasiwaachie computers bomba hivyo makafiri wazitumie kupotosha utamaduni wa zenj(???***??), wazibadilli na watumie kwa uamso ili kunajisi plan za makafir zaidi....Na pia ni haki muumini kupokea na kutunzwa na kafir so kupokea inweza kuwa sunna, au Jizzya.

Unawaamini wamarekani?Irani aliokota ndege ilitowekewa dummy sofwtare inayokuruhusu kui hack baadhi ya functions.Wkadhnai wameishusha kumbe jamaa wamezuga ili waipeleke ndani secrete sites,kui reverse engineering wakiwa na furaha kuwa Asiye na Mshirika(Lonely) kawabariki.Kumbe kidege kiechukua ushushu wa kutosha, kimepeleka computer viruses , sasa hivi jamaa mitambo inaliwa na computer virus wengine wabaya kuliko hata mitambo ingepigwa Bomu kadhaa.

Nawapatia huruma na siasa zao za msimu, za kutaka umaarufu, kutukuzana za kuiga na kubuuzwa kwani wanakula na kulala kwa wanyempiga vita.

NANI HAJUI SERA YAO NI MISAADA NA+MISAADA NI YAO TUU KUNGURU WA BARA WASIJEZENGEA.BAHATI MBAYA KUNGURU WABAYA NI WA ZENJ
 
Back
Top Bottom