Marekani imetangaza kuwa haitahusika katika Mpango wa Ulimwengu unaolenga kutengeneza, kutoa na kusambaza chanjo dhidi ya COVID-19

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,800
4,460
Kulingana na habari katika gazeti la "Washington Post", Msemaji wa White House Judd Deere amesema kuwa Marekani haitashiriki katika Mpango wa Chanjo dhidi ya Covid-19 (Covax), ambao unaratibiwa na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO).

Akisisitiza kuwa Marekani itafanya suala la chanjo peke yake, Deere, amesema

"Marekani itaendelea kushirikiana na washirika wake wa kimataifa kuvishinda virusi, lakini haitajishirikisha na mashirika ya kimataifa chini ya ushawishi wa Shirika la Afya Duniani na Uchina."

Utawala wa Donald Trump umetangaza mnamo Mei 29 kwamba umemaliza uhusiano wake na WHO kwa madai kwamba "Shirika hilo lilifanya maamuzi yaliyoathiriwa na China katika kupambana kwake na janga hilo".

Mikutano inafanywa na zaidi ya nchi 170 zilizo chini ya mpango wa Covax, ambao unakusudia kuharakisha juhudi za kutengeneza chanjo ulimwenguni, kuwezesha nchi zote kufaidika na chanjo na kuwafanya watu walio katika hatari kubwa wanufaike na chanjo wakiwa wa kwanza.

Mashirika mengi na nchi nyingi zikiwemo nchi washirika wa Marekani kama Ujerumani na Japan, wameunga mkono mpango huo.
 
Dduuhh!! Kwa hiyo washirika wa USA wameamua kumuacha USA awe ana bweka bweka tu wala hawamuungi mkono !?

Daahh kweli USA ipo ICU
 
Back
Top Bottom