Hey guys mimi naona si vizuri kumtumia Nyerere kisiasa. Ni vizuri kumuongelea kwa mazuri lakini kwenda kwenye kaburi lake na kutumia kijiji chake kuweka mipango ya kuwadanganya watanzania kuhusu ufisadi si vizuri. Kitu kingine cha kuangalia ni kwamba CUF na CHADEMA wakitaka kufanya kama CCM je wataruhusiwa? Huu ni wakati wa CCM kubadilika na kuacha kuogopana na kutishia walarushwa laana za Nyerere. Wala rushwa wanatakiwa kufungwa. Vilevile CCM wanatakiwa kuelewa kwamba Watanzania wanabadilika na itakuwa vigumu sana kwa sasa kuficha siri za rushwa kwani dunia imekuwa ndogo sana karne hii. Mimi naomba tuache kumtumia Nyerere kwa siasa, na nimesikitishwa na hatua ya CCM kumtumia mtu aliyefariki.