WanaJF nichukue fursa hii kuwataarifu kuwa Marehemu Ally Zona amezikwa jioni hii katika kijiji cha Semngano kilichopo katika Kata ya Kilulu Wilayani Muheza Mkoani Tanga. Msiba uko Tanga Mjini. Mwili wa Marehemu baada ya kuswaliwa ulisafirishwa kuelekea Muheza kwa Mazishi.
Viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Tanga Mjini walishiriki msibani hapo na baadaye Viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Muheza wakiongozwa na Katibu wao Bw. Martini Kifua na Katibu Mwenezi Bw. Rajab Mhina walishiriki katika Mazishi na kukabidhi Mchango wao wa Rambirambi kwa Baba Mkubwa wa Marehemu. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI AMENI.
Viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Tanga Mjini walishiriki msibani hapo na baadaye Viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Muheza wakiongozwa na Katibu wao Bw. Martini Kifua na Katibu Mwenezi Bw. Rajab Mhina walishiriki katika Mazishi na kukabidhi Mchango wao wa Rambirambi kwa Baba Mkubwa wa Marehemu. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI AMENI.