Marefa wa Tanzania na Wasaidizi wenu mpaka siku mkifa kwa kupigwa vibaya Viwanjani ndiyo mtajua kuchezesha Soka kwa Haki na siyo Chuki na Maagizo

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,471
108,599
Hivi sheria gani ya Soka ambayo FIFA pia wanaitambua isemayo Kona ikiwa inapigwa huku Mabeki Wawili wakiwa katika Milingoti halafu Mchezaji wa Timu Pinzani akatokea mbali na Kuruka hadi Kufunga zuri ni Kuotea?

TFF, Bodi ya Ligi na Chama cha Waamuzi nchini Tanzania endeleeni tu Kuulea huu Upuuzi kama uliotokea jana pale Gwambina Stadium ila nawaambieni kuna Siku mtakuja Kuokota Maiti za Marefarii na Washika Vibendera Viwanjani ndipo Akili zenu zitawakaa sawa.

Nitashangaa kama ndani ya Saa kati ya 24 hadi Saa 72 sijasikia Yule Mwamuzi na Mshika Kibendera Mfupi kama Kiberiti wa Mechi ya Jana ya Gwambina FC na Simba SC pale Misungwi Mkoani Mwanza hawajafungiwa Kuchezesha Ligi Kuu kwani huenda Jana matokeo yangekuwa mengine Amani Uwanjani ingetoweka na hata Damu pia Kumwagika kwa Fujo Kubwa ambayo ingetokea.

Kuna Vitu vinakera na havivumiliki tena.
 
Ingependeza zaidi kama ungeweka ukweli wa tukio kuliko kukanusha tu kuwa mleta post anadanganya,ungetudaidia na sisi wengine ambao hatujaujua huo ukweli.
Ukweli wa tukio ni kwamba line 1 hakukataa goli, narudia hakukataa goli bali mara tu Chama alipopiga kona yeye alinyoonya kibendera kuashiria goal kick akimaanisha mpira ulitoka nje mara tu ulipopigwa na Chama na ukapiga kona kurudi ndani ya uwanja. Marudio ya picha yameonesha mshika kibendera hakuwa sahihi maana mpira haukutoka nje.
 
Usiwe mfuata mkumbo. Angalia ule mpira wakati chama anaupiga ulikuwa kwenye right angle ya kona? We angalia vizuri
Oya hebu acha ushabiki maandazi mkuu, pale kuna tatizo gani? Hebu tizama hii video.


1. Mpira umetengwa katika right spot nae line 2 yupo hapo hapo anaona.
2. Ule mpira haujatoka nje ya uwanja kwa maana ya kuvuka goal line.
3. Aliefunga hakuwa ameotea wakati kona inapigwa.
4. Hakuna mchezaji wa Gwambina aliefanyiwa rafu wakati wa tukio la ufungaji goli.


Hebu tueleze hapa bwana mtaalamu pale ni kigezo gani kimetumika kukataa goli lile.
 

Attachments

  • 2752180-5f0a30f72ee5b8c358e8ac49a36a1cf8.mp4
    2.4 MB
We pimbi ule mpira umetengwa out of its position.
Una taaluma yoyote ya masuala ya uamuzi? Je mpira umeanza kuufuatilia lini?

Je unajua kama hiyo ingekuwa ndio sababu, kwakuwa linesman alikuwa hapo hapo alitakiwa kumzuia Chama asipige ile kona mpaka ajiridhishe kuwa huo mpira upo katika spot sahihi?

Hivi nyie utopolo akili hamna au? Ndio ujinga kuanzia mashabiki mmeambukiza mpaka team nzima.

Inasikitisha sana kuona mtu kama wewe kwenye jukwaa letu la Sports.
 
Usiwe mfuata mkumbo. Angalia ule mpira wakati chama anaupiga ulikuwa kwenye right angle ya kona? We angalia vizuri
Wewe zwazwa kweli, kama ule mpira haukuwa sehemu sahihi ungerudishwa kupigwa kona tena, na sio kuweka goal kick. Goal kick maana yake mpira ulikuwa umetoka nje ya uwanja upande wa goal line kabla ya mfungaji kuuweka kambani, kitu ambacho hakijatokea.
 
Azam Tv nao chenga tu yaani hawawezi kuonyesha kama mpira ulitoka ukiwa hewani au la. Inawezakana mwamuzi alikuwa sahihi ila bila msaada clear wa video tutabaki kumlaumu tu.
 
Sasa pale ilitakiwa iweje, toa ufafanuzi, je kwanini isingerudiwa kona?, kwanini linesman hakumwambia chama aweke vizuri mpira? Toa excuses za kimpira na sio kishabiki bro!! Lile ni goal halali kabsa with no excuses
Usiwe mfuata mkumbo. Angalia ule mpira wakati chama anaupiga ulikuwa kwenye right angle ya kona? We angalia vizuri
 
Usiwe mfuata mkumbo. Angalia ule mpira wakati chama anaupiga ulikuwa kwenye right angle ya kona? We angalia vizuri
Ingelikuwa ivyo kona ingerudiwa mkuu au kutopigwa mpaka arudishe mahala sahihi

Anachodai line 1 ni kuwa mpira ulizunguka nje kabla ya kurejea ndani, kitu ambacho kwa mujibu wa marudio ya video mpira haukuwa umetoka.
 
Back
Top Bottom