Marando na watuhumiwa wa ufisadi

2015

Senior Member
Aug 13, 2011
123
40
Wana JF

Kwanza na-declare interest mm ni mfuasi na mwanachama wa CHADEMA, Hili swala la Marando kuwa wakili wa baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi km vile manji na mahalu litakuja kuwa na madhara makubwa sana hapo badae ktk harakati za chama za kuchua dola natambua kabisa ile ni professional yake na ni vigumu aache kazi aliyoisomea kwa muda mrefu, lakini kabla ya kuchua kazi lazima mtu ufanya client assessment.

Kwa kuwa ameamua kuwa ktk siasa na kufanikiwa kuwa mjumbe wa cc ya cdm ni wakati wake muafaka wa kuhakikisha kimoja kati ya professional yake na siasa hakuna kinacholeta madhara kwa kingine. Kwa hiyo moja ya criteria ya kutumika kwake kum-accept client iwe ni asiwe mtuhumiwa wa ufisadi. Nionavyo mm professional yake kwa sasa inaleta madhara ktk siasa si kwake tu bali kwa Chadema kwa ujumla coz ni vigumu sana mtu kupinga ufisadi majukwaani na kuukubali mahakamani na watu wote wakaamua kukuamini ww ni mpiganaji wa kweli wa ufisadi.

Swala kubwa la sisi wana-chadema tunalotakiwa kulielewa ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi hawawezi kutofautisha professional na siasa kiasi kwamba point tutakayoitumia kuuelezea uma ya kuwa hii ni siasa na hii ni professional haitaweza kuzaa matunda yeyote. Marando na uongozi wa juu ulitazame hili kwa mapana na marefu ili nguvu iliyokwisha tumika kukifikisha chama hapa isije kupotea kirahisi kisa mtu mmoja ambae ana uwezo wa kuchua kesi zingine na kuendelea na maisha.

Tujiulize swali dogo kwa mfano leo ROSTAM amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za wizi wa KAGODA na marando akafanya km anavyofanya kwa wale wa EPA itakuwa sahihi? Au kuwatetea wa EPA itakuwa halali na kumtetea Rostam itakuwa haramu wakati wote ni mafisadi?

Nawasilisha
 
wewe jamaa .... hivi ukiwa kama daktari halafu mwizi akaletwa hospitalini ameumizwa vibaya je hautamtibu kwasababu ni mwizi ?

Nakubaliana na kufahamu unachokisema lakini ni asilimia ngapi ya watz watakaokuwa wanafikiria hivi? kwa uchunguzi mdogo wa kuhoji baadhi ya wananchi hili swala linawakera lakini hawana cha kufanya ndo maana nikaona the best solution ni yeye kuachana na kesi hizi na ajikite ktk kesi zingine
 
Hata mm nimekuwa najiuliza maswali mengi sana kuhusu huyu bw. Marando. Anachukua majukumu ya kuwatetea mafisadi mahakamani lakini anakwenda kuwasema majukwaani. Yaani hii inawachanganya sana watu ambao tayari walishaanza kujenga imani na CHADEMA. Kama Dr. Slaa kwa bahati atapita hapa atolee ufafanuzi suala hili akiwa kama Katibu mkuu wa chama.
 
Mleta mada hajui anachosema kabisaaa kwani akiwa mwanasheria si ni kazi yake kutetea watu au umehujui kazi yake pole badilisha mada kwani umechemka.
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Mimi naamini serikali inapaswa si tu kupeleka watu mahakamani, wapeleke watuhumiwa sahihi kwa makosa sahihi. Na hicho hakifanyiki hivi sasa, haingii akilini kuona hukumu za watu waliochukua bil 2, huku "wamiliki" wa kampuni iliyochota bil 40 wakiwa hawajulikani.

Kuna watu watapewa misalaba isiyokuwa ya kwao. Kama wana makosa kweli, serikali ipeleke ushahidi utakaokuwa scrutinized na watu kama Marando, tupate wakosaji wa ukweli, sio waigizaji.
 
wewe jamaa .... hivi ukiwa kama daktari hala<span style="font-family: &amp;quot">f</span>u mwizi akaletwa hospitalini ameumizwa vibaya je hautamtibu kwasababu ni mwizi ?
<br />
<br />
safi sana ulivyomfafanulia.
 
marando for ccccm hukujua hilo wakili wa serikali,,,,,more to come out.........
 
wewe jamaa .... hivi ukiwa kama daktari halau mwizi akaletwa hospitalini ameumizwa vibaya je hautamtibu kwasababu ni mwizi ?
Unaleta mifano ya Kindergarten kwa Great Thinkers
 
wewe jamaa .... hivi ukiwa kama daktari halafu mwizi akaletwa hospitalini ameumizwa vibaya je hautamtibu kwasababu ni mwizi ?
hapa ndo ninapokuwa na doubt na uelewa wa wanaJF wengi. hivi kutibu mtu ndo kumtetea na kuhalalisha wizi wake? Marando anawatetea. hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. nashangaa wengi wanaokusifu kwa utumbo wako huu. Mleta mada unamantik. marando is threat to chadema than any. even shibuda is less. mark my words.
 
hapa ndo ninapokuwa na doubt na uelewa wa wanaJF wengi. hivi kutibu mtu ndo kumtetea na kuhalalisha wizi wake? Marando anawatetea. hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. nashangaa wengi wanaokusifu kwa utumbo wako huu. Mleta mada unamantik. marando is threat to chadema than any. even shibuda is less. mark my words.

kwa uelewa wako ni vigumu sana kuweza kutambua professionalism and its ethical codes of conduct ...... kazi ya wakili ni kumtetea mhalifu na sio kuhukumu yupi ni mhalifu na yupi si mhalifu .... kwani hii kazi ya wakili ni kutetea watu wasio na makosa? ... silly mind ! .... as well daktari jukumu lake ni kutoa tiba kwa mgonjwa pasipo kuangalia ameathirika vipi na ugonjwa wake .... your thinking capacity is very low

hata wewe ukifanya uhalifu sasa hivi ... katiba inasema you have the right for an attorney (legal representative ) na serikali pia ina jukumu la kugharamia wakili wa kukutetea

kwa hiyo chadema na uongozi wote haioni hili na kukemea ni wewe tu mwenye narrow mind unaeona ?

try to be analytical ....
 
Unaleta mifano ya Kindergarten kwa Great Thinkers

hutakaa ukaweza kuconnect huo ufafanuzi mpaka siku yako ya kufa ..... hata hujaelewa nini kinazungumziwa hapa ..... this is a white wash to your deducted brain ...... unachujua ni chuki dhidi ya dini na makabila .....

WHY DO YOU PREACH HATE ?
Because you are a failure isn't it?
 
Wana JF
Kwanza na-declare interest mm ni mfuasi na mwanachama wa CHADEMA, Hili swala la Marando kuwa wakili wa baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi km vile manji na mahalu litakuja kuwa na madhara makubwa sana hapo badae ktk harakati za chama za kuchua dola
Natambua kabisa ile ni professional yake na ni vigumu aache kazi aliyoisomea kwa muda mrefu, lakini kabla ya kuchua kazi lazima mtu ufanya client assessment, Kwa kuwa ameamua kuwa ktk siasa na kufanikiwa kuwa mjumbe wa cc ya cdm ni wakati wake muafaka wa kuhakikisha kimoja kati ya professional yake na siasa hakuna kinacholeta madhara kwa kingine. Kwa hiyo moja ya criteria ya kutumika kwake kum-accept client iwe ni asiwe mtuhumiwa wa ufisadi
Nionavyo mm professional yake kwa sasa inaleta madhara ktk siasa si kwake tu bali kwa Chadema kwa ujumla coz ni vigumu sana mtu kupinga ufisadi majukwaani na kuukubali mahakamani na watu wote wakaamua kukuamini ww ni mpiganaji wa kweli wa ufisadi.
Swala kubwa la sisi wana-chadema tunalotakiwa kulielewa ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi hawawezi kutofautisha professional na siasa kiasi kwamba point tutakayoitumia kuuelezea uma ya kuwa hii ni siasa na hii ni professional haitaweza kuzaa matunda yeyote.
Marando na uongozi wa juu ulitazame hili kwa mapana na marefu ili nguvu iliyokwisha tumika kukifikisha chama hapa isije kupotea kirahisi kisa mtu mmoja ambae ana uwezo wa kuchua kesi zingine na kuendelea na maisha. Tujiulize swali dogo kwa mfano leo ROSTAM amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za wizi wa KAGODA na marando akafanya km anavyofanya kwa wale wa EPA itakuwa sahihi? Au kuwatetea wa EPA itakuwa halali na kumtetea Rostam itakuwa haramu wakati wote ni mafisadi?

Nawasilisha
ndio mtakapojua kuwa hakuna upinzani tanzania wote wako kwa ajili ya kutaka kula tuuuu na hawana jipya eti watasaidia watu hakuna ppo wala nini nguvu...
 
hapa ndo ninapokuwa na doubt na uelewa wa wanaJF wengi. hivi kutibu mtu ndo kumtetea na kuhalalisha wizi wake? Marando anawatetea. hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. nashangaa wengi wanaokusifu kwa utumbo wako huu. Mleta mada unamantik. marando is threat to chadema than any. even shibuda is less. mark my words.
Comrade Ngwendu, ni kweli kabisa hawa Pro-CDM-JF,uelewa wao ni mdogo sana kama huo mfano wa mgonjwa na Wakili.
Tatizo hawataki kujifunza na kukubali mawazo kutoka kwa watu wengine wao ni CDM tu mpaka imewapa upofu na akili zimedumaa kabisa tena zimefunikwa na blanketi jeusi,
hawa Pro-CDM-JF ni pumba sana mpaka wanatia huruma
 
Role ya Marando ni kubwa sana hasa upande wa kotini kwa maslahi ya wapinzani wote nchini. Siku zote amekuwa akisema hakubaliani na aina ya watu wanaoletwa kotini kwa tuhuma za ufisadi kwakuwa ni dagaa tu, mapapa hayaletwi. Hivi karibuni aliulizwa swali hilo kwenye mdahalo na akina Nape akaeleza hivyo hivyo. Kwa maneno rahisi ni kuwa washitakiwa wa ufisadi wanabambikwa kesi. Fikiria kubambikwa kesi na machungu yake? Ulishawahi kufuatilia au hata kuiskia kesi ya Mahalu? Umeshaskia mashahidi wanaotakiwa Mahakamani kumtetea mshitakiwa? Dogo, TAFAKARI!
 
Mleta mada hajui anachosema kabisaaa kwani akiwa mwanasheria si ni kazi yake kutetea watu au umehujui kazi yake pole badilisha mada kwani umechemka.

Uwe unasoma na kuelewa na sio kupost tu, nimesema naelewa anachokifanya marando ni kazi yake kwa kuwa ni mwanasheria lakini nikatahadharisha ya kuwa ameshachanganya na siasa na vilevile si wananchi wengi wenye uwezo wa kutenganisha hivi vitu viwili, Kuna umuhimu gani wa kuanza kuwaelewesha watu eti ile ni professional yake acha awatete na tusitumie huo muda kueneza zaidi somo hili la ufisadi kwa watz coz sio watz wote wameshaelewa madhara mazima ya ufisadi
 
Wale ni watuhumiwa bado hawajahukumiwa. Ana haki ya kuwatetea, kwani nao ni sehemu ya jamii ya Watanzania.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom