Marando atangaza kulitetea MwanaHalisi bure

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Leo Mabere Marando ametangaza wazi wazi kwamba baada ya Mhariri wa MwanaHalisi kutishiwa na Karamagi yeye alimwandikia Mhariri na kumthibitishia kwamba atawatetea bure na amewataka Umoja wa Wapinzani wakifikishwa Mahakamani atatumia pesa zake kuwatetea bure .

Your Say now
 
Leo Mabere Marando ametangaza wazi wazi kwamba baada ya Mhariri wa MwanaHalisi kutishiwa na Karamagi yeye alimwandikia Mhariri na kumthibitishia kwamba atawatetea bure na amewataka Umoja wa Wapinzani wakifikishwa Mahakamani atatumia pesa zake kuwatetea bure .

Your Say now

Brilliant Marando!!!
 
Leo Mabere Marando ametangaza wazi wazi kwamba baada ya Mhariri wa MwanaHalisi kutishiwa na Karamagi yeye alimwandikia Mhariri na kumthibitishia kwamba atawatetea bure na amewataka Umoja wa Wapinzani wakifikishwa Mahakamani atatumia pesa zake kuwatetea bure .

Your Say now

Mwisho wa MAFISADI ukielekea ukingoni hata pesa huwa hazifanyi kazi.

Kifo cha nyani miti yote uteleza. Sasa watu hawajali hata pesa, kazi ni kazi ukombozi kwanza pesa baadaye.

Karamagi(FISADI) hana nguvu kabisa kuna nguvu ya Umma ambayo ni kubwa sana zaidi ya Karamagi(FISADI)
 
Can Marando be truested? Huyu jamaa mission zake ni wazi kabisa, ni ofisa usalama wa taifa ambaye huwa anatumiwa na CCM kurekebisha mambo yao. Siquestion uwezo wake wa kazi ila naQ intetion yake. Just opinion
 
Bongolander your question is right ila sasa people do learn through mistakes. Marando yeye katoa offer na alimpigie yeye mwenyewe owner wa MwanaHalisi kusema yuko tayari kusimama na leo karudia ombi ikiwa watashitakiwa lakini bado haina maana kwamba atapelekewa kesi kama watu wana wasi wasi na yeye .Tanganyika ina mawakili kibao ambao wana sifa na wengine wanachipukia .So again issue ni kwamba wataamua when is right time .
 
Can Marando be truested? Huyu jamaa mission zake ni wazi kabisa, ni ofisa usalama wa taifa ambaye huwa anatumiwa na CCM kurekebisha mambo yao. Siquestion uwezo wake wa kazi ila naQ intetion yake. Just opinion

Bongolander,

Ni kweli kabisa unachosema ila pia kumbuka kuwa wanaovujisha hii mikataba ni hao hao wanausalama wa taifa au trusted members of the govt.

Wakati mwingine watu kama kina Marando wanatakiwa sana hasa nyakati kama hizi
 
Bongolander
JF Senior Expert Member
-----------------------------------------------------------------
Can Marando be truested? Huyu jamaa mission zake ni wazi kabisa, ni ofisa usalama wa taifa ambaye huwa anatumiwa na CCM kurekebisha mambo yao. Siquestion uwezo wake wa kazi ila naQ intetion yake. Just opinion


Mkuu Bongolander,

Heshima mbele, anytime mtu anapoandika bila ya unazi as you did here, inakuwa ni common sense, na siasa ya taifa at best, bravo on that,

Marando, Freeman, na Mrema, hawajwahi kuwa wapinzani hata siku moja, lakini tunwashukuru sana kwa kumkosesha tembo usingizi sometimes!
 
Mkuu Bongolander,

Heshima mbele, anytime mtu anapoandika bila ya unazi as you did here, inakuwa ni common sense, na siasa ya taifa at best, bravo on that,

Marando, Freeman, na Mrema, hawajwahi kuwa wapinzani hata siku moja, lakini tunwashukuru sana kwa kumkosesha tembo usingizi sometimes!

Wakati mwingine inabidi nijiulize kama ninahitaji kupewa maana au tafsiri mpya ya neno wapinzani.
 
Historia na kumbukumbu zinaonyesha kwamba wewe Es umekuwa na beef na Mbowe muda wote wa maisha yako. Je unataka leo niamini kwamba umeanza tena kuendeleza fitina ambazo zinaonekana hata kule CCM? Maana Malecela bila ya aibu na utu na hata bila ya kujali kwamba ni mzazi ila kwa kulinda tumbo lake na kwa uchache wao alitoa maneno makali dhidi ya Zitto na kuhitimisha kwamba atimuliwe Bungeni.Sasa yule mzee na labda uwezo wake wa Kisiasa sasa umefoikia kikomo kwa utetezi wake jambo kama lile .

Huoni kwamba hii ni advantage hata Malecela anaweza kuinga mkono kama kweli Mbowe , Mrema na Marando ni mali yao kwa kuwa wanaisaidia CCM .Je wewe huna furaha kwamba Chama chako kina msaada toka kwa hawa tu ? Maana maandiko yako yanaonyesha hasira kubwa kwa hawa watu 3 .Je unaweza kuelezea ni kipi cha mno?

Umesema hawa jamaa si wapinzani means ni CCM wenzio , je unaweza kuthibitisha madai yako maana labda mnashiriki wote katika vikao vya kuuza Nchi au ni bla bla zako za kima mara za ku derail ukweli ?

Heshima kwako nisaidie majibu
 
1.
Murangira
Senior Member
--------------------------------------------------------------------------------
Historia na kumbukumbu zinaonyesha kwamba wewe Es umekuwa na beef na Mbowe muda wote wa maisha yako. Je unataka leo niamini kwamba umeanza tena kuendeleza fitina ambazo zinaonekana hata kule CCM?

Mimi nimetoa hoja, lakini kama kawaida wewe unataka personal badala ya kujibu hoja, here I come,

Freeman, ni rafiki yangu wa karibu toka tukiwa watoto, alipopata ajali kwenye ile miaka ya 80s pale Salender Bridge, mimi nilikuwa ninacheza Disco RSVP, nilipoambiwa tu niliacha starehe zangu, na kuwa mtu wa kwanza kufika pale na ku-secure gari na mali zake pale kwenye scene ya ajali, na kuhakikisha kuwa usafiri wa kumepeleka Hospitali umepatikana, na mali zake zote pale zimefikishwa nyumbani kwake Sea View, ndipo nikaenda Hospitali Muhimbili, na washikaji wengine walioujiunga nasi mpaka asubuhi.

Mara ya mwisho alipoalikwa na Rais Bush, kuhudhuria mkutano wa Republican Party, kule NY mimi nilikuwa kule kwa shuguli zangu binafsi, na nilikuwa nilishirikiana naye throught out mpaka mwisho wa shughuli zake, baba yake mzazi alikuwa ni rafiki yangu zaidi na nilikuwa nikikaa naye sana kupiga story pale Sea View, familia yangu na ya Freeman, ni very intact, nimehudhuria vilivo vingi sana vya familia yake, na yeye pia na familia yake wamehudhuria sana ya kwetu, please hili la personal beef ba Freeman ninaomba uliondoe mawazoni mwako kuwa hata yeye na familia yake wakikusikia watakucheka sana!, maana to this day we are very close kifamilia!

2.
Maana Malecela bila ya aibu na utu na hata bila ya kujali kwamba ni mzazi ila kwa kulinda tumbo lake na kwa uchache wao alitoa maneno makali dhidi ya Zitto na kuhitimisha kwamba atimuliwe Bungeni.Sasa yule mzee na labda uwezo wake wa Kisiasa sasa umefoikia kikomo kwa utetezi wake jambo kama lile .

(a). Malecela, sijui anahusiana nini na hoja yangu,

However, Malecela ni mzee mwenye umri wa miaka 72, unless wewe kwenu hakuna wazee, maana wangekuwepo usingekuwa na tatizo la kuelewa kuwa wazee huwa hawaongezeki uwezo wa kisiasa wakifikia umri huo, ila huwa wanaongezeka busara zaidi kwenye any professional waliko,

(b). Hoja ya kumfukuza Zitto, bungeni alikuwa-created na Luwaassa, ambaye moja ya shughuli zake bungeni ni kusimamia shuguli za serikali ndani ya bungeni, ilishinikizwa na Mundhiri, na kupigiwa kura na wabunge wote walikokuwepo, Malecela alichangia kama mbunge, na makamu wa mwenyekiti wa CCM, na alichangia maoni yake kutokana na ishu ta hand, wabunge wengi walipiga kura ya kumsimamisha bunge kwa kufuata sheria za bunge, huo ulikuwa ni uamuzi wake binafsi kama una tatizo nao mtumie ujumbe au muandikie barua, na uwaaidikie wabunge waote waliohusika kumfukuza Zitto bungeni, hakufukuzwa kwa kura moja ya Malecela,

(c). Malecela, hakupiga kura wala kutoa maoni yake kwa ajili ya tumbo, hapana, maana yeye kama waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais mstaafu, kisheria ya taifa letu taifa linampatia nyumba mbili, moja Dodoma, nyingine Dar, walinzi wa personal na nyumbani, chakula, wafanyakazi wa ndani, magari mawili mapya kila mwaka, safari mbili za nje ya nchi kwa matibabu kila mwaka, ujumbe wa kudumu cc na NEC, mpaka atakapoitwa kwa muumba wake.
And this works for Kawawa, Seif Hamadi, Salim, Warioba, Sumaye, Mwinyi, Mkapa, Bilali, na Salmin.

Now guy, Malecela hahitaji kufanya kazi yoyote at this point and time kupata hayo mafao juu, hayo mafao yapo pale pale afanye kazi au asifanye, awe mwansiasa au asiwe, ajiunge na upinzani au asijiunge, mafao yatakuwa pale pale, kwa hiyo hoja ya tumbo uliyoisema ni mufilisi mkuu! sasa anaishi kwa mafao, haishi kwa mshahara wala posho!

3.
Huoni kwamba hii ni advantage hata Malecela anaweza kuinga mkono kama kweli Mbowe , Mrema na Marando ni mali yao kwa kuwa wanaisaidia CCM .Je wewe huna furaha kwamba Chama chako kina msaada toka kwa hawa tu ?

Furaha yangu ni pale tu, viongozi wetu wa upinzani na CCM, wanapofanya kazi ya kulisaidia taifa, lakini siwezi kuwa na furaha ya kuwa na kina the Marando likes kwenye siasa yetu, ninawaheshimu Zitto, na Dr. Slaa kwa sababu uwezo wao bungeni sijui kama unaweza kufikiwa na Freeman na Marando walipokuwa humo humo bungeni, ninaomba uniambie Freeman na Marando, walifanya nini walipokuwa bungeni?

Lakini ninamuheshimu Freman, kwa kuipa, meno makali Chadema, na kuweza kuwapatia Zitto na Slaa, platform ya kulisaidia taifa letu, lakini misaada ya kina the Marando likes kwa CCM, au kina Tambwe na Akwilombe, au Guninita? No thank you hawa hawana msaada wowote ila wanajali matumbo yaka ulivyosema, lakini hawana faia kwa taifa langu!


4.
Maana maandiko yako yanaonyesha hasira kubwa kwa hawa watu 3 .Je unaweza kuelezea ni kipi cha mno?

Mwananchi yoyote mwenye akili timamu atakayesoma huu ujumbe wako na wangu, sina sababu ya kuwa na wasi wasi kwake kuelewa mwenye hasira kati yangu na wewe ni nani, hilo wala halinisumbui maana ninaiamini sana hii forum kwenye hilo la kuchagua mchele na pumba!

5.
Umesema hawa jamaa si wapinzani means ni CCM wenzio , je unaweza kuthibitisha madai yako maana labda mnashiriki wote katika vikao vya kuuza Nchi au ni bla bla zako za kima mara za ku derail ukweli ?

Je na wewe unaweza kuthibitisha madai yako kuwa hawa kina Marando, ni upinzani?


6.
Heshima kwako nisaidie majibu

Heshima ikurudie mara mbili mkuu, na tuendelee kukta ishu na kumkoma nyani giladi mpaka milima ya Sinai!
 
nilivyopata ile email ya mwanahalisi waliyoisambaza kwa mabalozi na vyombo vya habari vya nje. niliitafutia fremu na kisha nikaipeleka benki kama special item deposit.

hata hivyo niliamini kuwa serikali ingechemsha sana kama ingejaribu kufungia au kushtaki mwanahalisi. Asante Marando kwa ofa yao ya kuwatetea mwanahalisi bure. kuna wanasheria wengi sana wanasubiria kwenye line kulitetea hili gazeti.

Marando, wewe kama ni sisiemu or not it is up to you. Fanya kile walichofanya hawa wanaovujisha hii habari tuliyopewa na viongozi kule urafiki.

Uthibitisho kama huu ndio unahitajika. yote waliyofanya sirini yatawekwa wazi hapa na JF kama kawaida yake itakuwa source ya mambo haya kwa wote tulio nje ya nchi.

mpaka kieleweke mwaka huu or otherwise!
 
Mzee Es you are good katika ku spin . Haya maneno yako ya kulia lia na kusema sana ili uweze ku justify madai yako nadhani ni muda sasa wana mtandao wamesha jua . Unajidai kila mara wewe na Mbowe ni kitu kimoja lakini uchochoroni umejawa fadhaa na uoga na unabakia kumrushia maneno ya nguoni.Si mara moja umetoa madai makali dhidi ya Mbowe lakini huna uthibitisho ndiyo maana nakuvaa ili uachane na blah blah hizi ial tukate issue .

Kumgusa Malecela nilijua utakuja na ngojera kibao lakini nasema Mzee yule ana tamaa na uroho wa madaraka .Hawezi kukaa bila ya madaraka kama Kingunge ndiyo maana na uzee wote na vyeo vyote na kumpamba kote bado anatala kufia kwenye Ubunge huku wananchi wa Mtera hawana lolote la maana .

Busara zipi unaongelea hapa za Malecela ? Yaani busara za kuamuru watu wapigwe kule kwa Cheyo kisa CCM wana dola ? Busara zipi ambazo hadi sasa hajamweleza mwenyekiti wake kuwa serious na kuangalia madai ya Slaa ?Busara zipi unazo ongelea zile za kupanga kuiba kura zetu ili wabaki madarakani?

Wachache hapa wamesha kujua kama Mwafrika wa Kike ila wengi hawajakujua . Ninacho kikataa ni kwamba uache kuleta majungu hapa ila tukate issue .Ila usikate issue kwa maslahi ya umimi ial kwa Taifa . Hivi si wewe majuzi ulidai kwamba Slaa ni muongo wakiwa na zitto na ukasema adhabu yao inakuja ni kufungwa na kufutika katika historia ya Siasa za tanzania na kwamba wana hatarisha usalama wa Nchi ? Umejua lini kwamba Slaa anasimamia maslahi ya Nchi yangu ?
 
Can Marando be truested? Huyu jamaa mission zake ni wazi kabisa, ni ofisa usalama wa taifa ambaye huwa anatumiwa na CCM kurekebisha mambo yao. Siquestion uwezo wake wa kazi ila naQ intetion yake. Just opinion

Haya ni maneno ya 'watumwa' wa Mrema. Yamewakaa hadi leo; ni wagumu wa kujifunza! Haya tuletee unayemtaka aliye bora kuliko Marando.
 
Hivi si wewe majuzi ulidai kwamba Slaa ni muongo wakiwa na zitto na ukasema adhabu yao inakuja ni kufungwa na kufutika katika historia ya Siasa za tanzania na kwamba wana hatarisha usalama wa Nchi ? Umejua lini kwamba Slaa anasimamia maslahi ya Nchi yangu ?

Labda hii peke yake ndio hoja ya msingi kwenye post yako maana mengine nimeshayajibu kule mwanzo, naona kwenye hili wewe na mjumbe mwingine hamjanielewa vizuri, nilisema na ninarudia tena kesi iende mahakamani ili ukweli ufahamike uko wapi, kama viongozi wetu wamehusika wahukumiwe kwa the full strength ya sheria zetu, na ikibainika kuwa Zito na Slaa, hawana ushaidi wa ukweli kisheria, basi wafunguliwe kesi ya uhaini ambayo itawafanya tusiwasikie tena kwenye siasa, yes I stand on this words na ndio niliyoyasema, kama unapingana nayo weka hoja yako, na majuzi tu mwanasheria mkuu amesema kuwa wale wote waliohusika na kuvunja sheria kwenye mkataba wa Radar wakipatikana watafunguliwa kesi ya uhaini, sijui kama umesikia?

Malecela is doing just fine at his age, kama ni kupenda madaraka, naomba unitajie kiongozi yoyote au mwana siasa yoyote unayemjua duniani asiyependa madaraka, kuamua kufia kwenye ubunge wake huko Mtera, nitakusikiliza kama ni kuvunja sheria za nchi yetu, otherwsie umejawa na wivu tu mkuu, ambao hauwezi kutusaidia kwenye taifa letu

katika hiii forum, ninafahamika kwa kukata ishus kiroho mbaya na kumkoma nyani mchana kweupe mpaka giladi, na kusimamia hoja, na pia kutetea haki za wanyonge, nina marafiki wengi sana in the real life kwenye hii forum, na wengine through PM, na wengine through e-mail, Mwafrika Wa Kike ni my "former friend" lakini "turned enemy" recently kutokana na kutofautiana kiitikadi, lakini ninamuheshimu tena sana kwa a bold stand on any ishus za kisiasa, and I wish wangekuwepo wengine kama yeye wengi zaidi, otherwise sina ugomvi naye huwa ninasema mara moja halafu ninasonga mbele, ninasahau ya jana na kujali ya leo,

kuanzia kwenye PM na mahali popote pale sijawahi kukosea kuwajua wanaotumia majina mengi, maana huko nyuma sana in the past, leo nitakwambia ukweli kulikuwa na moderator mmoja ambaye siku hizi hayumo humu tena hapa forum, aliyekuwa na tabia ya kutoa ID za watu humu, ndio mana nikawajua watu wengi humu, maana huko alikokuwa akiyatoa nilikuwa na access nako, narudia hilo sijawahi kukosea kama ndio unalolisema,

Freeman, tunatofautiana kiitikadi ya siasa ya taifa letu, otherwise yeye na familia yake ambao wengi wao wapo hapa wanakuangalia na maneno yako, ni ndugu zangu wa karibu sana siasa haijawahi kutuletea problem hata siku moja, kama kweli unawaamini Marando na the likes kuwa ni wapinzani, then usingekuwa na tatizo, the fact kwamba una tatizo inaonyesha kuwa na wewe huwaamini au?

Ahsante Mkuu, tuendeelee kukata ishu!
 
Field Marshal ES,

Kama unamjua Mbowe kama rafiki yako ni vema lakini huwezi kujua kila jambo kuhusu Mbowe; huwezi kutuambia kuwa Mbowe ni binadamu asiyebadilika. Kama urafiki wa enzi zenu ulikuwa wa kucheza dansi na kusaka shilingi, mwenzako sasa kashapiga hatua nyingine. Ungekuwa rafiki yake kweli ungemuunga mkono. Tatizo lako wewe unamhukumu Mbowe kwa hisia na judgment za utoto wenu...mwezi mtu mzima sasa. hapa hakuna nafasi ya utoto...tunajadili mambo serious!

Kuhusu upinzani: mpinzani ni mtu yeyote ambaye hakubaliani nawe kuhusu jambo (lolote). Unataka kutuambia Mbowe, Marando na Mrema hawajawahi kupingana na jambo lolote linalofanywa na serikali? Sera zake? Sheria zake? Utaratibu wake wa kufanya mambo? Ndiyo, watu tuna kasoro na tofauti zetu, lakini huwezi kupuuza mchango wa watu hawa katika harakati za mageuzi Tanzania.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom