Marais wetu wanajitambulisha nje ili iweje?

Spiderman

JF Admin
Jan 1, 1970
7,219
441
Kujulikana ni jambo la kawaida katika jamii, lakini jambo la msingi ni kuangalia unajulikana kwa mambo gani.

Kama ni kujulikana tuu, hata Adolf Hilter, Iddi Amini Dada na Bokasa wanajulikana, lakini wanajulikan akwa mambo gani, ndilo jambo la msingi.

Katika nchi zetu za Kiafrika, imezoeleka kuona viongozi wa juu wanapochanguliwa tuu wanakimbilia nchi za Ulaya na Marekani wakidai wanaenda kujitambulisha.

Hilo ni jambo jema, lakini je, kuna umuhimu sana wa kwenda kujitambulisha? Kuna vitu ambavyo vinaweza vikamfanya kiongozi ajulikane, hata kama hajajitambulisha. Na kwa kawaida, mtu hujulikana kwa yale mambo makubwa aliyofanya, si kwa kujitambulisha tu.

Ni wazi kuwa viongozi kama Nelson Mandela na Mwalimu Nyerere wanajulikana duniani kote, kwa kupigania na kutetea haki za Waafrikam kutafuta uhuru na kupinga unyonyaji katika bara la Afrika.

Jambo la kujiuliza ni kwa mbona viongozi wa Ulaya na Marekani wanapochanguliwa hawaji Afrika ili waje wajitambulishe kama viongozi wetu wanavyofanya, lakini bado wanajulikana?

Isitoshe, kama rais atatembelea kila nchi kwa muda wa siku tatu kwa lengo la kujitambulisha, itachukuwa miaka miwili kuzimaliza. Ingependeza kama viongozi wetu wangetulia nyumbani wakawatumikia wananchi wao kuliko kutembea huku na kule wakidai wanajitambulisha.

Kujitambulisha ni vyema lakini uchapa kazi wako, sera nzuri, kusimamia masilahi ya nchi na maendeleo kwa wananchi kunaweza kumfanya kiongozi ajulikane na akumbukwe hata kama hayuko madarakani.
 
Nyerere naye alikuwa anaenda nje kujitabusha??

Mbona anajulika sana huko nje?

ninadhani alikulikana kutokana na misimamo yake na uchapaji kazi wake by then.

Ingawaje kwa westernes kama wewe ulikuwa socialist au communism basi wewe ulikuwa adui mkubwa. Waliowaondoa watu kama Kwame, Lumumba, Austino Neto kwa wasi wasi tu kuwa watafuata msimamo wa East block by then.


Huko Ulaya hakika wana hamu kubwa ya kurudi kututawala na kutuibia in the name of investors etc.

Na wanataka kupta viongozi kama walivyokuwa akina Mabuti ili ku"acomplish malengo yao' HAKIKA VIONGOZI WETU WANACHAGULIWA NA WATU WAO BADALA YA KUKAA CHINI NA KUTAFUTA UFUMBUZI WA KWELI WA KUPAMBANA NA HII VITA YA UMASIKINI, TUNAANZA KUIKIMBIA KIMBIA KWENDA ULYA KUPIGA MAGOTI YA NINI HASA?

AU UONGOZI UMEWASHINDA?
 
Admin, Mkira,
hakuna ulazima wa viongozi wetu kwenda kujitambulisha nchi za nje. kuna balozi za nchi za nje zinatuma taarifa ndefu na za kina kuhusu nani ameingia madarakani Tanzania.

Kabla Kikwete hajaingia Marekani, Uingereza n.k, tayari wanakuwa wanamjua undani wake. wanajua ni kiongozi wa namna gani, pamoja na mwelekeo wake kisera.

kwa kweli hakukuwa na ulazima wa Kikwete kwenda USA kuzungumza na Cheney na Dr.Rice kwa muda usiozidi saa moja. hakukuwa na haja ku-fly all the way from Tanzania to pay a courtesy at the WB na IMF, ukizingatia kwamba Wolfowitz alikuwa keshapanga kuja Tanzania.

Zaidi, kulikuwa na ulazima upi wa Kikwete na Lowassa wote kwenda USA ndani ya mwezi mmoja?? Halafu wote wanafanya ziara UAE!! Kwanini ziara hiyo isifanywe na kiongozi mmoja??

Taifa linapoteza fedha nyingi kwa gharama zisizo za lazima za viongozi wakuu wa serikali.
 
JokaKuu nakuunga mkono kabisa kujuliakana kwa JK si kwa US na UK tu Nchi wanamjua .JK ni mtu wa CCM miaka mingi sana wengine hamjazaliwa JK ni kiongozi .Amekuwa Waziri wizara tofauti na zaidi Mambo ya Nje .Bush alichukua Nchi uliza kafanay ziara ngapi za kujitambulisha ama Blair ama rais wa Ujerumani ambaye juzi alikutana na JK . Nasema JK anawachezea Watanzania wana mbwembwe na watanzania wanaumia .Pesa zinaliwa na watu wanachelewa umaarufu wa Rais .Wazungu kumjua JK ni lazima maana kuna mahala Mkira kasema kwamba wana nia ya kutaka kurudi Africa na wamesha rudi kinamna ni lazima tu watamjua JK na si lazima JK kujulikana kwao wanapashwa kuijua Tanzania na wanaijua kwamba sisi ni matajiri tuna kila kitu kuanzia makaa ya mawe , gesi , hadi urenium na mafuta sasa tunataka nini ? Mbuga za wanyama Mlima mrefu sana Africa ,ok siasa za uoga pia tunazo na sasa tuna amani ambayo sijui itadumu hadi lini .
 
Mzee Chifu,

Hawa wazungu wote kwenye ofisi za ubalozi zao bongo wana maafisa wa ujasusi, kuanzia CIA, KGB, FBI, M16, Mount Royal-Canada, siku hizi mpaka NYPD wana majasusi wao hapa bongo,

wakati wa uchaguzi wetu wa rais, na wabunge kazi yao hawa jaamaa ilikuwa kuangalia kwa makini interest zao hapa bongo, na hasa dini za viongozi, kwani interest kubwa yao hapa sasa hivi ni Mujahadina, na Al-Queda, kwamba hawatapata safe haven,

kwa hiyo hawa majajsusi, tayari walishapeleka habari za rais mpya hata kabla hajachaguliwa kule Dodoma, ndani ya CCM, ndio maana mabalozi wa UK na US walikuwa hawaishi majumbani kwa JK na JM, kile kipindi kila wiki, tena walikuwa wakiwafuata mpaka Dodoma na Bagamoyo/Chalinze,


kwa hiyo habari za JK zilikuwa kule State Department siku nyingi, hata kabla mzee hajaenda kujitambulisha, na rais wa US na West kwa ujumla tayari walikuwa na habari zake zote, in details,

Now lets look at kujitambulisha, unaendaje kujitambulisha kwa rais ambaye tayari ulishaarifiwa kuwa hana nafasi ya kukuona? Bush aliambiwa hana nafasi, Kule German hivyo hivyo aliambiwa hana nafasi, mzee Blair ndio kabisaa hana nafasi, lakini rais wetu akaenda anyway! kujitambulisha kwa mawaziri na kina Chenney, what a shame! Kina Mwai Kibaki na Kagame wanakwenda kwa safari za kibinafsi lakini wanapokelewa na Bush mwenyewe kule Rose Garden na mpaka Oval Office, lakini wa kwetu aliyekuja rasmi kujitambulisha wanaishia kule Watergate Office kwa kina Chenney, aibu!

Yaani hata huyu mama wa ujerumani naye amekataa kuwa yuko bussy, so far rais wetu amepokelewa na mzee Chirac tu na tunajua siri yake anataka kuchukua miradi yote inayomilikiwa na US hapa bongo, maana US imechukua miradi yake yote kule Sierra Leone, na Senegal, na Congo-Zaire, kwa kuwatumia kina Kagame na M7,

Mzee JK, na Mtandao hizi sifa zitawaua, tulitegemea kuwa rais mpya atasimamisha safari za viongozi wetu wote wa taifa kwa angalau miaka miwili tu ili kuweka mambo sawa hapa nyumbani, kumbe ni yale yale ya Mkapa, ya kutaka ujiko nje huku nyumbani kumeoza, mnakimbilia kuvaa suti kwenda kwa wazungu ambao they are so bussy kiasi kwamba hawana nafasi ya kuwaona marais mnaowakilisha wananchi karibu 40 Millioni!

Ni lini mtasikia aibu kama waafrika na kutulia kwenu kama wazee wa Swazi na Botswana, ambao hawaendi huko kila leo lakini nchi zao ni bomba na kila siku tunakimbilia huko bondeni? Aibu acheni hizo!
 
Mzee ES, Admin,
Heshima zenu. Nadhani wakati umewadia rais wetu akumbushwe kuwa yeye si Foreign Minister tena. Haya mambo ya globe trotting ni aibu tupu. Nasikia Septemba anakuja tena Marekani. Atakuwa UN, ataenda California na Minnesota.
 
Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote! Labda Kikwete anadhania hawamkumbuki? Watu wakuu hawakumbukwi kwa mambo madogo.. wanakumbukwa kwa mambo makubwa!! Kama Kikwete yuko makini na anachotaka kufanya basi ashughulikie mambo makubwa, ambayo ni:

a. Kubadilisha uchumi wetu na kuufanya wa kisasa zaidi (kilimo kikiwa ni kipaumbele).
b. Kubadilisha elimu yetu ili iwe inayokwenda kwa wakati, inayopatikana kiurahisi, na yenye kufaa wakati huu.
c. Kubadilisha mwelekeo wa kisiasa, kwa kushughulia mara moja na milele suala la Zanzibar.
d. Kuja na mikakati yenye kina ya kupambana na tatizo la Ukimwi na ubovu wa sekta ya afya.
e. Kuhakikisha kuwa miundo mbinu ya Tanzania, inaboreshwa na kufanywa ya kisasa zaidi.

Rais akionekana angalau anashughulia mambo hayo, basi awaache wengine waende nje na picha yake kumtambulisha!!!!
 
Dah! Mimi naona ni kazi nzuri sana kwa rais wetu kwenda kujitambulisha nje! kwanini??!! ndio swali watu wanajuiliza hilo

Kwanza.. Rais wa awamu ya tatu alienda kujitambulisha nje ya nchi.. sasa ikaja uchaguzi mwingine ndio kikwete kachaguliwa.. sasa lazima aende nje kujitambulisha kwanza kama rais mpya wa tanzania.. kwa nchi zingine... na kuongea na wananchi rai wa tanzania.. huko nje. Sasa mimi hio naona ni lazima sana rais aende kujitambulisha.

Nchi kama Ulaya, na zinginezo zina balozi.. na katika hizo balozi zina picha ya rais kikwete.. sasa kama rais wa nchi hio(ulaya) au kiongozi yeyote akienda kuangalia pale.. hawezi kumjua kikwete kwa picha tu.. lazima wakutane waongee...

Na mnaajua kwamba Tanzania... tunauhaba wa pesa.. kutokana na RUSHWA.

Sasa ni lazima kwa rais wetu.. kujitambulisha nchi zingine... kuomba msaada.. kwasababu tanzania bado tunahitaji Wawekezaji, Tunahitaji watu wa kununua bidhaa zetu.. Tunahitaji kukuza uchumi wa nchi yetu.

Sasa kama rais kikwete akienda kujitambulisha huko ni sawa tu.. na pia kwa marais wote.. huo ndio muundo wao nadhani. kwamba kwenda kujitambulisha...

Naomba nirekebishwe nilipokosea.... na Kupata maoni yenu.
 
Richard Williams,

Mawazo yako yapo safi. Ila fikiria haya yafuatayo,

1. Ngoja msafara wa rais unapita halafu anza kuutupia mawe(huna nia ya madhara makubwa)

2. Nenda kateke radio Tanzania na TVT kisha tangaza nchi imepinduliwa na wewe.

3. Kachore katuni na kuichapisha kwenye gazeti lako la kiswahili na kiingereza au iweke kwenye tovuti.

4. Ita waandishi wa habari kisha tangaza unaenda Lebanon kusaidia kuwapa fedha na kusaidia kuipiga Israel

Ukifanya hayo yote au baadhi au moja itatokea nini?? NAOMBA MAJIBU.

Sasa turudi kwenye upande mwingine wa sarafu:
Assume wewe ndio JK.

1. Anza kampeni kwa wananchi wote kila mtaa, shawishi wananchi wawe na moyo wa kujitolea na kusaidia jamii, kutengeneza barabara(zisizo za lami), kusafisha mazingira, wenye uwezo kusaidia jamii kama Raza alivyofanya Zenji majuzi.(wenye kutaka sifa kama Manji wamejaa tele acha wenye huruma kama mimi).

2. Kufanya wananchi wanayolilia, kuondoa mikataba feki yote, including wa TRC (haujaingiwa lakini ni siri), kuhakikisha misaada mingi inatolewa na wananchi wenyewe, kuacha kununua ma shangingi na kujenga mahospitali na mashule. Kupunguza mikutano na kongamano na seminar na warsha ......

3. Kupanua sekta ya uchumi na kuipa kilimo kipaumbele kwasababu ni source kubwa ya export, (uki export unapata Usd, hence Tzs ina appreciate, balance of payments inakuwa fresh)

4. Kuwajali wafanya kazi wa serikalini, na kuifanya serikali best employer, ili iwa atract wasomi na best students. Hii itawafanya wafanyakazi kuwa responsible na kuwa na hofu ya kupoteza kazi..(who cares if she/he loses a job paying 80Usd per month take home - graduate huyo!! no wonder wanaiba!!)

5.Kusisitizia ujenzi wa miundo mbinu, wawekezaji wa kutoka nje wawekeze kwenye huduma za jamii na miundo mbinu.

6. Kupunguza utitiri wa expatriates Tanzania. Na kuteua wafanyakazi (mawaziri na viongozi serikalini) kwa vigezo vya utendaji na sio vinginevyo

7. Kusomesha wanafunzi wanao onyesha vipaji maalum ktk vyuo vyenye standards kubwa kisha kuhakikisha wanarudi na kuifanyia Tanzania kwa miaka isiyopungua kumi, (msisitizo kwenye science na technology). Kushirikiana na Universities na kuwekeza ktk researches za ki science.

Sasa ndugu yangu naomba uniambie kama ukifanya vitendo vya mwanzoni na rais akifanya hayo mambo saba (sio exhausted list) itakuwaje kwenye kujitanga kimataifa?(kujulikana?)
Bila kupinga ukifanya hayo hapo juu(saba) UCHUMI UTAKUA, badala ya JK kwenda kujitambulisha wao ndio watamtambua na kuanza kumtafuta....UONGO???

Hope nimekujibu

FD
 
Sorry naomba isomeke hivi....

3. Kachore katuni ya kumdhalilisha mtume Muhammad (S.A.W)na kuichapisha kwenye gazeti lako la kiswahili na kiingereza au iweke kwenye tovuti

FD
 
Kama atatokea rais KATIKA NCHI ZA africa na kufanya kazi NZURI. MFANO KWA KUFUATA vipengele alivyosema hapo juu bwana FD. Ninadhani hatakuwa na muda wa kwenda kujitambulisha nje ya nchi BALI HAO WALIOKO NDANI NA NJE YA NCHI WATAMTAFUTA HUYO RAIS NA KUANZA KUMTANGAZA WENYEWE KWA NGUVU ZOTE. BADO KITAMBO KIDOGO ATAPATIKA KWA KUCHAGULIWA NA WALA SI VINGINEVYO. WANANCHI WATAGUNDUA TU KUWA WANADANGANYWA SI MUDA MREFU NA WATAWAKATAA HATA KAMA WATATUMIA MABILIONI YA FEDHA KUWAHONGA WATACHUKUA LAKINI HAWATAWACHAGUA. LET US BE OPTIMISTIC. TUOMBE VYUO VIKUU VIJENGWE ZAIDI! JAPO SASA TUNASIKIA WAMEMSHTUKA NA KUSEMA SERIKALI HAITAWAKOPESHA WATAKAOSOMA KATIKA PRIVATE UNIVERSITY.

NA PIA WAVULANA WENYE DIVSION ONE TU NDIYO WATAKAOPESHWA NA SERKALI!
ILA WATAENDELA KUWEKA VIONGOZI WAO KAMA WATAREKEBISHA UTAWALA WAO, KUFUATILIA MIKATABA FEKI KAMA IPTL, KIA, MEREMETA, ETC NA KUACHA KUSAINI MINGINE FEKI.

OGOPA NGUVU YA KURA INATISHA! NDIYO MAANA HUKO MASHARIKI MWA ZAIRE PAMOJA NA KUWA AZARIAS RUBERWA ANA MAJESHI YAKE HUKO. LAKINI KABILA AMEZOA KURA NYINGI SANA HUKO!
 
Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote! Labda Kikwete anadhania hawamkumbuki? Watu wakuu hawakumbukwi kwa mambo madogo.. wanakumbukwa kwa mambo makubwa!! Kama Kikwete yuko makini na anachotaka kufanya basi ashughulikie mambo makubwa, ambayo ni:

a. Kubadilisha uchumi wetu na kuufanya wa kisasa zaidi (kilimo kikiwa ni kipaumbele).
b. Kubadilisha elimu yetu ili iwe inayokwenda kwa wakati, inayopatikana kiurahisi, na yenye kufaa wakati huu.
c. Kubadilisha mwelekeo wa kisiasa, kwa kushughulia mara moja na milele suala la Zanzibar.
d. Kuja na mikakati yenye kina ya kupambana na tatizo la Ukimwi na ubovu wa sekta ya afya.
e. Kuhakikisha kuwa miundo mbinu ya Tanzania, inaboreshwa na kufanywa ya kisasa zaidi.

Rais akionekana angalau anashughulia mambo hayo, basi awaache wengine waende nje na picha yake kumtambulisha!!!!
Just remembering this, which was written on 1st August 2006,
 
Hili ni wazo mwanana.Congratulations.Ni wale marais wasiokuwa na cha kuwapa wananchi wao ndio wanaotoa hoja kama hizo zilizofirisika.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom