Maradhi shambulizi ya moyo

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,080

heart-disease-visual-guide-s2-heart-attack.jpg

SHAMBULIZI LA MOYO (HEART ATTACK)








Moja ya magonjwa hatari sana ambayo yanaweza kumpata mtu yoyote ni ugonjwa wa shambulizi la moyo. Huu ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo vya wanaume na wanawake.

Kwa kawaida, ugonjwa huu hutokea pale ambapo sehemu ya nyama ya moyo inapoharibika au kufa kutokana na kukosa damu ya kutosha.

Je tatizo hili husababishwa na nini?
Husababishwa na kuziba kwa mishipa ya damu inayosambaza damu katika moyo (coronary artery blockage) kutokana na mafuta mabaya mwilini (atherosclerotic plaque).

Watu gani wapo katika hatari ya tatizo hili?
Watu walio katika hatari ya kukumbwa na ugonjwa huu ni pamoja na


  • Wenye umri mkubwa miaka 45 kwa wanaume na 55 kwa wanawake
  • Wavutaji wa sigara
  • Watu wenye mafuta ya lijamu katika damu au wale wenye mafuta mabaya aina ya triglycerides na low density lipoprotein kwa kiwango kikubwa katika damu zao
  • Wenye kisukari
  • Wenye matatizo ya shinikizo la damu
  • Walio na unene kupita kiasi (obesity)
  • Wenye matatizo sugu ya kushindwa kufanya kazi kwa figo zao (chronic renal failure)
  • Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)
  • Wanywaji wa pombe kupindukia
  • Watumiaji wa madawa ya kulevya hasa cocaine na methamphetamine
  • Watu wenye msongo wa mawazo (Chronic high stress levels)
  • Upungufu wa vitamin B2, B6, B12 na folic acid
Dalili za shambulizi la moyo

  • Maumivu makali ya ghafla kifuani ambayo husambaa kwenye taya, shingo, bega na mkono wa kushoto
  • Kupumua kwa shida
  • Kutoka jasho kwa wingi sana (diaphoresis)
  • Kuhisi mapigo ya moyo yanapiga haraka (palpitations)
  • Kichefuchefu
  • Kutapika
  • Kuchoka haraka sana
  • Kupoteza fahamu
Shambulizi la moyo limehusishwa na nini?
Tafiti mbalimbali zimeusisha mambo yafuatayo na shambulizi la moyo


  • Msongo wa mawazo
  • Maambukizi hasa vichomi vinavyosababishwa na vimelea vya chlamydophila pneumonia.
  • Hutokea zaidi asubuhi hasa saa tatu (saa 3 asubuhi)

Vipimo na uchunguzi

  • ECG - Kipimo hiki huonyesha ni sehemu gani ya moyo iliyoathirika
  • Coronary angiography - Kinasaidia kwa kuangalia wapi ambapo mishipa ya damu imekuwa membamba sana kupita kiasi (narrowing of vessels) au imeziba.
  • Cardiac markers levels
  • X-ray ya kifua (chest X-ray)
  • MPI (Myocardial Perfusion Imaging) - Kipimo hiki hufanywa kwa kutumia mashine maalum ya PET Scan ambapo kinauwezo wa kugundua tatizo la shambulizi la moyo, huchunguza kikamilifu maumivu ya kifua, huangalia mwelekeo wa tiba ya kuzuia damu kuganda, hutoa mwelekeo wa ugonjwa wa shambulizi la moyo kama ni mzuri au mbaya, hutathmini ubora wa tiba ya shambulizi la moyo kabla na baada ya mgonjwa kupata tiba, huweza kutambua hata shambulizi la moyo ambalo si rahisi kugundulika kwa kutumia vipimo vyengine na pia hutathmini ukubwa wa tatizo la shambulizi la moyo. Hata hivyo kwa sasa kipimo hiki hakipatikani nchini kwetu.
Ili kuweza kutambua uwepo wa tatizo hili, mwaka 1979, shirika la Afya Duniani (WHO) liliweka vigezo vya kutambua shambulizi la moyo. Vigezo hivyo ni

  • Historia ya kuwa na maumivu ya kifua zaidi ya dakika 20
  • Mabadiliko katika kipimo cha ECG, na
  • Kupanda na kushuka kwa kipimo kiitwacho kitaalamu cardiac biomarkers hasa creatine kinase - MB na troponin
Matibabu
Shambulio la moyo ni tatizo linalohitaji matibabu ya dharua. Lisipotibiwa kwa haraka husababisha kifo katika muda mfupi sana tangu mgonjwa apatwe na tatizo. Matibabu ya tatizo hili hujumuisha


  • Kumpa mgonjwa hewa ya oksijeni
  • Mgonjwa hupewa vidonge vya Aspirini ndogo kuzuia damu kuganda (thrombolytic) kwa ajili ya kuyeyusha damu iliyaganda na hivyo kuzibua mirija midogo ya damu katika moyo iliyozibwa na kuganda huku kwa damu.
  • Vile vile mgonjwa hupewa dawa za kuweka chini ya ulimi kiitwacho nitrogylycerin (glyceryl trinitrate) ambazo husaidia kutanua mishipa ya damu (vasodilation)
  • Dawa ya kutuliza maumivu kwa mfano morphine
  • Dawa ya kuyeyusha mafuta katika mishipa ya damu kama vile clopidogrel
  • Kuzibua mishipa ya damu inayosambaza damu katika moyo kwa kutumia - Percutaneous coronary intervention (PCI)
  • Upasuaji (CABG)
Njia za kuzuia shambulizi la moyo

  • Kuacha kuvuta sigara
  • Kufanya mazoezi ya mara kwa mara
  • Kupunguza unywaji wa pombe
  • Kubadilisha aina ya mlo. Kupunguza mafuta katika mlo na chumvi.
  • Kutumia mafuta ya samaki (omega-3 fatty acids)
  • Kuna utafiti unaosema kuwa uchangiaji damu hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo hasa kwa wanaume.
Madhara ya shambulizi la moyo

  • Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)
  • Matatizo katika mfumo wa mapigo ya moyo (Atrial fibrillation) ambayo hatimaye hupelekea kifo
  • Shambulizi la moyo kurudia mara ya pili
  • Kifo cha ghafla (sudden death)
Shambulizi la Moyo (Heart Attack)
 
Asante kwa kutukumbusha tujitahidi kurekebisha life style zetu ili kuwa na afya bora - japo ni changamoto kubwa.
 
Uuuh na mimi nasubiri tiba asili ya hili tatizo, pleasee Mzizimkavu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
hata mimi nina tatizo kama hilo naomba mzizi mkavu amwage shule ya miti shamba hapo

Uuuh na mimi nasubiri tiba asili ya hili tatizo, pleasee Mzizimkavu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
DAWA YA MASHAMBULIZI YA MOYO (HEART ATTACK) KUNYWENI KWA WINGI MAJI YA UVUGUVUGU BDIO DAWA KUBWA YA MASHAMBULIZI YA MOYO.


Heart Attacks and Drinking Warm Water

heart_01.jpg
This is a very good article. Not only about the warm water after your meal, but about Heart AttacksThe Chinese and Japanese drink hot tea with their meals, not cold water, maybe it is time we adopt their drinking habit while eating.

heart_02.jpg
For those who like to drink cold water, this article is applicable to you. It is nice to have a cup of cold drink after a meal. However, the cold water will solidify the oily stuff that you have just consumed. It will slow down the digestion. Once this 'sludge' reacts with the acid, it will break down and be absorbed by the intestine faster than the solid food. It will line the intestine. Very soon, this will turn into fats and lead to cancer. It is best to drink hot soup or warm water after a meal.
Common Symptoms Of Heart Attack...
heart_ani.gif
A serious note about heart attacks - You should know that not every heart attack symptom is going to be the left arm hurting. Be aware of intense pain in the jaw line.
You may never have the first chest pain during the course of a heart attack. Nausea and intense sweating are also common symptoms. 60% of people who have a heart attack while they are asleep do not wake up. Pain in the jaw can wake you from a sound sleep. Let's be careful and be aware. The more we know, the better chance we could survive.
A cardiologist says if everyone who reads this message sends it to 10 people, you can be sure that we'll save at least one life. Read this & Send to a friend. It could save a life. So, please be a true friend and send this article to all your friends you care about.
I JUST did...
 
Mkuu MM somo limekuja wakati muafaka maana Dar sasa ni gumzo kuwa haya maradhi sasa kinga yake ipo pia yanaambukiza tu
 
Back
Top Bottom