Mara ya mwisho kulia (kilio) ni lini? Ilikuwa kwa jambo gani?

2weeks ago

Sababu ni depression
Goddess,ninajua unachokipitia,ukiwa kwenye hiyo hali lia kweli kweli,lia haswaa,haya maisha acha tu,tunapanga mengi mazuri na tunakuwa na matarajio makubwa sana,ila the theory of nature inatushauri kuwa tayari kuyaona,kuyasikia na kufanyiwa yote tuyapendayo na tusiyoyapenda,hapo ndyo sisi binadamu hujikuta kwny hali ya hopping for the best but expecting for the worst,pole sana
 
Jana tu nimelia sn baada ya kupata taarifa za kifo cha school mate,dom-mate,comb-mate kilichotokea mbeya huko kwa kupigwa na side mirror ya gari akiwa anatembea pembeni ya barabara. Imeniuma sn

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nililia sana na hadi Leo nikikumbuka siishagi kulia,tarehe 16/09/2016 Mimi na mchumba wangu tukiwa safarini kutoka dar to songea tukisafir kwa basi la new force,usiku wa saa mbili kijijini kifanya - njombe basi lilipinduka,nikaumia mkono wa kushoto,mchumba wangu akawa na hali mbaya sana,damu zilikuwa zinamvuja maskioni,puani na mdomoni alikuwa anatema damu tu,aliongea maneno machache ambayo hadi Leo nikiyakumbuka siishagi kulia,muda mfupi sana baada ya hapo akafariki dunia akiwa anawahishwa hospitali ya mission Ikonda,RIP minza na bado ninakupenda sana,nimejaribu kupenda kwingine sabab mm ni binadamu siwez ukwepa ubinadam ila haijasaidia,popote ulipo jua ninakupenda sana sana minza naomba niishie hapa maana naandika nikiwa ninalia,pumzika kwa amani minza wangu
Daaaaahhhhh pole mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mara ya mwisho kutoa chozi ilikuwa mwezi wa 3 mwaka jana (2020), Eva wangu alikuwa anaumwa sana halafu dalili zilikuwa za corona.

Nilikuwa mbali nae, yeye alikuwa DSM na mimi nilikuwa kijijini kwetu. Alinipigia simu tukawa tuonaongea nae japo kwa shida sana (ishu ya upumuaji) .Nilijikuta chozi linanidondoka kidume. Dah!!

Mungu ni mwema, dogo alipona na mida hii nimetoka kubonga nae....
 
Mara ya mwisho kutoa chozi ilikuwa mwezi wa 3 mwaka jana (2020), Eva wangu alikuwa anaumwa sana halafu dalili zilikuwa za corona.

Nilikuwa mbali nae, yeye alikuwa DSM na mimi nilikuwa kijijini kwetu. Alinipigia simu tukawa tuonaongea nae japo kwa shida sana (ishu ya upumuaji) .Nilijikuta chozi linanidondoka kidume. Dah!!

Mungu ni mwema, dogo alipona na mida hii nimetoka kubonga nae....
Kumbe uzi wangu huu bado upo...

 
Karibu kila siku nalia,ninaposali na kuutafakari upendo wa Mungu na alikonitoa najikuta chozi linadondoka.
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom