johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,832
- 141,749
Aliyekuwa mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara yupo mubashara Clouds 360 anaelezea jinsi ruzuku ya chama inavyofisadiwa.
Mwita anadai mbunge wa Tarime John Heche alipokuwa mwenyekiti wa Bavicha alikuwa analipwa mshahara sh 1.5 mil kila mwezi kinyume cha utaratibu.
Anadai wabunge wa viti maalumu ndio mtaji wa Mbowe pale CHADEMA.
Anadai yeye ndio mbunge bora wa jiji la Dsm, amejenga madaraja na hospitali pale Chanika na kwamba wakati wa mafuriko wapiga kura wake huja nyumbani kwake kupata hifadhi.
Kadhalika anadai ameondoka Chadema baada ya Mbowe na Dr Mahanga kumhakikishia kuwa hataitishwa kugombea tena 2020.
Mwita anadai mwaka 2008 alihama CCM na kwenda Chadema baada ya kugombana na aliyekuwa Katibu mkuu mzee Makamba na yule mwenyekiti wa UVCCM Dr Nchimbi.
Amesisitiza kuwa amejiuzulu ubunge muda huu baada ya kuona kuna fursa ya yeye kurudi tena bungeni katika uchaguzi mdogo kwa tiketi ya CCM hivyo hakuna atakachopoteza. Pia amedai yeye hakuutaka uenyekiti bali alitamani sana Mwenyekiti wa chama taifa awe Tundu Antipas Lissu.
Amemaliza kwa kusema ameshachukua fomu ya kugombea tena ubunge wa Ukonga na kwamba katika mazingira ya kisiasa akitokewa na baya lolote atamhisi Mbowe!
Source: Clouds tv!
Mwita anadai mbunge wa Tarime John Heche alipokuwa mwenyekiti wa Bavicha alikuwa analipwa mshahara sh 1.5 mil kila mwezi kinyume cha utaratibu.
Anadai wabunge wa viti maalumu ndio mtaji wa Mbowe pale CHADEMA.
Anadai yeye ndio mbunge bora wa jiji la Dsm, amejenga madaraja na hospitali pale Chanika na kwamba wakati wa mafuriko wapiga kura wake huja nyumbani kwake kupata hifadhi.
Kadhalika anadai ameondoka Chadema baada ya Mbowe na Dr Mahanga kumhakikishia kuwa hataitishwa kugombea tena 2020.
Mwita anadai mwaka 2008 alihama CCM na kwenda Chadema baada ya kugombana na aliyekuwa Katibu mkuu mzee Makamba na yule mwenyekiti wa UVCCM Dr Nchimbi.
Amesisitiza kuwa amejiuzulu ubunge muda huu baada ya kuona kuna fursa ya yeye kurudi tena bungeni katika uchaguzi mdogo kwa tiketi ya CCM hivyo hakuna atakachopoteza. Pia amedai yeye hakuutaka uenyekiti bali alitamani sana Mwenyekiti wa chama taifa awe Tundu Antipas Lissu.
Amemaliza kwa kusema ameshachukua fomu ya kugombea tena ubunge wa Ukonga na kwamba katika mazingira ya kisiasa akitokewa na baya lolote atamhisi Mbowe!
Source: Clouds tv!