Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,808
- 11,973
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA KWA UMMA
Leo jumamosi tarehe 04/09/2021 kulikuwa na kongamano la Katiba Mpya lililokuwa limeandaliwa na Bavicha Taifa katika Mkoa wa Mara wilaya ya Musoma mjini.
Juzi Mkuu wa Mkoa wa Mara akatangaza kuwa Leo itakuwa siku ya usafi Mkoa wa Mara na hivyo kila Mwananchi ambaye hatashiriki atapigwa faini ya shilingi elfu hamsini, Bavicha wakawatangazia wanachama na wananchi waje na vifaa vya usafi ili washiriki kufanya usafi na Mkuu wa Mkoa na baadaye wataendelea na kongamano Lao lililokuwa lifanyike katika ofisi ya Chama Wilaya.
Usiku wa saa Saba na nusu Jeshi la Polisi walivamia ofisi za Chama Wilaya na kuchukua mahema na Viti vilivyokuwa vimeandaliwa Kwa ajili ya kongamano hilo .
Leo Jumamosi asubuhi polisi wamezingira na kufunga Kwa kufuli lao Geti la kuingia ofisini na kuizingira ofisi , na hakuna dalili kuwa wanafanya usafi na badala yake wanawakamata wananchi ambao walikuwa tayari kushiriki zoezi la kufanya usafi.
Waliokamatwa mpaka sasa na Jeshi la Polisi Wilaya ya Musoma Mjini ni pamoja na;
(1). PATIRICK MWENGE NYABAGWE.
(2). GEORGE BURUMA RUBARE.
(3). NAHIMA MZURI KWAO SELEHIMAN.
(4). MAGRET EMANUEL.
(5). MUSILA JUMA.
Tunaendelea kufuatilia ukiukwaji na ukandamizaji wa Haki dhidi ya raia unaoendelea kufanywa na Jeshi la Polisi wakishirikina na vyombo vingine vya Dola .
Tunalaani na kukemea ukiukwaji na uvunjaji huu wa Katiba NA Sheria za Nchi unaoendelea kufanywa na kupandikiza mbegu za chuki ,ubaguzi,uhasama na mgawanyiko ndani ya jamii ya Watanzania Kwa misingi ya kiitikadi.
Tunaendelea kusisitiza kuwa ni Haki ya Watanzania kukusanyika na kujadiliana kuhusu Katiba Mpya na kufanya hivyo hakuna kipengele chochote cha Katiba au sheria kimevunjwa au kukiukwa ,isipokuwa wanaozuia ndio wanavunja Katiba na sheria za Nchi yetu.
Tunaendelea kuvitaka vyombo vya Dola kutimiza majukumu Yao Kwa weledi na kufuata sheria badala ya kutumia mabavu kupambana na wananchi ambao wanataka kujadiliana kuhusu Katiba ya Nchi Yao Kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.
Tunajiuliza Tume ya Haki za Binadamu na utawala Bora iko wapi ? Au haioni wala kusikia ukiukwaji huu wa Haki za Binadamu unaoendelea kutendeka nchini?
Imetolewa Leo Jumamosi tarehe 04 Septemba,2021.
John Mrema
Mkurugenzi wa Itifaki,, Mawasiliano na Mambo ya Nje.
TAARIFA KWA UMMA
Leo jumamosi tarehe 04/09/2021 kulikuwa na kongamano la Katiba Mpya lililokuwa limeandaliwa na Bavicha Taifa katika Mkoa wa Mara wilaya ya Musoma mjini.
Juzi Mkuu wa Mkoa wa Mara akatangaza kuwa Leo itakuwa siku ya usafi Mkoa wa Mara na hivyo kila Mwananchi ambaye hatashiriki atapigwa faini ya shilingi elfu hamsini, Bavicha wakawatangazia wanachama na wananchi waje na vifaa vya usafi ili washiriki kufanya usafi na Mkuu wa Mkoa na baadaye wataendelea na kongamano Lao lililokuwa lifanyike katika ofisi ya Chama Wilaya.
Usiku wa saa Saba na nusu Jeshi la Polisi walivamia ofisi za Chama Wilaya na kuchukua mahema na Viti vilivyokuwa vimeandaliwa Kwa ajili ya kongamano hilo .
Leo Jumamosi asubuhi polisi wamezingira na kufunga Kwa kufuli lao Geti la kuingia ofisini na kuizingira ofisi , na hakuna dalili kuwa wanafanya usafi na badala yake wanawakamata wananchi ambao walikuwa tayari kushiriki zoezi la kufanya usafi.
Waliokamatwa mpaka sasa na Jeshi la Polisi Wilaya ya Musoma Mjini ni pamoja na;
(1). PATIRICK MWENGE NYABAGWE.
(2). GEORGE BURUMA RUBARE.
(3). NAHIMA MZURI KWAO SELEHIMAN.
(4). MAGRET EMANUEL.
(5). MUSILA JUMA.
Tunaendelea kufuatilia ukiukwaji na ukandamizaji wa Haki dhidi ya raia unaoendelea kufanywa na Jeshi la Polisi wakishirikina na vyombo vingine vya Dola .
Tunalaani na kukemea ukiukwaji na uvunjaji huu wa Katiba NA Sheria za Nchi unaoendelea kufanywa na kupandikiza mbegu za chuki ,ubaguzi,uhasama na mgawanyiko ndani ya jamii ya Watanzania Kwa misingi ya kiitikadi.
Tunaendelea kusisitiza kuwa ni Haki ya Watanzania kukusanyika na kujadiliana kuhusu Katiba Mpya na kufanya hivyo hakuna kipengele chochote cha Katiba au sheria kimevunjwa au kukiukwa ,isipokuwa wanaozuia ndio wanavunja Katiba na sheria za Nchi yetu.
Tunaendelea kuvitaka vyombo vya Dola kutimiza majukumu Yao Kwa weledi na kufuata sheria badala ya kutumia mabavu kupambana na wananchi ambao wanataka kujadiliana kuhusu Katiba ya Nchi Yao Kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.
Tunajiuliza Tume ya Haki za Binadamu na utawala Bora iko wapi ? Au haioni wala kusikia ukiukwaji huu wa Haki za Binadamu unaoendelea kutendeka nchini?
Imetolewa Leo Jumamosi tarehe 04 Septemba,2021.
John Mrema
Mkurugenzi wa Itifaki,, Mawasiliano na Mambo ya Nje.