Mara: Mzazi ampiga mwalimu na kumjeruhi baada ya kumuadhibu mwanae

Kulikuwa mtoto mmoja wa kiume wa brother wangu mmoja. Alikuwa mtukutu sana. Kesi shuleni(primary) haziishi, kila wakati "uje na mzazi wako"
Akiitwa mzazi, alikuwa ananiomba niende. Baada ya majadiliano, nawaomba radhi sana Walimu wake.
Hitimisho inakuwa viboko sita vya makalioni kutoka kwa mzazi. Nakabidhiwa kiboko. Nilikuwa nacharaza bakora kisawasawa. Toto halitowi hata chozi.
Jioni tukikutana nyumbani, maneno yake:
"Daa! Baba mdogo anachapa fimbo kuliko hata Mwalimuu!!
Uzuri wa yule mtoto, kichwani alikuwa yuko vizuri.
Paaap! akafaulu darasa la saba, akapelekwa shule moja nzuri sana Mkoa wa Pwani. Ile karibia anamaliza form two, akamlamba mwenzie ngumi za uso, akafukuzwa shule.
Brother akawazaa, akaona ngoja amtafutie shule moja private ya watemi watupu, kwao makonzi ya kichwa ni kama kutafuna karanga.
Akaipata Tanga mjini. Dogo likapigana kitemitemi mpaka likamaliza form four.
Baba yake akawa ameishapoteza matumaini kabisa hata maendeleo yake hafatilii.
Siku ambayo sitakuja kuisahau ni siku ambayo Dogo anamkabidhi baba yake matokeo ya mitihani ya form four.
Brother alicheka, alicheka, mpaka akakaa chini!! Kulikoni?
Dogo limepaform, limepiga division one, point 16 yenye misonge miwili, Mathematics na Physics!!
Toka siku hiyo wakawa marafiki kama mtu na mdogo wake!
Ila dogo unaonekana una mastory sana, hheereh
 
Waalimu wasipobadilika watapigwa sana. Watu siyo ng'ombe wa kufundishwa kwa fimbo. Tanzania mtu anamaliza form ana miaka 18, mtu mzima. Anapigwa stiki. Yuko form six, ana miaka 20. Wenzake mtaani wameoa, yeye anachezea stiki.
Mambo ya ajabu sana.

Aliyebuni hizi fimbo sio binadamu wa kawaida. Atakuwa beberu au mkoloni tu.
 
Mpaka anatoa kwenye ATM ana 380k - 400k

Wa sekondari hawa diploma science wanakula 530k, hamna mwl wa primary wala secondary serikalini anaelipwa laki 8
Usilokijua ni kama usiku wa giza... Ebu uliza tena kwa waalimu ambao wana miaka 10 na zaidi kazini upate mrejesho

Sent from my G3121 using JamiiForums mobile app
 
UFAFANUZI WA ADHABU YA FIMBO.

Kwanza niwapongeze walimu wenzangu kwa shughuli tunayofanya ya ujenzi na uandaaji wa kada mbali mbali za kujenga taifa letu. Pia poleni kwa misuko suko ya mazingira yetu ya kazi pamoja na changamoto nyinginezo.
Nikiwa kama Mwalimu naelewa uchungu mnaopata mnapokumbana na hali ngumu mathalani mada yetu hapa.

Wazazi/walezi na watanzania kwa ujumla, kwanini Walimu tunatumia fimbo kama adhabu?

Kwanza muelewe, si shule zote Walimu wana chapa wanafunzi, kuna shule adhabu ya fimbo ni mwiko, na ufaulu wa wanafunzi upo imara tu, niwaambie tu Walimu hao ni matokeo ya mfumo wa walimu wale wale wanaotumia fimbo. Suala linalofanya approach kuwa tofauti ni mazingira ya ufanyaji kazi, huwezi kukuta shule yenye mazingira mazuri ya ufundishaji (well-established learning environment) walimu wakawa wanachapa, kuna shule zina wanafunzi wachache sana, pia matumizi ya fimbo ni madogo, kwanini? Kwa sababu adhabu yoyote inahitaji usimamizi, na ifike wakati muelewe kwamba adhabu lazima iwe na maumivu, ili mkosaji ajutie makosa yake, kama adhabu haimuumizi mkosaji hiyo siyo adhabu. Kama una kundi kubwa la wanafunzi wa kuhudumia, hutathubutu kutoa adhabu na kupoteza muda wa kusimamia wakati ambao una mikondo minne ya kufundisha, fimbo ni time saving punishment, mnamalizana yanaisha.

Pia, hakuna kitu waalimu tunaogopa kama adhabu za kisaikolojia, kumbuka neno ama adhabu ya UTENGWAJI inauma na inakaa kichwani kuliko maumivu ya fimbo, na hukaa miaka yote ya maisha ya mwanafunzi, unakumbuka mpaka leo maneno walimu waliokutamkia ila sio fimbo zao, mpka leo unaishia tu kusema ‘yule ticha anachapaa’ ila hujawahi kumfikiria kama mwalimu mbaya, hakuna mwalimu anayetaka ku impart adhabu ya kisaikolojia kwa mwanafunzi, ili anendelee kukaa akilini mwake mpaka atakapokuwa mkubwa.

Elimu ya Ualimu, inafundisha adhabu nyingi, ila walimu wengi wanatumia fimbo kama adhabu tulioona kuwa reliable, waalimu sio wanakada waliopewa mafunzo (trained) sisi ni wanakada tulioelimishwa (educated) hatungoji muongozo kutoka serikalini ni namna gani tuadhibu. Adhabu zifuatazo hazipendelewi na walimu, kwa sababu hukaa akilini kwa mwanafunzi au usimamizi wake unahitaji muda wa ziada zaidi.

1. Detention; kumfungia mwanafunzi kwenye darasa maalumu mithili ya jela ili kumtenga na wenzie na shughuli zote za shule (imagine)

2. Rejection; mfano, imagine wanafunzi wanakusanya madaftari halafu la mwanafunzi mkosaji husahihishi, au wakati wa kujibu maswali hata akinyoosha kidole peke yake humchagui.

3. Suspension; kumuondoa mwanafunzi shule ka kipindi fulani , wengi mnaifahamu

4. Time-out; kumfukuza mwanafunzi kwenye kipindi.

Kumbuka; adhabu zote hizi zinafanywa kwa kipindi fulani.

Kuna adhabu kama kazi za shule, jamani hizi ni mpaka shule ikihitaji huwezi kumpa adhabu mtoto achimbe shimo wakati shimo halihitajiki shuleni, apande maua wakati yapo, afagie wakati pasafi, huo ni uwendawazimu. Kumpa mtoto adhabu constructive kama kuandika essay, sas nyie hii adhabu inamkuta mtoto kipanga, unadhani ataumia? Na kwa taarifa yenu ni kwamba, kama huna cha kuandika, ni huna tuu kwa sababu mental ability has procrastinating peak.

Naomba mjue kama Walimu tuna kazi ngumu, msituchukie ati kwa sababu tumeadhibu watoto wenu, japo kisingizio chenu ni tunazidisha.

Mungu awabariki walimu wenzangu, kuufuta ujinga ni kazi ngumu kwa sababu ujinga wa watu wengi ndio utajiri wa wanye ufahamu kwa namna yoyote lazima tupigwe mawe.

Nawasilisha.
 
Mi nasema walimu wapigwe Tu tena wapigwe Sana wakikaidi wavunjwe hata miguu maana hawa ndo hutumika kuchakachua matokeo ya uchaguzi WA rais, wabunge, madiwani. Wapigwe Tu.
 
Usilokijua ni kama usiku wa giza... Ebu uliza tena kwa waalimu ambao wana miaka 10 na zaidi kazini upate mrejesho

Sent from my G3121 using JamiiForums mobile app
HuYO hajui kitu huyo tatizo jf KIla MTU msomi na mjuaji wapo walimu wanakula mil 1.5 mshahara WA mwl inategemea amekaa muda GANI kazini ndo unasikia kupandishwa daraja huo ndo mshahara hii kitu mwendazake ndo aliwazingua miaka yake yote.
 
Mwl wa shule ya serikali kumpiga mwanafunzi ni kijiongezea jukumu ambalo hauwezi kulipwa nimalize kusema angalizo hili lizingatiwe
 
Kama huna karama ya kufundisha nenda kalime! KUPIGA SIO KUFUNZA MNAWAUMIZIA WENZENU WATOTO TU.!!!
Nani alikufunza kuwa MIFIMBO HUFUNDISHA???? AU KUMFANYA MTOTO AELEWE???!
Sina karama ndio maana sifundishi tena ningekuwa mwalimu huyo mzazi angekuwa hospital.
Kama mtoto ni jeuri na kiazi asiadhibiwe?
Mwambie mwanao ulimwengu utamfundisha akileta ujeuri
 
Walimu ni tatizo kwa taifa hili..hasira zenu za mshahara mdogo msihamishie kwa watoto wetu..kwanza walimu wengi ni vilaza wengi wao option ya maish ilikua hiyo baada ya kukosa ufauru mzuri..unadhani watakua na idea gani zaidi kutumia akili kuchapa watoto.

#MaendeleoHayanaChama
 
Madogo wa skuizi bila stiki hawaendi na wana dharau sana tena baadhi wanataka hadi kupigana na waalimu wao!

Huyo mwanafunzi afukuzwe shule, mzazi nae sheria zimuadabishe. Sheria zipo zifatwe tu na zitumike ipasavyo kwa wote waliozikiuka.
Anakosa Gani sasa mwanafunzi..yeye kachapwa na Mwalimu!?
 
Inasikitisha sana...

Ila kabla ya kuhukumu inabidi story iwe balanced...
 
Nasoma comments; wengi inaonekana hamtaki adhabu ya fimbo, kwa taarifa yenu adhabu sio fimbo peke yake, na hakuna mwalimu anayetaka kushika mamiti haya, kujichosha tuu, muda unapita kuna siku zitaachwa tu, zinachosha
 
Walimu ni tatizo kwa taifa hili..hasira zenu za mshahara mdogo msihamishie kwa watoto wetu..kwanza walimu wengi ni vilaza wengi wao option ya maish ilikua hiyo baada ya kukosa ufauru mzuri..unadhani watakua na idea gani zaidi kutumia akili kuchapa watoto.

#MaendeleoHayanaChama

aisee
 
Back
Top Bottom