Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,007
- 9,873
Mwananchi mmoja aliyejulikana kwa jina la Nyimano Ghati mkazi wa kata ya Nkende Halmashauri ya mji wa Tarime Mkoani Mara amedaiwa kumpiga na kumjeruhi mwalimu wa shule ya msingi Nkende Mwl. Edina John kwa madai ya kuwa mtoto wake anayesoma shule hiyo alipewa adhabu na mwalimu.
Kufuatia tukio la mwalimu wa shule ya msingi Nkende kupigwa na mzazi, viongozi wa kamati ya shule hiyo wameitisha kikao cha dharula ili kuzungumzia tukio hilo ambapo diwani wa kata Nkende, Daniel Komote amelaani kitendo hicho na kuwaomba walimu waendelee kufanya kazi kwa ufanisi.
Kufuatia tukio la mwalimu wa shule ya msingi Nkende kupigwa na mzazi, viongozi wa kamati ya shule hiyo wameitisha kikao cha dharula ili kuzungumzia tukio hilo ambapo diwani wa kata Nkende, Daniel Komote amelaani kitendo hicho na kuwaomba walimu waendelee kufanya kazi kwa ufanisi.