Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,000
- 9,861
Polisi Wilaya ya Serengeti wanamshikilia Changwa Sebeki (19) mkazi wa Kijiji cha Merenga kwa tuhuma za mauaji ya Kegoka Mwikwabe (22) anayedaiwa alimuondoa kwenye harusi kwa kukosa zawadi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Danilel Shillah leo Jumapili Novemba mosi ameliambia Mwananchi kwa njia ya simu kuwa tukio hilo limetokea jana Oktoba 31 majira ya saa 1.30 jioni kijijini hapo.
"Mtuhumiwa alimkatakata kwa panga na kusababisha kifo chake. Sababu ni kuwa katika harusi moja, marehemu alikuwa anasimamia vijana (wanaocheza na binti) kutoa zawadi lakini mtuhumiwa alicheza (na binti) na alipoambiwa atoe zawadi (kama ilivyo kwa taratibu za Kikurya), hakuweza kutoa hivyo akatolewa nje.
“Kutokanana kitendo hicho (kilichofanyika mwaka jana), mtuhumiwa huyo aliweka kisasi moyoni na alipokutana jana na aliyemtoa harusini akaamua kumkata.
Kamanda Shillah amesema wanatarajia kumfikisha mtuhumiwa mahakamani kwa kosa alilotenda na amewataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Danilel Shillah leo Jumapili Novemba mosi ameliambia Mwananchi kwa njia ya simu kuwa tukio hilo limetokea jana Oktoba 31 majira ya saa 1.30 jioni kijijini hapo.
"Mtuhumiwa alimkatakata kwa panga na kusababisha kifo chake. Sababu ni kuwa katika harusi moja, marehemu alikuwa anasimamia vijana (wanaocheza na binti) kutoa zawadi lakini mtuhumiwa alicheza (na binti) na alipoambiwa atoe zawadi (kama ilivyo kwa taratibu za Kikurya), hakuweza kutoa hivyo akatolewa nje.
“Kutokanana kitendo hicho (kilichofanyika mwaka jana), mtuhumiwa huyo aliweka kisasi moyoni na alipokutana jana na aliyemtoa harusini akaamua kumkata.
Kamanda Shillah amesema wanatarajia kumfikisha mtuhumiwa mahakamani kwa kosa alilotenda na amewataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi.