Mapungufu makubwa ya Taifa Stars katika mechi ya jana dhidi ya Lesotho

kasenene

JF-Expert Member
Jun 6, 2008
1,632
2,413
Wadau,
Jana nimeangalia mechi ya Taifa Stars na Lesotho na yafuatayo ndio niliyoyaona mimi kama mfuatiliaji soka wa mda mrefu.

1. Team haina ushirikiano yaani kila mchezaji anacheza kadiri anavyojua yeye hii ikapelekea kabisa kuonyesha jinsi baadhi ya wachezaji kama Samatta walivyotofauti kabisa na wachezaji wanaocheza ligi za ndani kwa mambo mengi kama jinsi ya kumiliki mpira, kutoa pasi e.t.c

2. Wachezaji kutokujua majukumu yao wanapokuwa uwanjani mfano Kichuya tofauti na kupiga kona sikujua jukumu lake uwanjani lilikuwa ni nini hakuonekana kabisa na wala mwalimu hakulitambua hilo

3. Wachezaji kuwa na papara wakati wakupokea mpira, wakati wa kutoa pasi na kadiri wanavyozidi kulisogelea lango la wapinzani (hili limekuwa tatizo la muda kidogo kwa timu nyingi za kiafrica, hili tatizo lilipungua saana kipindi cha Maximo naona sasa limerudi)

4. Japo pumzi wanayo lakini stamina ni tatizo jambo linalopelekea wachezaji wengi kuanguka anguka bila kuguswa

5. Mwalimu kufanya mabadilikio yasiyokuwa na tija. Sijui alilenga kufanya nini

6. Mwisho vijana vipaji wanavyo wanachotakiwa kupata ni mwelekezi sahihi. Yaani inatia hasira karibia kutoa machozi inapoonekana vipaji kama vile vinapotea kwa kutokuwa na waelekezi weledi(angalia Samatta anavyocheza kwa msisitizo)
 
Unetuwekea matokeo ya mpira wa jana.
Matokeo ilikuwa ni suluhu ya 1-1 huku Tz wakitangulia kufunga goli kupitia Samatta kwa free kick "safi" na Lesotho wakasawazisha kwa uzembe wa beki zetu.Magoli yote yalifungwa kipindi cha kwanza. SUPER SPORT 233 WALIONYESHA WANAWEZA RUDIA LEO
 
MTU kama Maximo alitakiwa akae na timu muda mrefu. Sasa bongo siasa tu. Toka afukuzwe sijaona kinachofanyika.
 
Nimemsikia leo Mwalimu akieleza sababu za kufungwa...kwa upuuzi aloongea leo ningekuwa Rais wa TFF ningemtimua right away after the press conference...Mungu wangu hivi sisi tukoje?
 
Sisi tunaweza mashindano ya ngono na kulewa
Umenikumbusha miaka hiyo UDSM! Komba's family: Mmoja alikuwa bingwa wa pombe Mabibo Hostel afu ndg yk bingwa wa Sigara! Mmoja lawyer na mwingine engineer
 
MTU kama Maximo alitakiwa akae na timu muda mrefu. Sasa bongo siasa tu. Toka afukuzwe sijaona kinachofanyika.

Mambo ya Maximo waulize yanga! Aliwaleteaga matapeli wa Sao Paulo pale jangwani hawataki hata kumsikia sasa hivi
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom