Mapungufu katika Wimbo wa Taifa la Tanzania

October

JF-Expert Member
Oct 5, 2009
2,145
92
Nimekua nikitafakari Wimbo wetu wa taifa nikabaini kua una mapungufu kadhaa ambayo aidha yangetakiwa yarekebishwe au kutafuta wimbo mbadala.

Kwanza wimbo huu si wimbo wenye asili ya Tanzania ni wimbo tulioiga kutoka Afrika Kusini. Nionavyo mimi hii si dalili nzuri kuiga wimbo wa taifa na kutumia wimbo ambao hauna asili ya nchi unayoiwakilisha. Sidhani kama Tanzania tumekosa ubunifu kiasi cha kuiga wimbo wa nchi nyingine. Kuna sababu gani ya msingi kungiwa wimbo na wazulu?

Pili naona kwamba wimbo wetu haumjali mtanzania na wala haumpi kipaumbele hata kidogo, Hii inadhihirishwa na ukweli kwamba mambo baraka kwa mtanzania zimetajwa katika beti la pili, badala ya kuwa Beti la kwanza. Hii ni aibu na laana kwa watanzania. Tunajilaani wenyewe kwa kuwajali wageni kuliko sisi watanzania. Bahati mbaya hali hii imekua kama self fulfilling prophecy, ndio maana wageni wanatetemekewa na wenyeji wanaonekana mafala ndani ya nchi yao.

Huu wimbo umepitwa na wakati, Unazungumzia kudumisha uhuru wakati hakuna nchi inyotawaliwa sasa hivi. Ilikua sawa wakati wa kupigania uhuru na kipindi cha ujamaa kuwa na wimbo kama huu lakini sasa mambo yamebadilika, nchi zote zimejikomboa, wale tuliojipendekeza kuwasaidia kupigania uhuru wameshapata uhuru wao, hawatujali wala kututhamini na huku sisi tunaendeleza wimbo wa enzi hizo.

Vilevile naona wimbo huu haumjengei mtanzania mapenzi na nchi yake, haumfanyi mtu kuwa proud na nchi yake. Hakuna kitu chochote kinachozungumzia uzuri wa nchi yetu wala uzuri wa watanzania au ushujaa wa watanzania….hakuna.

Naomba tuendeleze mapungufu ya wimbo huu...

Napendekeza wimbo wa ‘Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote….' ukifanyiwa marekebisho kidogo ungefaa zaidi
 
Maoni yako yana mvuto lakini siyo sahihi kwa sababu kadhaa.

(1) kwamba wimbo ulitungwa na mtu ambaye siyo mtanzania siyo sababu ya msingi ya kuubatilisha kama wimbo wa Taifa. Kuna nchi nyingi sana ambazo nyimbo zake za Taifa zilitungwa na raia wa nchi nyingine ambao hata hawakuwahi kukaa katika nchi zile; kwa mfano.
(a): Panama: ulitungwa na raia wa spain.
(c): Chile: ulitungwa na raia wa spain.
(b): Spain: ulitungwa na raia wa ujerumani.
(c): Uingereza: ulitungwa na raia wa ufaransa.

(2) Wimbo ule una beti mbili, beti ya kwanza inazungumzia Afrika ambayo Tanzania ni sehemu yake, na beti ya pila inazungumzia Tanzania specifically; kwa hiyo Tanzania inazungumzwa katika beti zote mbili ingawa mara nyingi ni ubeti wa pili tu unaotumika katiak functions nyingi.

Sijui wewe unaashiria nini kusema kuwa Tanzania imeongelewa katika ubeti wa pili tu kwa vila una maana ya kuse sisi siyo sehemu ya Afrika. Nyimbo za nchi nyingi sana zinaongelea humanity zaidi kuliko utaifa na wala hata hazitaji jina la nchi yao, kwa mfano wimbo wa taifa wa USA hautaji chochote kuhusu nchi ya USA, nimepata kopi rilycs zake kutoka wikipedia ni hiz hapa:
Code:
O! say can you see by the dawn's early light
What so proudly we hailed at the twilight's last gleaming?
Whose broad stripes and bright stars through the perilous fight,
O'er the ramparts we watched were so gallantly streaming?
And the rockets' red glare, the bombs bursting in air,
Gave proof through the night that our flag was still there.
O! say does that star-spangled banner yet wave
O'er the land of the free and the home of the brave?

On the shore, dimly seen through the mists of the deep,
Where the foe's haughty host in dread silence reposes,
What is that which the breeze, o'er the towering steep,
As it fitfully blows, half conceals, half discloses?
Now it catches the gleam of the morning's first beam,
In full glory reflected now shines in the stream:
'Tis the star-spangled banner! Oh long may it wave
O'er the land of the free and the home of the brave.

And where is that band who so vauntingly swore
That the havoc of war and the battle's confusion,
A home and a country should leave us no more!
Their blood has washed out their foul footsteps' pollution.
No refuge could save the hireling and slave
From the terror of flight, or the gloom of the grave:
And the star-spangled banner in triumph doth wave
O'er the land of the free and the home of the brave.

O! thus be it ever, when freemen shall stand
Between their loved home and the war's desolation!
Blest with victory and peace, may the heav'n rescued land
Praise the Power that hath made and preserved us a nation.
Then conquer we must, when our cause it is just,
And this be our motto: 'In God is our trust.'
And the star-spangled banner in triumph shall wave
O'er the land of the free and the home of the brave!
(3) Neno uhuru limetukia katika wimbo ule kwa maana pana zaidi ya hiyo unayodhani ya kukwepa ukoloni. Nina imani kuwa hadi leo hii umshasikiwa watu wanalalamika kukosa uhuru ndani ya nchi yao. Ukienda kwenye mbuga za Loliondo, utajikuta kuwa huna uhuru wa kufanya ambayo ungefanya kabla ya kuingia pale hata kama hujavunja sheria yoyote ya nchi. uhuru huyo ndio unaoongelewa katika wimbo wetu. I love the song:
[ame]http://www.youtube.com/watch?v=tTaz2Dn4IFw[/ame]

(4) Pendekezo lako la kutumia wimbo wa "Tanzania Tanzania nakupenda..." ni zuri, lakini vile ukubali kuwa pendekezo hili linaweza kusikikilizwa tu kama wewe una uhuru wa kutoa mapendekezo.
 
Huo wimbo hasa baada ya kukaa nje ya Tanzania unaniudhi sana, kwa sababu unataja na kusifia Africa wakati wenzetu wengi wa Afrika wala huwa hawakumbuki nchi nyingine za Afrika. Ukombozi uliisha sasa ni kuubadili na kusema yetu ya Tanzania full stop.

Mambo mengine ni ya kurekebisha hapa na pale. Tunapenda uafrika lakini Afrika hawatupendi kwa hiyo tujipende wenyewe.
 
Nimekua nikitafakari Wimbo wetu wa taifa nikabaini kua una mapungufu kadhaa ambayo aidha yangetakiwa yarekebishwe au kutafuta wimbo mbadala.


Kwanza wimbo huu si wimbo wenye asili ya Tanzania ni wimbo tulioiga kutoka Afrika Kusini. Nionavyo mimi hii si dalili nzuri kuiga wimbo wa taifa na kutumia wimbo ambao hauna asili ya nchi unayoiwakilisha. Sidhani kama Tanzania tumekosa ubunifu kiasi cha kuiga wimbo wa nchi nyingine. Kuna sababu gani ya msingi kungiwa wimbo na wazulu?

Pili naona kwamba wimbo wetu haumjali mtanzania na wala haumpi kipaumbele hata kidogo, Hii inadhihirishwa na ukweli kwamba mambo baraka kwa mtanzania zimetajwa katika beti la pili, badala ya kuwa Beti la kwanza. Hii ni aibu na laana kwa watanzania. Tunajilaani wenyewe kwa kuwajali wageni kuliko sisi watanzania. Bahati mbaya hali hii imekua kama self fulfilling prophecy, ndio maana wageni wanatetemekewa na wenyeji wanaonekana mafala ndani ya nchi yao.

Huu wimbo umepitwa na wakati, Unazungumzia kudumisha uhuru wakati hakuna nchi inyotawaliwa sasa hivi. Ilikua sawa wakati wa kupigania uhuru na kipindi cha ujamaa kuwa na wimbo kama huu lakini sasa mambo yamebadilika, nchi zote zimejikomboa, wale tuliojipendekeza kuwasaidia kupigania uhuru wameshapata uhuru wao, hawatujali wala kututhamini na huku sisi tunaendeleza wimbo wa enzi hizo.

Vilevile naona wimbo huu haumjengei mtanzania mapenzi na nchi yake, haumfanyi mtu kuwa proud na nchi yake. Hakuna kitu chochote kinachozungumzia uzuri wa nchi yetu wala uzuri wa watanzania au ushujaa wa watanzania….hakuna.
.
naomba tuendeleze mapungufu ya wimbo huu
.
.
Napendekeza wimbo wa ‘Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote….’ ukifanyiwa marekebisho kidogo ungefaa zaidi


Mkuu, nimekuvulia kofia. Mada yako ni tamu kama asali.
 
Tanzania is not in isolation. Tanzania is part of Africa and at the time that song was composed Tanzania was in the depth of the liberation struggle. We cannot divorce ourselves from an ideal of Africa. We are part of it and we pay tribute to it by putting it in the first verse of our national anthem. We should be proud of that.
 
Tanzania is not in isolation. Tanzania is part of Africa and at the time that song was composed Tanzania was in the depth of the liberation struggle. We cannot divorce ourselves from an ideal of Africa. We are part of it and we pay tribute to it by putting it in the first verse of our national anthem. We should be proud of that.

Well said;

Nyimbo za mataifa mengi zina maudhui yanayochanganya historia na malengo ya taifa lile kwa watu wake. Wimbo huu nao una maudhui hayo hayo; sioni ubaya au upungufu wake kabisa.
 
****************. mwimbo huu utadumu miaka mia kenda maana hauna muda. Dumisha uhuru maana yake sio kutafuuta uhuru. akili zako zinadhani uhuru ni dhdi ya mkoloni tu. Ulivyo huna akili unaamini katika mipaka ya kikoloni iliyoundwa hivi vinchi. Afrika ni moja, afrika must unite.
Hata kama ni uhuru wa mawazo, haya hayana maana. una question wimbo wa taaifa kwa hoja dhaifu namna hii? Eti wa wazulu, unaimbwa kizulu? sasa tanzaia ulitaka uwe wa? maana ukiwa wa kisukuma, wahaya watagoma, ukiwa wa kichaga wanyakyusa watagoma....... mawazo yako finyu hayaoni hii busara waliyotumia wazee?
 
October:

Ule wimbo hauna matatizo yoyote yale. Kuna nchi zina nyimbo za taifa zinazomsifia Malkia au Mfalme na bado nchi hizo zina uzalendo.

Kwa mfano UK, wana msifia Malkia. Na kwa kusikiliza wimbo huo walikuwa tayari kwenda nje kupiga vita, kutafuta makoloni kwa maslahi ya taifa lao. Ngoja nikopi huo wimbo na tuone kama wimbo wa Tanzania una mapungufu yoyote.

God save our gracious Queen,
Long live our noble Queen,
God save the Queen:
Send her victorious,
Happy and glorious,
Long to reign over us:
God save the Queen.
O Lord, our God, arise,
Scatter her enemies,
And make them fall.
Confound their politics,
Frustrate their knavish tricks,
On Thee our hopes we fix,
God save us all.
Thy choicest gifts in store,
On her be pleased to pour;
Long may she reign:
May she defend our laws,
And ever give us cause
To sing with heart and voice
God save the Queen.

Kuna matatizo yanayofanya watanzania kuwa na mashaka na uzalendo wao. Mojawapo ni USHINDI. Watanzania wanahitaji ushindi: uwe wa michezo, maarifa, njaa, vita au kitu chochote kitakachopandisha morale ya wananchi kuwa juu.

Waulize wakina Kichuguu, Jasusi, FMES walivyojisikia na wimbo wao pale Filbet Bayi au Nyambui alipokuwa anavalishwa medani na wimbo wa taifa kupingwa.
 
I always like this song, makes me to love my motherland,

sing with me;

Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote
Nchi yangu Tanzania
Jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuota wewe
Niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote

wimbo wa taifa hauoni ndani hapa!!

muanzisha thread, ukiweka kongamano la watanzania watunge wimbo wa taifa leo hii, bado utakuwa na mapungufu tu,somethings just happens and live!
 
hii thread ya kijinga na aliyeileta ni mjnga na anatapika tu humu. mwimbo huu utadumu miaka mia kenda maana hauna muda. Dumisha uhuru maana yake sio kutafuuta uhuru. akili zako zinadhani uhuru ni dhdi ya mkoloni tu. Ulivyo huna akili unaamini katika mipaka ya kikoloni iliyoundwa hivi vinchi. Afrika ni moja, afrika must unite.
Hata kama ni uhuru wa mawazo, haya hayana maana. una question wimbo wa taaifa kwa hoja dhaifu namna hii? Eti wa wazulu, unaimbwa kizulu? sasa tanzaia ulitaka uwe wa? maana ukiwa wa kisukuma, wahaya watagoma, ukiwa wa kichaga wanyakyusa watagoma....... mawazo yako finyu hayaoni hii busara waliyotumia wazee?

mpwa,
najua una roho ya uzalendo na machungu haswa na taifa letu la Tanzania.
Naomba kidogo upunguze munkari ili tuidumishe amani yetu.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Jamii Forums na watu wake especially Bigilankana
 
Maoni yako yana mvuto lakini siyo sahihi kwa sababu kadhaa.

(1) kwamba wimbo ulitungwa na mtu ambaye siyo mtanzania siyo sababu ya msingi ya kuubatilisha kama wimbo wa Taifa. Kuna nchi nyingi sana ambazo nyimbo zake za Taifa zilitungwa na raia wa nchi nyingine ambao hata hawakuwahi kukaa katika nchi zile; kwa mfano.
(a): Panama: ulitungwa na raia wa spain.
(c): Chile: ulitungwa na raia wa spain.
(b): Spain: ulitungwa na raia wa ujerumani.
(c): Uingereza: ulitungwa na raia wa ufaransa.

(2) Wimbo ule una beti mbili, beti ya kwanza inazungumzia Afrika ambayo Tanzania ni sehemu yake, na beti ya pila inazungumzia Tanzania specifically; kwa hiyo Tanzania inazungumzwa katika beti zote mbili ingawa mara nyingi ni ubeti wa pili tu unaotumika katiak functions nyingi.

Sijui wewe unaashiria nini kusema kuwa Tanzania imeongelewa katika ubeti wa pili tu kwa vila una maana ya kuse sisi siyo sehemu ya Afrika. Nyimbo za nchi nyingi sana zinaongelea humanity zaidi kuliko utaifa na wala hata hazitaji jina la nchi yao, kwa mfano wimbo wa taifa wa USA hautaji chochote kuhusu nchi ya USA, nimepata kopi rilycs zake kutoka wikipedia ni hiz hapa:

http://www.youtube.com/watch?v=tTaz2Dn4IFw

(4) Pendekezo lako la kutumia wimbo wa "Tanzania Tanzania nakupenda..." ni zuri, lakini vile ukubali kuwa pendekezo hili linaweza kusikikilizwa tu kama wewe una uhuru wa kutoa mapendekezo.

Asante Mkuu kwa mchango wako uliotukuka.

Nimelikiziza hii clip Youtube Clip na nimesikia beti moja tu katika wimbo huu,

Sasa naomba kuuliza, Beti hili ni lile la kwanza linalozongumzia Viongozi na Afrika Peke yake au ni lile la pili linalozungumzia Tanzani, Uhuru na Umoja?

Kama ni beti la kwanza, huoni kwamba unatukuza Afrika kuliko Tanzania? Kipi kinakuja kwanza katika list ya priorities, Afrika kwanza au Tanzania kwanza?
 
hii thread ya kijinga na aliyeileta ni mjnga na anatapika tu humu. mwimbo huu utadumu miaka mia kenda maana hauna muda. Dumisha uhuru maana yake sio kutafuuta uhuru. akili zako zinadhani uhuru ni dhdi ya mkoloni tu. Ulivyo huna akili unaamini katika mipaka ya kikoloni iliyoundwa hivi vinchi. Afrika ni moja, afrika must unite.
Hata kama ni uhuru wa mawazo, haya hayana maana. una question wimbo wa taaifa kwa hoja dhaifu namna hii? Eti wa wazulu, unaimbwa kizulu? sasa tanzaia ulitaka uwe wa? maana ukiwa wa kisukuma, wahaya watagoma, ukiwa wa kichaga wanyakyusa watagoma....... mawazo yako finyu hayaoni hii busara waliyotumia wazee?

This language is not good! mbona muanzisha thread ameweka hoja zake, kirafiki bila matusi yoyotem. kwa nini watu wengine mnapenda kujiona mko bora sana juu ya wengine?

ukiona haikufai nenda thread zingine! ulichofanya hapa mkuu ni makosa na hii haipendezi kabisa kwenye forums zenye watu wa kila aina!

umeanzisha thread gani ya akili tuichangie??

mimi mwenyewe nimechangia kuwa haitawezekana kubadilisha kwa hali ya sasa,lakini sijatumia matusi, kwa ufahamu wake point alizoweka ni nzuri, mjibu kwa upendo, we are Tanzania na wimbo wa taifa unasema dumisha umoja na amani! unayeuabudu huo wimbo hautaki kudumisha umoja na amani ndani ya JF!!!
 
hii thread ya kijinga na aliyeileta ni mjnga na anatapika tu humu. mwimbo huu utadumu miaka mia kenda maana hauna muda. Dumisha uhuru maana yake sio kutafuuta uhuru. akili zako zinadhani uhuru ni dhdi ya mkoloni tu. Ulivyo huna akili unaamini katika mipaka ya kikoloni iliyoundwa hivi vinchi. Afrika ni moja, afrika must unite.
Hata kama ni uhuru wa mawazo, haya hayana maana. una question wimbo wa taaifa kwa hoja dhaifu namna hii? Eti wa wazulu, unaimbwa kizulu? sasa tanzaia ulitaka uwe wa? maana ukiwa wa kisukuma, wahaya watagoma, ukiwa wa kichaga wanyakyusa watagoma....... mawazo yako finyu hayaoni hii busara waliyotumia wazee?

Asante kwa maoni yako yaliyotukuka ila punguza jazba kaka, hii ni discussion tu yenye lengo la kupata maoni ya watu.
 
Kwanza wimbo huu si wimbo wenye asili ya Tanzania ni wimbo tulioiga kutoka Afrika Kusini. Nionavyo mimi hii si dalili nzuri kuiga wimbo wa taifa na kutumia wimbo ambao hauna asili ya nchi unayoiwakilisha. Sidhani kama Tanzania tumekosa ubunifu kiasi cha kuiga wimbo wa nchi nyingine. Kuna sababu gani ya msingi kungiwa wimbo na wazulu?

Ni kweli,lakini huu wimbo haufanani ONE-TO-ONE na wa sauzi,kilichozingatiwa katika ku-match na beats za sauzi ni nature ya ujumbe uliopo.so far HAKUNA UBAYA KATIKA KUKOPI TECHNOLOJI.lakini ikumbukwe kwamba kuna so many criterias zilizingatiwa wakati wanauedit wimbo huu

Pili naona kwamba wimbo wetu haumjali mtanzania na wala haumpi kipaumbele hata kidogo, Hii inadhihirishwa na ukweli kwamba mambo baraka kwa mtanzania zimetajwa katika beti la pili, badala ya kuwa Beti la kwanza. Hii ni aibu na laana kwa watanzania. Tunajilaani wenyewe kwa kuwajali wageni kuliko sisi watanzania. Bahati mbaya hali hii imekua kama self fulfilling prophecy, ndio maana wageni wanatetemekewa na wenyeji wanaonekana mafala ndani ya nchi yao.
hapa umechemsha.
kwenye hizo three bolded statements HAKUNA LINK YA MOJA KWA MOJA itakayofanya hizo sentensi tatu zitegemeane.i mean hatuwezi kusema kwamba kuanza na mungu ibariki tanzania kutafanyamsiwajali WAHINDI,au kutawafanya MSIWATETEMEKEE WAKINA R.A!NEVER ON EARTH!kuna so many reasons to account for the worst situation


Huu wimbo umepitwa na wakati, Unazungumzia kudumisha uhuru wakati hakuna nchi inyotawaliwa sasa hivi. Ilikua sawa wakati wa kupigania uhuru na kipindi cha ujamaa kuwa na wimbo kama huu lakini sasa mambo yamebadilika, nchi zote zimejikomboa, wale tuliojipendekeza kuwasaidia kupigania uhuru wameshapata uhuru wao, hawatujali wala kututhamini na huku sisi tunaendeleza wimbo wa enzi hizo.
hapa napo umejichanganya sana mkuu wangu!sio sahihi kwamba WITH TIME NA ADVANCEMENTS OF SCIENCE AND TECHNOLOGY TUKAWA TUNABADILISHA WIMBO WA TAIFA.MATAIFA YALIYOENDELEA bado yana nyimbo zile zil;e na wanakumbbuka siku walizopata uhuru!THIS IS FAKE BWANA


Vilevile naona wimbo huu haumjengei mtanzania mapenzi na nchi yake, haumfanyi mtu kuwa proud na nchi yake. Hakuna kitu chochote kinachozungumzia uzuri wa nchi yetu wala uzuri wa watanzania au ushujaa wa watanzania….hakuna.

kuwa na mapenzi na nchi yako hakujengwi na wimbo!I MEAN WATU WALIOPO ULAYA NA MAREKANI NA TAALUMA ZAO hawazikimbii nchi hizi kwa dhana ya wimbo,ni umaskini wao tu.

wimbo wa taifa unajitosheleza na umebeba content STAHILI!HAUNA MAPUNGUFU!...

kuhusu kuzielezea adventures za nchi hii ndio maana tunazo nyimbo kama tanzania tanzania AMBAZO NI TOO COMMERCIAL...

unajua nini wazee,
tufikie mahala tuwe wakweli...!tuache negative attitudes na taifa letu (HATA KAMA HAMUISHI HUKU)
 


Kwanza wimbo huu si wimbo wenye asili ya Tanzania ni wimbo tulioiga kutoka Afrika Kusini. Nionavyo mimi hii si dalili nzuri kuiga wimbo wa taifa na kutumia wimbo ambao hauna asili ya nchi unayoiwakilisha. Sidhani kama Tanzania tumekosa ubunifu kiasi cha kuiga wimbo wa nchi nyingine. Kuna sababu gani ya msingi kungiwa wimbo na wazulu?

Wimbo wa Taifa letu umetokana na wimbo unaotumiwa na Afrika Union (kabla ikiitwa OAU). Kuna Africa Union Anthem ambayo ina tune kama za wimbo wetu wa Taifa. Kabla ya Afrika Kusini kujikwamua kutoka kwenye ubaguzi wa rangi (Apartheid), walikuwa wakitumia wimbo mwingine ambao ni tofauti kabisa na huu wa sasa, uliitwa "Die Stem". Ila wimbo unaofanana na wetu ulikuwa ukitumiwa na chama cha ANC cha Afrika Kusini, na haukuwa wimbo wa Taifa, japokuwa ulitungwa na Mwafika Kusini miaka mingi iliyopita.

Napendekeza wimbo wa ‘Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote….’ ukifanyiwa marekebisho kidogo ungefaa zaidi
Ni kweli kuwa wimbo ulioutaja hapo juu ni mzuri sana. Ni wimbo unaosisimua na unaweza kuongeza uzalendo kama utatumika mara kwa mara. Katika kipindi cha uongozi wa Hayati Baba wa Taifa na hata kipindi cha Mkapa, wimbo huo ulikuwa ukiimbwa sana kwenye hafla mbalimbali za kitaifa baada ya kuimbwa wimbo wa Taifa.

Ila kwa mtazamo wangu sioni kuwa unajitosheleza sana kama ulivyo na kukidhi kuwa wimbo wa Taifa (kama ulivyobainisha). Marekebisho yanayotakiwa ni pamoja na kuupa nguvu zaidi inayohitajika ili kuonyesha historia ya Taifa letu. Mabadiliko hayo inabidi yafanywe kwa makini, maana yanaweza kuharibu ladha ya wimbo wenyewe kama yakifanywa holela.
 
Ni kweli,lakini huu wimbo haufanani ONE-TO-ONE na wa sauzi,kilichozingatiwa katika ku-match na beats za sauzi ni nature ya ujumbe uliopo.so far HAKUNA UBAYA KATIKA KUKOPI TECHNOLOJI.lakini ikumbukwe kwamba kuna so many criterias zilizingatiwa wakati wanauedit wimbo huu


hapa umechemsha.
kwenye hizo three bolded statements HAKUNA LINK YA MOJA KWA MOJA itakayofanya hizo sentensi tatu zitegemeane.i mean hatuwezi kusema kwamba kuanza na mungu ibariki tanzania kutafanyamsiwajali WAHINDI,au kutawafanya MSIWATETEMEKEE WAKINA R.A!NEVER ON EARTH!kuna so many reasons to account for the worst situation



hapa napo umejichanganya sana mkuu wangu!sio sahihi kwamba WITH TIME NA ADVANCEMENTS OF SCIENCE AND TECHNOLOGY TUKAWA TUNABADILISHA WIMBO WA TAIFA.MATAIFA YALIYOENDELEA bado yana nyimbo zile zil;e na wanakumbbuka siku walizopata uhuru!THIS IS FAKE BWANA




kuwa na mapenzi na nchi yako hakujengwi na wimbo!I MEAN WATU WALIOPO ULAYA NA MAREKANI NA TAALUMA ZAO hawazikimbii nchi hizi kwa dhana ya wimbo,ni umaskini wao tu.

wimbo wa taifa unajitosheleza na umebeba content STAHILI!HAUNA MAPUNGUFU!...

kuhusu kuzielezea adventures za nchi hii ndio maana tunazo nyimbo kama tanzania tanzania AMBAZO NI TOO COMMERCIAL...

unajua nini wazee,
tufikie mahala tuwe wakweli...!tuache negative attitudes na taifa letu (HATA KAMA HAMUISHI HUKU)

Mkuu, sio dhambi kubadili wimbo wa Taifa, kama Taifa litaona inafaa. Mabadiliko mengi hufanywa kadiri muda unapohitaji. Kwa mfano, mabadiliko ya Katiba, Bendera za nchi n.k.

Zipo nchi ambazo zimewahi kubadili nyimbo zao za Taifa. Mfano ni Afrika ya kusini na Zimbabwe. Ukitafuta taarifa zaidi utaweza kugundua kuwa zipo nchi nyingine nyingi ambazo zimewahi kufanya mabadiliko ya nyimbo zao za Taifa pia.

Kinachohotajika ni sababu tu za kufanya mabadiliko hayo. Lazima tukubali kubadilika, kurekebisha na kuboresha kila inapobidi.
 
Wimbo wa Taifa letu umetokana na wimbo unaotumiwa na Afrika Union (kabla ikiitwa OAU). Kuna Africa Union Anthem ambayo ina tune kama za wimbo wetu wa Taifa. Kabla ya Afrika Kusini kujikwamua kutoka kwenye ubaguzi wa rangi (Apartheid), walikuwa wakitumia wimbo mwingine ambao ni tofauti kabisa na huu wa sasa, uliitwa "Die Stem". Ila wimbo unaofanana na wetu ulikuwa ukitumiwa na chama cha ANC cha Afrika Kusini, na haukuwa wimbo wa Taifa, japokuwa ulitungwa na Mwafika Kusini miaka mingi iliyopita.


Ni kweli kuwa wimbo ulioutaja hapo juu ni mzuri sana. Ni wimbo unaosisimua na unaweza kuongeza uzalendo kama utatumika mara kwa mara. Katika kipindi cha uongozi wa Hayati Baba wa Taifa na hata kipindi cha Mkapa, wimbo huo ulikuwa ukiimbwa sana kwenye hafla mbalimbali za kitaifa baada ya kuimbwa wimbo wa Taifa.

Ila kwa mtazamo wangu sioni kuwa unajitosheleza sana kama ulivyo na kukidhi kuwa wimbo wa Taifa (kama ulivyobainisha). Marekebisho yanayotakiwa ni pamoja na kuupa nguvu zaidi inayohitajika ili kuonyesha historia ya Taifa letu. Mabadiliko hayo inabidi yafanywe kwa makini, maana yanaweza kuharibu ladha ya wimbo wenyewe kama yakifanywa holela.

Wadau mnao-uponda huu wimbo mmeshausikia wimbo wa taifa wa Zambia?? ama wa zamani wa Namibia na Zimbabwe? kwa taarifa yenu tu huu wimbo haukuwa wimbo wa taifa wa Afrika ya kusini ingawaje ulitungwa na mmisionari mweusi wa afrika kusini (kanisa la methodist) miaka mingi kabla ya kuzaliwa ANC. Nchi ya kwanza kuutumia kama wimbo wa taifa ni Tanzania, ikifuatiwa na Zambia na hata Namibia na Zimbabwe walishawahi kuutumia. Sasa Afrika ya Kusini wanautumia nusu wakichanganya na nusu nyingine ya watu weupe.

Mtoa hoja ananikumbusha siku moja kwenye mechi ya kimataifa kati ya BafanaBafana na Nigeria mtazamaji mmoja aliitwa mbele ili aimbe wimbo wa taifa(Afrika Kusini) akashindwa na badala yake akaanza kuimba wimbo mmoja maarufu ulokuwa ukitumiwa na ANC wakati wa kupigania uhuru kwa sababu ndio aliokuwa anaufahamu vizuri ama alikuwa anaupenda zaidi!!
 
Mkuu, sio dhambi kubadili wimbo wa Taifa, kama Taifa litaona inafaa. Mabadiliko mengi hufanywa kadiri muda unapohitaji. Kwa mfano, mabadiliko ya Katiba, Bendera za nchi n.k.

Zipo nchi ambazo zimewahi kubadili nyimbo zao za Taifa. Mfano ni Afrika ya kusini na Zimbabwe. Ukitafuta taarifa zaidi utaweza kugundua kuwa zipo nchi nyingine nyingi ambazo zimewahi kufanya mabadiliko ya nyimbo zao za Taifa pia.

Kinachohotajika ni sababu tu za kufanya mabadiliko hayo. Lazima tukubali kubadilika, kurekebisha na kuboresha kila inapobidi.
Lakini pia tatizo kubwa tulilinalo mbele ya watu wa dunia nyingine Ni uafrica kwanza ndipo Tanzania.Yaani ukitaja wewe ni Mwafrica mtu hana haja ya kuuliza nchi gani.Moja kwa moja mtu hategemei jema kutoka kwako.Na hii ni kwasababu Africa tu wamaskini wa kila kitu yaani hadi upendo tunauwana ovyo. Nadhani Mungu akianza kwa kubariki Africa Then Tanzania ni jambo jema zaidi.Kumbuka Tanzania imo Africa kwaiyo mungu anaweza kuanzia hata Tanzania.
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom